AL JAZEERA NAIROBI? why not DAR ES SALAAM?

Niliwahi kusema hapa TISS ilipaswa kuwa na kitengo kwaajili ya uchumi, ona sasa Kenya walivyochangamkia Sudan Kusini sisi tumelala ukisikia tuko huko ni juhudi zetu wenyewe lakini ukweli ni kwamba hiyo nchi ina-import skilled labour sasa hivi na wanaofaidi hilo ni Kenya.

Kama tungekuwa na TISS imara kwenye economics changanya na utulivu uliopo nchini kwetu tungekuwa na mashirika mengi ya kimataifa hapa kuliko Kenya na kampuni nyingi za kimataifa, hakika ingesukuma gurudumu letu la maendeleo mbele, lakini jamaa wapo kwa kulinda viongozi mafisadi na wanatumia nguvu kubwa sana kuhakikisha mafisadi hawatoki madarakani.

Mkuu hili ni tatizo kubwa tulilonalo. Sisi outsiders hatujui wanafanya nini, wao insiders wanajua wanafanya nini. Lakini tukiangalia kwenye upande wa ulinzi wa viongozi naweza kusema wanafanya kazi yao maana tunaona mafisadi wanalindwa, lakini kwenye upande wa uchumi naona mambo ni sifuri. Ina maana hakuna kitengo kinachoshughulikia suala hili.

Clearly tunaona jinsi Kenya ilivyospearhead kujitenga kwa Sudan Kusini tayari wanaanza kupata huge benefits, sijui sisi tunafanya nini. Au ndio yale yale kujisifia kuwa kisiwa cha amani, lakisiwa kilichojaa uzembe na ubabaishaji.....
 
Niliwahi kusema hapa TISS ilipaswa kuwa na kitengo kwaajili ya uchumi, ona sasa Kenya walivyochangamkia Sudan Kusini sisi tumelala ukisikia tuko huko ni juhudi zetu wenyewe lakini ukweli ni kwamba hiyo nchi ina-import skilled labour sasa hivi na wanaofaidi hilo ni Kenya.

Kama tungekuwa na TISS imara kwenye economics changanya na utulivu uliopo nchini kwetu tungekuwa na mashirika mengi ya kimataifa hapa kuliko Kenya na kampuni nyingi za kimataifa, hakika ingesukuma gurudumu letu la maendeleo mbele, lakini jamaa wapo kwa kulinda viongozi mafisadi na wanatumia nguvu kubwa sana kuhakikisha mafisadi hawatoki madarakani.

Kama ninavyoimba kila siku uvivu wetu, ubinafsi wetu yaani sasa hivi sidhani kama tumebakiwa na wazalendo kama Nyerere au Sokoine.

Kenya sasa hivi wanajenga reli Lamu to Juba wakati sisi tunashindwa kuboresha hata reli ya kati....reli Beira to Malawi......Reli Angola to DRC.....Nchi hizi za jirani waliokuwa wanategemea port zetu ndio hivyo wanatuhama itarudi ile hali ya 1989
 
You are very right they can't come to Tanzania at all.<br />
<br />
But lets ask our-self why this is happen what should we do to make Tanzania a new commercial hub.
<br />
<br />
Why- Because we talk too much without actions,even here at JF. What should be done-stop talking too much and do act in every aspects-positively!. We will see positive results in our country.
 
Hawawezikuja huku, watu wa huku sio serious kwanza watakosha hata correspondents humu teh! Nenden kenya aljazeera
 
Kama ninavyoimba kila siku uvivu wetu, ubinafsi wetu yaani sasa hivi sidhani kama tumebakiwa na wazalendo kama Nyerere au Sokoine.

Kenya sasa hivi wanajenga reli Lamu to Juba wakati sisi tunashindwa kuboresha hata reli ya kati....reli Beira to Malawi......Reli Angola to DRC.....Nchi hizi za jirani waliokuwa wanategemea port zetu ndio hivyo wanatuhama itarudi ile hali ya 1989


Mkuu unayosema yanasikitisha sana lakini ndio ukweli. I wonder kama kweli these things mean anything to TISS, sijui kama they even care. Ukweli ni kwamba wenzetu wote wanapiga hatua sisi tukopaleple na kujidai kuwa ni kiswa cha amani kilichojaa umasiki. Sasa tunafikia mahali hata zawadi tulizopewa na mungu zinaanza kupoteza maana kwa sisi wenyewe kutozithamini.
 
mashirika haya ya utangazaji ni vigumu sana kuwa hapa Bongo hii kwa sababu kuna aina fulani ya tarifa ambazo zinatakiwa zitangazwe
  • fikiria kwa nini TIDO alifukuzwa mtu aliye kuwa na uwezo mkubwa kuisaidia nchi hii hata kama watasema mkataba uliisha , awali TIDO alisema walikubaliana kuwa ataonzewa mkataba lakini ghafra akafukuzwa, hata hivyo mbona walimu wanaongewa mikataba tena baada ya umri wa kustaafu kufika

  • angalia system ya utangazaji na aina ya habari zinazo pewa kipao mbele na mashirika ya utangazaji hapa TZ na jinsi zinavyo tangazwa je Al jazeera, BBC wataweza

  • mambo yapo mengi ambayo wenzetu walio advance hawawezi kuyafuata
 
NasDaz ndo kaandika ukweli.................huo ndo ukweli wenyewe.

Ukiangalia hapa TZ watu kama Ulimwengu, Hamza Kassongo, Mdoe, Ayoub Rioba, Kajubi Mukajanga, Susan Mungi ndo magwiji wa habari ambao wako maofisini kama wahariri, mameneja au wakurugenzi.

Sasa hawa ukienda TV hizo zingine kama CNN, Aljazeera, BBC ndo watangaji (correspondents). Sasa unategemea nini kama mwakilishi wa TBC mmoja kanda ya kati hajamaliza hata darasa la saba unategemea nini
 
WA KULAUMIWA sio TISS, bali ni mimi hapa ila naomba mnisamehe kwa wale ambao mngependelea Al_jazeera wangekuwa hapa Dar. Bosi mkuu wa Al-Jazeera alinipa kazi ya kutathimini potentiality ya Dar kama ingeweza kuwa makao makuu ya Al_jazeera kiswahili. baada ya kufanya utafiti wangu nikagundua yafuatayo ambayo niliandikia ripoti na kuipeleka kwa BIG BOSS wa Al_Jazeera:
1. Hakuna dalili ya kuwapo kwa wanaataluma kwenye tasnia ya habari wenye shahada ya uzamivu (PhD) ambao wapo kwenye game.
2.Hata wanahabari wenye shahada ya uzamili (Masterz) nao ni wa kutafuta
3.Source kubwa ya waandishi wa habari ni pale mitaa ya Ilala/Buguruni al-maarufu DSJ
4. Waandishi karibu wote ni ama Chadema au CCM na hawawezi kuficha hisia zao za ushabiki wa vyama kwenye vyama hivi
5.Source yao kubwa ya habari ni Press Conferences
6.Waandishi wengi hawavutiwi na Press Conferences zisizo na bahasha.
7. Baadhi ya waandishi hawaoni taabu kunyofoa habari za mitandao ya kijamii kama JF na kuzifanya ndio habari za kwenye vyombo vyao
8.Waandishi wengi ni vigeu geu; hawana uhuru wa maoni na hawana tofauti yoyote ile na wanasiasa! Kwamba, leo akiandikia Tanzania daima ataisifia CHADEMA na kesho akiwa UHURU ataisifia CCM! In short, ni kama waganga njaa!
9........ Hii ya tisa, sitaisema, naogopa kuwatoa watu mapovu
10. Standby generators 24/7

Baada ya kupeleka hiyo ripoti, sikupata feedbback hadi niliposikia kwamba wameamua kuwa Nairobi! Nisameheni kwa kukosa uzalendo!
hayo mambo nitaya-turn upside down endapo CNN watakuja na kunipa kazi kama hiyo tena!!!


Maskini baadhi ya watanzania kama huyu hapo juu kumbe ni mbumbumbu kiasi hiki ?
Huyu bwana anadiriki kusoma uongo 100%,Hivi tunakwenda wapi watanzania?

Jamani naomba mtambue issue moja kubwa kuwa SHERIA ya uanzishwaji wa vituo vya utangazaji kwa Tanzania hairuhususu mgeni kumliki kituo cha utangazaji kwa 100%, ni lazima awepo mzawa na ni LAZIMA mzawa awe na Share zaidi ya mgeni/wageni.Hili ndilo lilotokea kwa aljazeera kwani hawawezi kukubali kuendesha kituo wakiwa na share ya 49%.

Mambo mengine ni propaganda tu na ugoro kama aliyendika hapo juu
 
Mi ni mdau c wa kiribu sanaa wa JF, lkn ni mkereketwa wa maendeleo ya nchi yangu sanaaa! Na ndomana nalipa kodi zoote! Shida ninayo ipa wana JF, 2naongea mno na ofkoz mengi 2nayojadili humu yana mantiki, lkn, lazima 2tafute chombo cha kufanya tathmini au hata ya yale ambayo yalisha wahi kujadiliwa kuwa yalipata ufumbuzi au uta2zi maana kl cku 2takua 2na2ma kero milioni mapendekezo trilion, utekelezaji cfuri, ina maana gani? Embu kwa hili la Al jazeera 2waulize wenyewe c wana contact? Alafu 2pate majibu kesho, na c hv!
 
Kwani AL JAZEERA ina faida gani? Kama ina faida basi turuhusu pia TALIBAN waje wafungue ofisi zao hapa kwetu.
 
Maskini baadhi ya watanzania kama huyu hapo juu kumbe ni mbumbumbu kiasi hiki ?
Huyu bwana anadiriki kusoma uongo 100%,Hivi tunakwenda wapi watanzania?

Jamani naomba mtambue issue moja kubwa kuwa SHERIA ya uanzishwaji wa vituo vya utangazaji kwa Tanzania hairuhususu mgeni kumliki kituo cha utangazaji kwa 100%, ni lazima awepo mzawa na ni LAZIMA mzawa awe na Share zaidi ya mgeni/wageni.Hili ndilo lilotokea kwa aljazeera kwani hawawezi kukubali kuendesha kituo wakiwa na share ya 49%.

Mambo mengine ni propaganda tu na ugoro kama aliyendika hapo juu

Mbumbumbu ni wewe usiyeyajua mapungufu yako!!! kwa chombo kikubwa kama Al-Jazeera kuweka HQ hapa ni costful kutokana na uhaba wa HR kwahiyo hata kama sheria zingekuwa zinaruhusu bado wasingefanya hivyo kwavile wangeingia cost ya kuwa na foreigners wengi. Al-Jazeera utasema sheria haziruhusu; what about mashirika ya UN?! nayo hayaruhusiwi na sheria?! Nitajie ni waandishi wangapi TZ wana shahada za uzamili? Nitajie ni waandishi wangapi watanzania unaweza kuwaita waandishi mbele ya wandishi wa habari duniani? Au kwavile ni Al-Jazeera Kiswahili ndo unazani sifa kuu ni kujua kiswahili?! Bro, pamoja na matusi yako ukweli ndio; TZ kuna uhaba wa wanataaluma ya habari ambao ni competent na professionals! Uandishi wa habari ni zaidi ya sauti mzuri ya kutangaza bro?! Hata kama hutaki, ukweli ndio huo; kwamba wandishi wengi wanatokea DSJ; so usitarajie mtu kama huyo afanye kazi kwenye kituo kikubwa kama Al-Jazeera! najua imekuchoma, lakini ukweli ndio huo!!
 
Kumbe, hata mambo ya habari yanapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko ndani ya katiba, km mchangia mmoja alivyosema kwamba sheria ya Tz hairuhusu chombo huru toka nje, km sheria ya jinc hii ipo kwenye habari, kwenye uwekezaji mwingine kulikosa nn? Hata serikali ingeweza kucmamia share nusu km kwenye madini, kuliko ilivyo sasa, Katiba iangalie haya pia,
 
Mi ni mdau c wa kiribu sanaa wa JF, lkn ni mkereketwa wa maendeleo ya nchi yangu sanaaa! Na ndomana nalipa kodi zoote! Shida ninayo ipa wana JF, 2naongea mno na ofkoz mengi 2nayojadili humu yana mantiki, lkn, lazima 2tafute chombo cha kufanya tathmini au hata ya yale ambayo yalisha wahi kujadiliwa kuwa yalipata ufumbuzi au uta2zi maana kl cku 2takua 2na2ma kero milioni mapendekezo trilion, utekelezaji cfuri, ina maana gani? Embu kwa hili la Al jazeera 2waulize wenyewe c wana contact? Alafu 2pate majibu kesho, na c hv!
 
quote_icon.png
By NasDaz
WA KULAUMIWA sio TISS, bali ni mimi hapa ila naomba mnisamehe kwa wale ambao mngependelea Al_jazeera wangekuwa hapa Dar. Bosi mkuu wa Al-Jazeera alinipa kazi ya kutathimini potentiality ya Dar kama ingeweza kuwa makao makuu ya Al_jazeera kiswahili. baada ya kufanya utafiti wangu nikagundua yafuatayo ambayo niliandikia ripoti na kuipeleka kwa BIG BOSS wa Al_Jazeera:
1. Hakuna dalili ya kuwapo kwa wanaataluma kwenye tasnia ya habari wenye shahada ya uzamivu (PhD) ambao wapo kwenye game.
2.Hata wanahabari wenye shahada ya uzamili (Masterz) nao ni wa kutafuta
3.Source kubwa ya waandishi wa habari ni pale mitaa ya Ilala/Buguruni al-maarufu DSJ
4. Waandishi karibu wote ni ama Chadema au CCM na hawawezi kuficha hisia zao za ushabiki wa vyama kwenye vyama hivi
5.Source yao kubwa ya habari ni Press Conferences
6.Waandishi wengi hawavutiwi na Press Conferences zisizo na bahasha.
7. Baadhi ya waandishi hawaoni taabu kunyofoa habari za mitandao ya kijamii kama JF na kuzifanya ndio habari za kwenye vyombo vyao
8.Waandishi wengi ni vigeu geu; hawana uhuru wa maoni na hawana tofauti yoyote ile na wanasiasa! Kwamba, leo akiandikia Tanzania daima ataisifia CHADEMA na kesho akiwa UHURU ataisifia CCM! In short, ni kama waganga njaa!
9........ Hii ya tisa, sitaisema, naogopa kuwatoa watu mapovu
10. Standby generators 24/7

Baada ya kupeleka hiyo ripoti, sikupata feedbback hadi niliposikia kwamba wameamua kuwa Nairobi! Nisameheni kwa kukosa uzalendo!
hayo mambo nitaya-turn upside down endapo CNN watakuja na kunipa kazi kama hiyo tena!!!

Nakuunga mkono kwa asilimia 90 kwa hoja zako hapa. Ni kweli quality ya waandishi wa habari wa Tanzania inasikitisha mno. Kiwango chao ni cha chini kabisa. Hawana mwelekeo wa kuandika habari za uchambuzi zaidi ya kuelekea kuandika habari za 'reporting' and not 'analysis'. Ndio maana magazeti mengi yamejaa habari za ...fulani alisema hivi na vile. Para ya pili akizungumza jana Dar es salaam huyo alisema kwamba....

Yaani ni uandishi wa habari wa ajabu kabisa. Gazeti peke ambalo angalau linajaribu kuandika analysis ni MwanaHalisi lakini nalo siku hizi limeingiliwa na mafisadi ambao inaelekea wamelinunua ndiyo maana unaona limeanza kuwaandama akina NAPE.

Gazeti la MTANZANIA ndiyo ni la ajabu kabisa limejaa longolongo za mafisadi yaani mara elfu hata UHURU la CCM.

Kwamba waandishi wa habari wa Tanzania wamejaa ubabaishaji n i matokeo ya jamii yetu. Huwezi kuwatenga waandishi wa habari na 'society' tuliyomo. Society yetu ikoje? Ni 'society' iliyojaa uvivu; wivu; majungu; maneno mengi; rushwa; kutaka vitu vya urahisi; uswahili; mbwembwe; kujisifu kwingi pasipo maana; umbumbumbu; ulimbukeni wa kuiga watu wengine; rushwa ya wazi wazi; unafiki; ujinga. na kadhalika. Haya ndiyo baadhi ya mambo yayoididimiza Tanzania. Watu wameingia mikataba hewa na wameiba mamilioni eti wanaachiwa hivi hivi ingekuwa China wangekula risasi. Mtu kama Lowassa ameruhusu Richmond ituibie na bado anataka urahisi na wako watanzania wanaomuunga mkono. Akina NAPE wanaotaka kuisafisha CCM eti nao sasa wanaandamwa kwa kuwa tu baadhi ya waandishi wa habari wamehongwa na mafisadi na ambao baada ya kupata laki tatu tatu wanashindwa kupiga picha ya mwarabu wa richmond.

Watu wamekula UDA lakini hakuna mwandishi wa habari anayeandika kwa kina wamekulaje. Utaona blahblah tu kwenye magazeti wanakazania tu kuandika maneno ya Masaburi kwamba eti wengine wanafikiri kwa makalio. Yaani mwandishi wa habari anaona hiyo ndiyo habari na wasomaji wanaishabikia lakini siyo issues zile za kina.

Slaa naye eti anapigiwa upatu awe Rais wa nchi hii. Mbowe naye eti ni tishio kwa CCM na TUNDU LISSU ni kiboko na pia eti LEMA. waandishi wa habari ndio wanaoaandika habari za udaku na ku-swet agenda kwa mambumbumbu watanzania.


mambo ya maana ya maendeleo hayaandikwi. Huoni makala kwenye magazeti za uchambuzi wa issues. Huoni makala zinazoandika umhimu wa kuwa na reli ya kutoka Dar hadi Kigoma, makala zenye data za kiuchumi na. Huoni makala kwenye magazeti zinazochambua umuhimu wa kujenga haraka babarabara kutoka Mbeya kwenda Sumbawanga na kadhalika. Huoni makala zinazochambua kwanini hakuna sababu tena ya ujenzi wa nyumba na ofisi katika jiji la Dar es Salaam badala yake tujenge mji mpya labda huko Kimara au Kibaha au Dodoma. Utaona makala za kijinga eti WanaCCJ wahamia Mbeya na sisi wasomaji tunashabikia habari za upuuzi. In Tanzania we do not have a think tank. Hatuna watu wa kufikiri. Watalaamu wapo lakini hawapati nafasi. Ma -DC wnaoteuliwa ni wacheza ngoma baadhi yao na ukiambiwa huyu ni DC unaweza kuingia uvunguni kwa aibu. DC gani ambaye ni mwakilishi wa Rais katika eneo analoongoza hajui hata maana ya uchumi na maendeleo ya kileo? Magazeti yetu hayaandiki kwa kuwa waandishi wa habari wengi ni uchwara kama ilivyo kwa watanzania wengi. Wanyarwanda wanakuja na kuvamia nchi yetu tunachekelea. Wakenya wanakuja nchini kwetu na kuona Wanawake wetu sisi tunachekelea na these isues you cant even see them in our newspaers. The kenyans want land and to do so they use or aplly a number of methods including marriages. sasa sisi tumebaki kujisifu Tanzania ni nchi ya amani. Watanzania hatuzalishi badala yake tumebaki kuwa wachuuzi wa bidhaa za Thailand. Pita katika barabara ya Morogoro kuanzia Ubungo hadi Kibaha. Pembzoni zimejaa kiolsks za bia eti hiyo ndiyo biashara. UJINGA. magazeti hayaandiki. Nchi gani itaendelea kwa kila mtu kuwa na kosk pembezoni mwa barabara huku viti vya plastick vyekundu, kijani, njano,bluu na kila rangi vikiwa vimetanda. Singapore miaka 50 iliyopita ilikuwa kama Tanzania lakini nchi hiyo leo hii ni First world na sisi tumebaki hapa tulipo. Huko Singapore wana CCM ya huko ambayo iko madarakani tangu wakati hu. Lakini tofuati iliyopo ni kuwa CCM ya Singapore ina watu wa kufikiri tofauti na CCM ya Tanzania. Magazeti hayandiki haya tumekazania kuandika kikombe cha babu na watanzania wanapenda kusoma habari za kiombe cha babu na gamba la CCM. stupid.
 
Mi ni mdau c wa kiribu sanaa wa JF, lkn ni mkereketwa wa maendeleo ya nchi yangu sanaaa! Na ndomana nalipa kodi zoote! Shida ninayo ipa wana JF, 2naongea mno na ofkoz mengi 2nayojadili humu yana mantiki, lkn, lazima 2tafute chombo cha kufanya tathmini au hata ya yale ambayo yalisha wahi kujadiliwa kuwa yalipata ufumbuzi au uta2zi maana kl cku 2takua 2na2ma kero milioni mapendekezo trilion, utekelezaji cfuri, ina maana gani? Embu kwa hili la Al jazeera 2waulize wenyewe c wana contact? Alafu 2pate majibu kesho, na c hv!

Mkuu nimetumia mfano wa Al jazeera kwa kuwa ndio kitu recent ninachokiona. Lakini kuna makampuni mengi zaidi ya Al jazeera, ambayo yanaweza kuja hapa TAnzania lakini hayaji. Let us go to broader issues here. What do our policies say when it comes to foreign investors? Are they only on papers, are they practical? au ndio uswahiliuswahili tu as usual, wa kusema tumevutia sana wawekezaji na tumeweka mazingira mazuri wakati maji, umeme, simu hata usafiri bado ni ucharwa kabisa. Hata kama Al jazeera ni pro-taliban, how come UK, US wawaruhusu kufungua ofisi kule? let us look at our policies, if they are more anti-taliban than Talioban enemenies themselves. Issue nzima hapa ni kuwa, kuna taasisi yoyote inayofanya kazi ya kuvutia wawekezaji wa maana ambao wanaweza kutoa ajira za maana kwa watanzania na za muda mrefu na wanaoweza kulipa kodi kwa serikali? Kuna taasisi yoyote au idara yoyote inayofanya kazi ya kuangalia potential investors na kuwavuta wawekeze nyumbani? Hata kama Ole Naiko anaweza kuongea kwa sauti kubwa kama hakuna barabara, umeme, usalama, significant educated work force hakuna la maana. Even worse serikali iko mute, haisadii kuendeleza hayo.

Ingekuwa rahisi sana kuwauliza wahusika kuhusu hili la Al jazeera lakini najua jibu litakuwa siasa, halitakuwa jibu la kweli. Ndio maana nikaamua kuwauliza wadau wa maendeleo, na tujadili hali kuhusu nchu yetu kukosa vitege uchumi vya maana kutokana na uzembe wetu.
 
Smatta naona uko hapa, piga nyundo. Lakini acha ushabiki wa Ukenya na utanzania, try to be objective as you can.
 
Maskini baadhi ya watanzania kama huyu hapo juu kumbe ni mbumbumbu kiasi hiki ?
Huyu bwana anadiriki kusoma uongo 100%,Hivi tunakwenda wapi watanzania?

Jamani naomba mtambue issue moja kubwa kuwa SHERIA ya uanzishwaji wa vituo vya utangazaji kwa Tanzania hairuhususu mgeni kumliki kituo cha utangazaji kwa 100%, ni lazima awepo mzawa na ni LAZIMA mzawa awe na Share zaidi ya mgeni/wageni.Hili ndilo lilotokea kwa aljazeera kwani hawawezi kukubali kuendesha kituo wakiwa na share ya 49%.

Mambo mengine ni propaganda tu na ugoro kama aliyendika hapo juu

Mkuu tatizo sio umbumbumbu, tatizo ni kuwa na sheria mbumbumbu zinazofukuza investors. Unaweza kuniambia kwenye sekta ya madini kuna sheria hiyo? kama haipo ni kwanini? Kwanini iwe kwenye habari tu? wapi ni hasara kwa taifa? kwenye media au kwenye madini? So moja ya issues hapa ni sheria mbumbumbu na sio umbumbumbu wa sheria.
 
Wakuu nilipost thread kule kwenye jamii intelligence naona imefinywa. Ilikuwa ni kuuliza ni kwanini mashirika karibu yote yanafungua ofisi zake Nairobi na sio Mwanza, Arusha au hapa Dar es salaam? Je TISS wanakuwa na taarifa in advance kuwa jamaa wanataka kufungua ofisi hizo? wana lobby ili jamaa wafungue ofisi hizo Tanzania? Ofisi hizo ni mzingo kwa nchi au ni advantage? Najua kuna watu hapa wenye uelewa kuhusu issue hii, ni vizuri tukiwa na TISS inayendana na wakati na sio inayfanya kazi kama za miaka ya karne ya 19

Tatizo la Tanzania tunaendesha biashara kisisa, kidini na kiutamaduni. Kenya wanapofanya biashara ni biashara na ndio hoja iliyojengeka hawa jamaa kuweka kituo pale Nairobi.
Mtakumbuka Mwanahabari wa kimataifa Tido Mhando walivyomfyeka pale TBS kwa hoja za kisiasa badala ya kujali taaluma na biasahara?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom