Al-Jazeera: Tanzania govt relocates its capital from the port city of Dar es Salaam to Dodoma

Kwa hiyo lugha ya kusema enough resource? Unahisi yupo sahihi hapo hebu msikilieze vizuri anavyoongea broken hapo. Kweli hakuna wasomi kwenye kile chama.
Mkuu vipi wale wa elimu ya hapa na pale chadema?
 
Tanzania hatuna wanaojua nini maana ya habari na kuitengeneza, wapo wapo kama vikasuku ama bendera fata upepo.
Leo kaandika hiki, hakijaisha tayari kashakiacha na kesho kahamia kwenye lingine ...yaani ilimradi tu yeye apate ugari mezani
 
tunajua unamlenga nani kwenye hii post,nakushauri tuuu kwamba usiwachokoze tisia raa eiii
Mimi naona Mhe. Nape amajitahidi, alijibu inavyostahili, alielewa swali na akatoa jibu linaloeleweka. Nitamponda sana Mhe. Nape akifungia vyombo vya habari lakini sio kuongea kingereza kwa unyenyekevu kama aliouonyesha leo. Mhe. Nape ni mbabe sana. Alimtukana sana Dr. Slaa. leo hii alionyesha unyonge sana.
 
Uandishi wa habari ni taaluma mkuu.Sisi tunadhani unaweza ku-train mtu kwa miezi mitatu kwenye hivi vyuo vyetu fake vya uandishi habari,tena Form IV, Div.IV au hata Zero, akawa mwandishi habari mahiri,haiwezekani.Ni lazima tubadili our mindset.Hata mimi niliiona hiyo taarifa.It was good.
Leo nikiwa nimekaa mchana hapa naangalia Al-Jazeera mara nikaona makala nzuri kabisa ikiongelea serikali ya Tanzania kuhamia Dodoma.

Nilichoona na kujifunza na kushangaa ni kwamba mbna hawa watu wanakuja wanafanya makala nzuri namna hii na kitu kinachovutia kuangalia namna hii wakati huo sisi tukashindwa.

Ni hayo tu, ngoja niwape makala yenyewe.

 
Leo nikiwa nimekaa mchana hapa naangalia Al-Jazeera mara nikaona makala nzuri kabisa ikiongelea serikali ya Tanzania kuhamia Dodoma.

Nilichoona na kujifunza na kushangaa ni kwamba mbna hawa watu wanakuja wanafanya makala nzuri namna hii na kitu kinachovutia kuangalia namna hii wakati huo sisi tukashindwa.

Ni hayo tu, ngoja niwape makala yenyewe.


Kaka wageni huwa wanayaona mema yetu wakati huo sisi tunahangaika na mada za kijinga.

Jaribu kupiga picha jinsi ambavyo hiyo makala imewapatia mengi watu wa mataifa mengine duniani.

Chema cha kwetu huwa hatukioni wala hatupendi kuumiza vichwa katika kutaka kukiona, ni wenzetu wenye akili zilizofunguka ndio wanaoyaona mazuri ya kwetu.
 
Mkuu mleta uzi, faida kubwa ya hiyo makala ya Dodoma ni kuutangaza huo mkoa.

Kitendo cha makao makuu kuwa katikati ya nchi maana yake nchi inafunguliwa kwa ajili ya macho ya kimataifa.

Shughuli za ujenzi hapo zinapata soko, shughuli zote zinazohusiana na ujenzi na zenyewe hazibaki nyuma.

Tanzania nzima inafunguka zaidi kwa Dodoma kuweza kufunguka.
 
Leo nikiwa nimekaa mchana hapa naangalia Al-Jazeera mara nikaona makala nzuri kabisa ikiongelea serikali ya Tanzania kuhamia Dodoma.

Nilichoona na kujifunza na kushangaa ni kwamba mbna hawa watu wanakuja wanafanya makala nzuri namna hii na kitu kinachovutia kuangalia namna hii wakati huo sisi tukashindwa.

Ni hayo tu, ngoja niwape makala yenyewe.



bado tupo chini sana kiteknolojia, nivigumu kufananisha aljazeera na uhuru media
 
Watangazaji na marepota wetu wa TZ wanakosa credibility kwa sababu zifuatazo,

1. Wengi uelewa wao katika fani ya habari ni mdogo mno. (Huwezi walinganisha na wakenya)
2. Matumizi ya technolojia ya kisasa kwao baado kabisa (wanashindwa kwenda na wakati)
Mfano, mechi za TZ hawawezi kuweka hata summary ya magoli yaliyofungwa sson baada ya mechi, licha ya kuwa na
re-play za kila goli lakini mechi za ulaya wanaonyesha jinsi magoli yalivyofungwa.
3. Wanapeana kazi kwa misingi ya Dini (Utakuta TV moja watangazaji karibu wote ni wa dini moja) No competition, no
religious balance.
4. Wanapeana kazi kwa misingi ya Kabila - No credibility competition.
5. Ni washamba sana. Mara kwa mara mtangazaji anasoma karatasi. Kichwa chake ni up and down always!
6. Hawajui kuchangua nguo za kuvaa - Tazama TBC1.
7. Habari nyingi zina ukakasi mkubwa. mengi yanafichwa makusudi.
8. Hawana uzalendo wa nchi. i.e Hawajui namna ya kuitangaza nchi yetu.
NB: Mtu wa nje ya TZ anaweza kuitangaza vizuri nchi kuliko watangazaji wetu.

NAJUA SIJAPATIA YOTE LAKINI UKWELI NI MWINGI.
Ndiyo maana napenda kuangalia TV za Kenya.

Umeongea mule mule kabisa.
Nyongeza kidogo;
1. Sio wabunifu,Hawako tayari kujifunza new technology, ukimpatia kama Ipad /tablets /laptop ataona kama umempatia limashine moja kubwa sana duniani.
2. Wazembe na wasiopenda kujituma yaani kujua dunia inavyokwenda, hawako tayari kujisomea, from job to Bar( Mhudumu leta Serengeti moja )
3. Elimu ndogo juu ya kazi waifanyayo, mtu akiwa ana maneno mengi mengi au mwenye muonekano mzuri bila fani tayari anakuwa mtangazaji, baadae anakwenda Mwl nyerere memorial kuzuga zuga miezi kazaa anarudi ,wao wanavyuo vyao hivyo, kazi tunayo.
4. Waajiri kutotilia mkazo swala la Taaluma katika kuajiri ( hapa kuna shida kubwa).
 
Back
Top Bottom