Viongozi haijali sasa kwasababu wanaoumia na kuharibiwa mali zao ni wananchi wa kawaida,wametulia kwao hawana muda kwa kujiuliza kwanini vijana hawa wenye bodaboda na wengine wanachanganyikiwa na kuchukua maamuzi kama hayo bila kuogopa serikali, hadi wengine kuingilia kufanya shughuli za ujambazi.
Wahenga wanasema usipoziba ufa utajenga ukuta,naona viongozi wamesahau kuwa mapinduzi mengi yaliyotokea hivi karibuni yamefanywa na vijana na haswa kwasababu wamekata tamaa ya maisha kwa kukosekana kwa ajira, sasa wafahamu kuwa hivi vikundi vikichoka kufanya fujo kwa wananchi, watashangaa pale watapohamia mjini kuvunja maduka, kuiba mali za watu na kufanya fujo na hapo watachodai si ajira tena bali ni mabadiliko ya serikali na watakuwa tayari kufa kama yaliotokea Tunisia.