Mkuu SlidingRoof tuna sheria zinazozuia wageni kuhold share 100% kwa baadhi ya sector mfano ni sector ya habari ndio maana ile 101.4fm ya BBC enzi zilee ya Mzee wetu Mengi alikuwa na share pale.nipo tayari kusahihishwa kwa hilo ila mfano mwingine ni kwenye firm za Auditing kuna sheria inabana wageni kuhold share 100% ndio maana hata PWC wapo wazawa kule.hivyo hivyo kwenye sector ya habari.unajua ile radio ya mengi zamani 101.4fm siku izi inaitwa sky fm? nafikiri chombo huru kama al jazzera ni vigumu kuuza hisa kwa wazawa kulinda mwelekeo na msimamo wao.ukitoa ubora wa uwanja wa ndege bado sijaona vitu vingi vya kututofautisha sana na nairobi,hata wao kule wanalia Dar inavyokuja spidi kuwa the East african main Commercial City! though tunazo changamoto nyingi lakini tusijishushe sana hasa kwa hawa jirani zetu.Asante mkuu.
Ngoja kwanza (TISS) iwashughulikie CHADEMA then inaweza kuangalia hayo mambo(MADOGOMADOGO).
Ila pia nina wasiwasi hao ALJAZEERA wsije kukiletea matatizo chama chetu tawala kama kina Mwanahalisi.
Who can attempt to do bussiness with people who are not serious like our leaders?Poor customer care, poor infrastructure including electricity and congested roads, watu wajanja wajanja na mafisadi, hata mimi nisingethubutu kuwekeza Dar/ Arusha wakati Nairobi ipo. Next city I would choose is Kigali!
Tumesha achwa tayari na ukumbuke sisi tunarudi nyuma wakati wao wanasonnga mbeleDAR SI JIJI LA KUFANANISHA NA NAIROBI....
Tanzania bado tupo nyuma sana.. tutakujwa kuachwa na Rwanda hivihivi...
Wakuu nilipost thread kule kwenye jamii intelligence naona imefinywa. Ilikuwa ni kuuliza ni kwanini mashirika karibu yote yanafungua ofisi zake Nairobi na sio Mwanza, Arusha au hapa Dar es salaam? Je TISS wanakuwa na taarifa in advance kuwa jamaa wanataka kufungua ofisi hizo? wana lobby ili jamaa wafungue ofisi hizo Tanzania? Ofisi hizo ni mzingo kwa nchi au ni advantage? Najua kuna watu hapa wenye uelewa kuhusu issue hii, ni vizuri tukiwa na TISS inayendana na wakati na sio inayfanya kazi kama za miaka ya karne ya 19
cha ajaabu Wabunge wanalilia usawa wa kila kona (ugonjwa wa sera za ujamaa)! sasa huko Matomboni uweke barabara uvute umeme italipa vipi wakati si economic viable (yaani hamna mwenye gari (wanatumia Punda na hamna anayeweza ku-afford kutumia umeme)? unajua kama tukiwa tunafanya mambo through economic advabtages basi Dar ingepaswa iwe na wizara yako temporary kui-upgrade ifanane na mega cities (energy and infrastructurewise) kama wanavyofanya wezetu Addis Ababa na Nairobi! Cha ajabu ukisikiliza Bungeni utaskia dar isitengewe hela kwa sababu ishaendelea tuwekeze Matombo! Heheh sasa huko Matombo kuna nini zaidi ya kilimo? utalii hamna? fursa za biashara mipakani hamna! Kwanini tusiipe majiji yetu (Dar (haswaa), Mwanza, mbeya, Tanga na Arusha) upendeleo muhimu maana tukiwekeza fedha itarudi! Kuna watu na shughuli za maendeleo kule...Kama sio Nairobi hiyo idhaa ya kiswahili ingefunguliwa Adis Ababa . Dar Es Sala haina chance. Sisi tumekalia kwenye siasa tu. Nairobi and Adis ndio Hub huu ukanda wa east and horn of africa .
Technically Logistic na mambo kama ya nishati yanaiweka Dar kuwa choice ya mwisho.
Lakini ukisikia hatujui kuingia mikataba na kujadiliana ndio matokeao yake haya .Tungeweza kutumia strength yetu pamoja na mapungufu tuliyonayo.
Mfano kwa kuwa tumewauzia wanayama wetu na tumewauzia mbuga zetu kwa bei cheee basi investment zao Tanzania iwe option ya Kwanza. Kifupi Hawa jamaa wa aljazeera( Nchi yao) wana historia na tazanaia zaidi kuliko kenya. Ni kwamba tumezubaa tu. Uliza role ya Ofisi zetu za kibalozi katika masuaa kama haya .......... zeroooooo
<br />kwa kweli, pamoja na mapungufu yote tuliyonayo hapa dsm, na kushindwa kuwavutia investors, still idhaa ya kiswahili BBC inasikilizwa zaidi na watanzania kuliko kenya, hata hii al jazeera itakuwa ivo ivo.. nadhani ni wakati muafaka sasa watanzania tukasusia kusikiliza hizi idhaa za kiswahili za nje mpaka waje TZ. Hata Kenya mgao upo...labda weather ikiwa kigezo..hapo naweza kukubaliana nao. But tusikubali kusikiliza idhaa hizi..wakitaka watangazie huko huko kama ilivyo <b>Dautch Weller</b>(DW), na Voice of America (VoA)..