Akina dada huu si uungwana

Kiluuj

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
692
277
Nilipokuoa ulinikuta na kila kitu.
Si vyombo,
Si vifaa,
Si bidhaa,
Vyote.
Ni vya kwangu na pengine pia wewe ila kama utakuwa wangu.

Leo tumekosana unazoa vyote na kwenda navyo kwenu!
Tena nikiwa kazini bila hata taarifa.
Vyumba vyote umesafisha!
Hata nguo zangu umebeba.

Na nyinyi wakwe hata aibu hamna?
Mtakubali vipi vyombo viingie nyumbani mwenu?
Huu ni uungwana?

Bahati yako huyo jamaa hapendi maneno mengi.
Ingekuwa mimi, SUBUTU!
 
Kwani vituo vya polisi vimefungwa?

Huyo ni mwizi na dawa ya wezi ipo....kwa nini usimpatie hiyo dawa?

Kama unaogopa basi ufunge huu uzi!
 
huyo ni jambazi sio mke,iweje achukue vitu vya mwenzake bila ruhusa,karipot polisi mkuu
 
Back
Top Bottom