Ajira yenye utata

Ajira yenye utata

Hapo kuna utapeli gani kwani?Wao kama wana pesa na wanataka kazi basi watoe Pesa wapewe kazi.Kama hawana Pesa wakatafute kazi za bure ziko nyingi sana.
Inaonekana Kwenye hiyo pesa unamgao wako
 
Unajua ni kazi gani?
Nachojua ni kwamba amaepewa masharti ya kazi,kama anaweza kuyatimiza ayatimize,kama hawezi aachane nayo.Kama ana mashaka pia aachane nayo.After all kazi za bure ziko nyingi sana.
 
Inaonekana Kwenye hiyo pesa unamgao wako
NIngekuwa na mgao ningepita kimya.Hapo naona mtu anayetaka kujifariji katika swala ambalo liko wazi.Anataka kazi,Sharti atoe Pesa.Kama kweli anataka kazi na yuko tayari kutake risk ya kutoa milioni 4 plus atoe tu ili apate kazi.Asipopata kazi basi aende polisi kuwashitaki kwa utapeli.
 
Mkuu unahangaika naye wakati naye ni miongoni kwa hao wanao taka hivyo 5M,achana naye,kikubwa mwomba ushauri aachane na hao matapeli

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu,Kama anataka kazi kwa nini asitoe hio pesa?Kama anayo io pesa kwa nini asitoe?Wakati mwingine mtu inabidi atoe kitu ili apate kitu.Ni swala la yeye tu kuwa tayari kupoteza iwapo kuna utapeli ila kama anataka kazi ambazo hulipii ziko nyingi sana aachane na hio kazi
 
Hyo 4million yote c ni ajira tosha kuliko kuajiriwa hpo,ngozi nyeusi shida mnaamini sana ujira kulko kujitaftia mwenyew ili hali unamtaji wako
 
NIngekuwa na mgao ningepita kimya.Hapo naona mtu anayetaka kujifariji katika swala ambalo liko wazi.Anataka kazi,Sharti atoe Pesa.Kama kweli anataka kazi na yuko tayari kutake risk ya kutoa milioni 4 plus atoe tu ili apate kazi.Asipopata kazi basi aende polisi kuwashitaki kwa utapeli.
Hakuna cha kupata kazi acha kumfariji ujinga hao ni matapeli
 
Kekundu kekunduuu... Wajinga ndio waliwaoo!

Hiyo hela ni almost 5m mnayo kwanza?

Kama mnayo kwa nini Asijiajiri?

Na mkiitoa wao wanamlipa kiasi gani kwa mwezi? Maana 5m is no joke aisee!

Anyway hao ni matapeliii ... kwa uzoefu wangu mwajiri anatakiwa akupe mafunzo kwa garama zake mwenyewe sio wewe utoe pesa
Ndo maana kampuni zingine kama hujui kazi utawekwa under supervision au probation for 3month ufundishwe kazi na utalipwa nusu mshahara then ukishajua ndo utalipwa mshahara mzima lakini sio wewe utoe pesa za mafunzo

Huo ni utapeli kimbia usigeuke nyuma!
 
Habari za majukumu ya kila siku ndugu zangu. Poleni na majukumu
Nielekee Kwenye mada. Nina mdogo wangu amefanya usaili katika shirika la LIVING FOUNDATION hapa Dar. Mdogo wangu amepata nafasi ya kufanya kazi Kwenye shirika, lakini ninawasiwasi huu
1. Wameambiwa watoe hela ya mafunzo 850,000/=
2. Hela ya usajiri 700,000/=
3. Hela ya kukatia visa 150,000/=
4. Hela ya tahadhari 3,000,000/=
Hela ya tahadhari inatakiwa ikae Kwenye fixed account ambapo account atakayofungua itabidi imilikiwe na shirika siyo yeye mwenye account.
Je, kwa waliowahi kufanya kazi Kwenye hili shirika kunaukweli wowote au tunataka kupigwa?
Najua humu ntapata mrejesho mzuri.
NB😛esa inatakiwa jumatatu iwe imekamilika yote.
Nawasilisha
Kampuni gani inaajiri watumishi kwa milioni nne man? Shituka
 
Hakuna kampuni yoyote duniani ambayo mwajiria anapaswa kutoa garama ya training. Matapeli hao.
 
MREJESHO WA AJIRA YENYE UTATA
Habari za majukumu ya kila siku ndugu zangu. Poleni na majukumu
Nielekee Kwenye mada. Nina mdogo wangu amefanya usaili katika shirika la LIVING FOUNDATION hapa Dar. Mdogo wangu amepata nafasi ya kufanya kazi Kwenye shirika, lakini nina wasiwasi huu
1. Wameambiwa watoe hela ya mafunzo 850,000/=
2. Hela ya usajili 700,000/=
3. Hela ya kukatia visa 150,000/=
4. Hela ya tahadhari 3,000,000/=
Hela ya tahadhari inatakiwa ikae Kwenye fixed account ambapo account atakayofungua itabidi imilikiwe na shirika siyo yeye mwenye account.
Je, kwa waliowahi kufanya kazi Kwenye hili shirika kunaukweli wowote au tunataka kupigwa?
Najua humu ntapata mrejesho mzuri.
NB: Pesa inatakiwa jumatatu iwe imekamilika yote.
Nawasilisha
Ndugu wana JF napenda kutoa mrejesho wa uzi niliouandiki kipindi cha nyuma
Ni kwamba, kamuni inayojiita living foundation kumbe ndiyo QNet, baada ya kumpa hela dogo akaenda kutoa, kilichofuata ni msoto mkali wa waisha hadi anajuta. Wajanja wameshatafuna pesa yeye kwa Sasa anahangaika kutafta wateja wengine. Mimi nimeshanawa mikono
Asanteni
 
MREJESHO WA AJIRA YENYE UTATANdugu wana JF napenda kutoa mrejesho wa uzi niliouandiki kipindi cha nyuma
Ni kwamba, kamuni inayojiita living foundation kumbe ndiyo QNet, baada ya kumpa hela dogo akaenda kutoa, kilichofuata ni msoto mkali wa waisha hadi anajuta. Wajanja wameshatafuna pesa yeye kwa Sasa anahangaika kutafta wateja wengine. Mimi nimeshanawa mikono
Asanteni
🤣 🤣 🤣 🤣 ukisoma huu uzi kunzia mwanzo, utagundua kwamba maoni 98% yalikuwa yametabiri matokeo. Ila na wewe kwa nini hukumuonya dogo baada ya kusoma maoni yetu?
 
Back
Top Bottom