Ajira kwa kijana

Ajira kwa kijana

Sambusa sh 300/400 duuh uswahilini huwezi uza hata uweke minofu,uswazi kwa bei hiyo unapata sambusa 3/4
 
Sambusa sh 300/400 duuh uswahilini huwezi uza hata uweke minofu,uswazi kwa bei hiyo unapata sambusa 3/4

Heheheee.. Uswahilini kuna hadi mishkaki ya 100/-
Huku kwetu sambusa za viazi zinaanzia 200/-
 
Kilomita 1 unauza sambusa 5,mara sambusa 200 utakuwa umetembea kilomita 40,mara mwezi utakuwa umetembea kilomita 1,200 sawa na kuukanyaga mkoa kwa miguu.
Zikidoda huyo mama anaweza kumruhusu dogo akanywee chai asubuhi au ndo bilabila?

Mmmh kwenye kilomita hapo! hahahahahahahahahaha!
 
Mkuu mi niko interested ila niko mkoani,kama unaweza nipangishia chumba maeneo hayo hayo ya ubungo na kunilipia miezi 6,na kunipa kitanda, subwoofer, tv flat,sofa seti moja bila kusahau nauli ya mimi na mke wangu hadi dar nipo shinyanga
Kazi naweza ifanya kwa moyo wote
 
Kuongea na kuwaza ni kazi rahisi tu, hiyo laki sita inatafutwa ati! Hivi unadhani kuuza sambusa 200 kwa siku mchezo ee.

Hardwork pays. Unadhani wale wanaotembeza vyombo na ma chupa ya chai wamalipwa shillimg ngapi kwa mwezi?? Less than 260,000/- But still they do it
 
Mkuu mi niko interested ila niko mkoani,kama unaweza nipangishia chumba maeneo hayo hayo ya ubungo na kunilipia miezi 6,na kunipa kitanda, subwoofer, tv flat,sofa seti moja bila kusahau nauli ya mimi na mke wangu hadi dar nipo shinyanga
Kazi naweza ifanya kwa moyo wote

Hahahaaa.. Maelezo yako yamenifanya nichungilie kwenye avatar yako.. Nijiuliza, hutalala kama huyo jamaa??
 
Kilomita 1 unauza sambusa 5,mara sambusa 200 utakuwa umetembea kilomita 40,mara mwezi utakuwa umetembea kilomita 1,200 sawa na kuukanyaga mkoa kwa miguu.
Zikidoda huyo mama anaweza kumruhusu dogo akanywee chai asubuhi au ndo bilabila?

hahaha zikidoda wanachanganya na mpya zinarudishwa sokoni
 
Hii biashara ya kutembeza vyakula sambusa/soseji n.k watu/wateja wengi huzitilia mashaka sana hususan kiafya labda huyo mama afungue Cafe ndio aajiri kijana au awe ana supply ktk cafe kwa oda maalum.
 
Bado anatengeneza sambusa.,,mi nataka niwe nakuja kununua kwa jumla..,then niziuze mwenyewe.
 
Muuzaji atapata shilingi 100 kwa kila sambusa atayo iuza. Kwahiyo akiuza sambusa 200 kwa siku atakuwa na 20,000/- per day.
mkuu kuuza sambusa 200 kwa siku sio kazi ndogo ati
 
Back
Top Bottom