Ajira yenye utata

Ajira yenye utata

Dah! Watu mna pesa asee, hivi kweli fedha zote hizo bado unawaza kuajiriwa?? Mwambieni dogo aache ufala akae chini aseti mipango ya biashara mumpe mtaji huo.

Watanzania kwanini mnapenda utumwa?
Sasa mtu anayetafuta ajira pesa yote hiyo anakuwa amepata wapi?
Kama mtatoa uje kutupa mrejesho mkuu
 
Huyo mdogo wako ana uhakika kuwa amepata kazi? Isijekuwa aliomba nafasi ya umiliki wa kampuni kwahiyo wanataka anunue hisa. 5millions kupata kazi tu?😲😲
 
Hiyo website ni ya org.. ya kichina makao yake makuu inonesha ni Hong kong na ina uhusiano na Qi ambayo ndio baba wa Qnet ambao kila siku hapa mnasema ni matapeli.

Na kama wanajitambulisha kama "living foundation" mbona address iwe kama Rhythim foundation? Something smells fishy here!
Asante mkuu kwa maoni yako nimejifunza kitu toka kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! Watu mna pesa asee, hivi kweli fedha zote hizo bado unawaza kuajiriwa?? Mwambieni dogo aache ufala akae chini aseti mipango ya biashara mumpe mtaji huo.

Watanzania kwanini mnapenda utumwa?
Sasa mtu anayetafuta ajira pesa yote hiyo anakuwa amepata wapi?
Kama mtatoa uje kutupa mrejesho mkuu
Nimekuelewa Darren2019

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ufupi tu

Kampuni inapokufanyia interview maana yake inahitaji watu. Proper company inakuwa na budget zote za kuhakikisha waliofaulu wanafanya transition ya kuwa wafanyakazi wao, kuanzia training, usafiri etc. Sasa unapoambiwa na kampuni leta pesa ya kukufundisha kazi, ujue tu una-deal na matapeli.
 
USITOE HIYO PESA ,naludia USITOE HIYO PESA Ukitoa hiyo pesa utakuwa mjinga wa karne au mbumbumbu wa taifa.
 
900k gross kwa mwezi afu utoe about 5M?? Hukupaswa hata kuomba ushauri.
Mkuu mawazo tunatofautiana sana, kunasisi ambao hatuwezi kunyumbulisha mambo au kuunganisha dots ndo maana inatubidi tuombe ushauri kwanza. Nashukuru nimekuelewa tupo pamoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za majukumu ya kila siku ndugu zangu. Poleni na majukumu
Nielekee Kwenye mada. Nina mdogo wangu amefanya usaili katika shirika la LIVING FOUNDATION hapa Dar. Mdogo wangu amepata nafasi ya kufanya kazi Kwenye shirika, lakini ninawasiwasi huu
1. Wameambiwa watoe hela ya mafunzo 850,000/=
2. Hela ya usajiri 700,000/=
3. Hela ya kukatia visa 150,000/=
4. Hela ya tahadhari 3,000,000/=
Hela ya tahadhari inatakiwa ikae Kwenye fixed account ambapo account atakayofungua itabidi imilikiwe na shirika siyo yeye mwenye account.
Je, kwa waliowahi kufanya kazi Kwenye hili shirika kunaukweli wowote au tunataka kupigwa?
Najua humu ntapata mrejesho mzuri.
NB😛esa inatakiwa jumatatu iwe imekamilika yote.
Nawasilisha
Cha?Sasa hio ni kazi au ni kazia,Kama mnazo hizo hela lipeni Ndugu yenu apate kazi.Kama hamna Pesa ya kulipa basi katafuteni Kazi za bure.
 
Visa ya kwenda wapi na corona yote hii?
Hio ni wizi.

Karibia 4mil mtapigwa pesa hio.
Weka website ya hio Kampuni.
But I can guarante you hapo kuna utapeli.
Hapo kuna utapeli gani kwani?Wao kama wana pesa na wanataka kazi basi watoe Pesa wapewe kazi.Kama hawana Pesa wakatafute kazi za bure ziko nyingi sana.
 
Back
Top Bottom