AL JAZEERA NAIROBI? why not DAR ES SALAAM?

AL JAZEERA NAIROBI? why not DAR ES SALAAM?

Wizara ya mama Nagu inabidi watupe majibu wasitumie kodi za wana nchi bure
 
they will soon have aljazerera reprentative in dar,no worries.time will tell and sometimes shout out work
 
Mtazamo
Huo ni ushabiki ulipitiliza. Nairobi na Dar ni sawa na kulinganisha Iringa na Dar. Nairobi wako mbali sana kwa HR, miundo mbinu, na goodwill. Angalia Nairobi ukiona uwekezaji wa Tanzania Kenya ni mabango ya Waganga wa kienyeji hasa kutoka Sumbawanga.

Wanasema dalili ya uchumi kukua na pia kuonyesha nchi ni rafiki kwa wawekezaji angalia mushrooming ya Real estate Kenya -kwa kweli utashangaa hawa ma developer jinsi wanavyojenga......hata kama ni Alshababu & the CO lakini haiondoi ukweli kuwa Kenya iko mbele. Na hili halijaanza leo ni jambo la siku nyingi. Tulipokuwa wadogo Kompyuta ilifunzwa Nairobi tu. Huku Bongo ilikuwa kama lile tangazo la Haki Elimu
 
Mkuu SlidingRoof tuna sheria zinazozuia wageni kuhold share 100% kwa baadhi ya sector mfano ni sector ya habari ndio maana ile 101.4fm ya BBC enzi zilee ya Mzee wetu Mengi alikuwa na share pale.nipo tayari kusahihishwa kwa hilo ila mfano mwingine ni kwenye firm za Auditing kuna sheria inabana wageni kuhold share 100% ndio maana hata PWC wapo wazawa kule.hivyo hivyo kwenye sector ya habari.unajua ile radio ya mengi zamani 101.4fm siku izi inaitwa sky fm? nafikiri chombo huru kama al jazzera ni vigumu kuuza hisa kwa wazawa kulinda mwelekeo na msimamo wao.ukitoa ubora wa uwanja wa ndege bado sijaona vitu vingi vya kututofautisha sana na nairobi,hata wao kule wanalia Dar inavyokuja spidi kuwa the East african main Commercial City! though tunazo changamoto nyingi lakini tusijishushe sana hasa kwa hawa jirani zetu.Asante mkuu.

lete link au ushadidi

mimi nimeleta ya TIC
 
Ngoja kwanza (TISS) iwashughulikie CHADEMA then inaweza kuangalia hayo mambo(MADOGOMADOGO).
Ila pia nina wasiwasi hao ALJAZEERA wsije kukiletea matatizo chama chetu tawala kama kina Mwanahalisi.

Mkuu kama wao wanaona Chadema ni tatizo inawezekana ikawa sahihi kuwashughulikia. lakini swali ni je ni nini kina manufaa zaidi kwa taifa? TISS kazi yao hasa ni ipi when it comes to potential investments zinazoweza kuwa na manufaa kwa Tanzania. Au TISS nako umeingia uswahili kiasi kwamba kila kitu kimekuwa localized na hawajui kuwa nani ni potential investor hapa East Africa? Hivi ni kweli kwamba Tanzania haiwezi kubadilika na kuwa East African hub?

Sidhani kama kiingereza ni issue, mbona Liberia kuna native english speakers wengi kuliko kenya lakini kukon ovyo kuliko hata dar?

Naona thread imevutia watu wengi hata wa TISS tuambieni kama kweli mlijua na mlifanya nini kuhakikiasha jamaa wanakuja hapa Dar, au mnafanya ninikukakikisha kuwa kesho hatupigwi bao.
 
Who can attempt to do bussiness with people who are not serious like our leaders?Poor customer care, poor infrastructure including electricity and congested roads, watu wajanja wajanja na mafisadi, hata mimi nisingethubutu kuwekeza Dar/ Arusha wakati Nairobi ipo. Next city I would choose is Kigali!
 
Who can attempt to do bussiness with people who are not serious like our leaders?Poor customer care, poor infrastructure including electricity and congested roads, watu wajanja wajanja na mafisadi, hata mimi nisingethubutu kuwekeza Dar/ Arusha wakati Nairobi ipo. Next city I would choose is Kigali!

Mkuu ni kweli kabisa siku hizi ukisikia kiongozi anaongea unajua kabisa kuwa ni uongo, tumesikia hivi karibuni hata bajeti zinapitishwa kwa hongo. Swali ni je hali hii tunaondokana nayo vipi? TISS wanajua kuwa hayo? Kama nchi how do we start to address them? au ndio tunaendelea na siasa uchwara za udini, kutukuza vyama vetu vya siasa kuliko nchi yetu, kulinda wezi na mafisadi, na kuacha Kenya wakiendelea kupiga hatua...?

Unajua kuna baadhi ya watu wanasema Tanzania iko hovyo kwa kuwa haina wasomi inaongozwa na wasomi hewa, ni kweli hatuna wasomi? kwanini tuina mambo ya ovyo? tutayaondoaje?
 
DAR SI JIJI LA KUFANANISHA NA NAIROBI....

Tanzania bado tupo nyuma sana.. tutakujwa kuachwa na Rwanda hivihivi...
Tumesha achwa tayari na ukumbuke sisi tunarudi nyuma wakati wao wanasonnga mbele
 
Tanzania bado tupo nyuma sana kwenye maswala ya uvutiaji,wenzetu ni wajanza sana na pia wana mazingira mazuri.tumebaki kuuza ardhi tu.
 
Mkuu, yaani ubabaishaji wote huu unategemea tupate uwekezaji wa maana?!?
Umeme, maji, barabara, rushwa, ufisadi, kukosa business mindset, utapeli, nk.
 
Tanzania siyo sehemu nzuri ya kuwekeza wakati hakuna umeme, maji na miundombinu ya iana mbalimbali ni mibovu. Wanao kuja hapa ni wezi na wameshatoa 10pc inayoruhusu wizi wao angalia migodi, reli, ndege na mengine jazia
 
Wakuu nilipost thread kule kwenye jamii intelligence naona imefinywa. Ilikuwa ni kuuliza ni kwanini mashirika karibu yote yanafungua ofisi zake Nairobi na sio Mwanza, Arusha au hapa Dar es salaam? Je TISS wanakuwa na taarifa in advance kuwa jamaa wanataka kufungua ofisi hizo? wana lobby ili jamaa wafungue ofisi hizo Tanzania? Ofisi hizo ni mzingo kwa nchi au ni advantage? Najua kuna watu hapa wenye uelewa kuhusu issue hii, ni vizuri tukiwa na TISS inayendana na wakati na sio inayfanya kazi kama za miaka ya karne ya 19

bongo huwezi kuwekeza bila kutoa kitu kidogo...
 
Acha hata kufikiria kufananisha Nbi na Dar, au Kenya na TZ. Kibaya ya yote ni attitude za viongozi na watu. Bongo ujinga, uzembe, uzuzu, uvivu, wizi mchwara na udanganyifu ndiyo national pride! Elimu, kujiendeleza, kujitegemea, independence, vinapigwa vita. Hii ni zaidi ya masula mengine ya operational difficulties. Hata kama mimi Mbongo ukweli usemwe. Hakuna mtu serious atakuja kufungua afisi za kimaatifa bongo..... labda mashirika ya kutoa misaada!
 
Kama sio Nairobi hiyo idhaa ya kiswahili ingefunguliwa Adis Ababa . Dar Es Sala haina chance. Sisi tumekalia kwenye siasa tu. Nairobi and Adis ndio Hub huu ukanda wa east and horn of africa .

Technically Logistic na mambo kama ya nishati yanaiweka Dar kuwa choice ya mwisho.

Lakini ukisikia hatujui kuingia mikataba na kujadiliana ndio matokeao yake haya .Tungeweza kutumia strength yetu pamoja na mapungufu tuliyonayo.

Mfano kwa kuwa tumewauzia wanayama wetu na tumewauzia mbuga zetu kwa bei cheee basi investment zao Tanzania iwe option ya Kwanza. Kifupi Hawa jamaa wa aljazeera( Nchi yao) wana historia na tazanaia zaidi kuliko kenya. Ni kwamba tumezubaa tu. Uliza role ya Ofisi zetu za kibalozi katika masuaa kama haya .......... zeroooooo
cha ajaabu Wabunge wanalilia usawa wa kila kona (ugonjwa wa sera za ujamaa)! sasa huko Matomboni uweke barabara uvute umeme italipa vipi wakati si economic viable (yaani hamna mwenye gari (wanatumia Punda na hamna anayeweza ku-afford kutumia umeme)? unajua kama tukiwa tunafanya mambo through economic advabtages basi Dar ingepaswa iwe na wizara yako temporary kui-upgrade ifanane na mega cities (energy and infrastructurewise) kama wanavyofanya wezetu Addis Ababa na Nairobi! Cha ajabu ukisikiliza Bungeni utaskia dar isitengewe hela kwa sababu ishaendelea tuwekeze Matombo! Heheh sasa huko Matombo kuna nini zaidi ya kilimo? utalii hamna? fursa za biashara mipakani hamna! Kwanini tusiipe majiji yetu (Dar (haswaa), Mwanza, mbeya, Tanga na Arusha) upendeleo muhimu maana tukiwekeza fedha itarudi! Kuna watu na shughuli za maendeleo kule...
 
Du AL SHABAB wamefungua ofisi Nairobi mmesikia mpaka mbunge kahusishwa kuwachotea hela na msomali kawanunulia majumba mtaa mzima.
acheni kuiga kila kitu, sasa Kenya kinawa-cost hata kambi za wakimbizi walisita
 
kwa kweli, pamoja na mapungufu yote tuliyonayo hapa dsm, na kushindwa kuwavutia investors, still idhaa ya kiswahili BBC inasikilizwa zaidi na watanzania kuliko kenya, hata hii al jazeera itakuwa ivo ivo.. nadhani ni wakati muafaka sasa watanzania tukasusia kusikiliza hizi idhaa za kiswahili za nje mpaka waje TZ. Hata Kenya mgao upo...labda weather ikiwa kigezo..hapo naweza kukubaliana nao. But tusikubali kusikiliza idhaa hizi..wakitaka watangazie huko huko kama ilivyo <b>Dautch Weller</b>(DW), na Voice of America (VoA)..
<br />
<br />
Tutasusia vipi wakati zinawapatia watanzania ajira,jambo la muhimu ni sisi wenyewe kubadilika kimawazo na vitendo,the biggest problem is that we're not ready in everything,just a crying babies.
 
hii nchi kama inaweza kukaa bila umeme kwa muda wote huu,unazani ni nani atakuja kuwekeza hapa wakati hakuna umeme
 
Tanzania imekuwa nchi ya kitapeli,Rais tapeli,mawaziri matapeli,wabunge na wanasiasa matapeli,watendaji serikalini matapeli,wananchi matapeli we're all pretenders na kuishi maisha fake ambayo hayalingani na vipato halali na ndio maana tunaishia kupata wawekezaji matapeli kama RITES,Richmond,Dowans,Artumas,IPTL n.k.
 
Back
Top Bottom