Ajali yaua watatu Bunju B, Dar

Ajali yaua watatu Bunju B, Dar

kwanini uwezi kumsaidia?

Kuna siku jamaa alishuhudia mwendesha boda boda anagongwa na gari ya mbele yake. Ile gari ikakimbia, yeye akasimama kumsaidia, alichokipata Mungu mwenyewe anajua. Waendesha bodaboda wenzake na aliyegongwa walivyofika hawakuuliza kama yeye ndiye kagonga au ni mtoa msaada walianza kutoa kipondo kwa msamaria mwema na gari lake likavunjwa vunjwa vioo..

Twende mbele turudi nyuma, serikali inalichekea hili tatizo la wahuni wanaoendesha boda boda na wasipokuwa makini hii nchi itajenga genge la wahalifu ambao watakuwa wanaendesha nchi kuliko jeshi la polisi huku wakishambulia wananchi bila ya kusemeshwa na mtu. Nimerudia tena hapo juu, mnapoona hawa waendesha boda boda wanafikia kuvamia vituo vya polisi na kumtoa mwenzao na wakaendelea kupeta mitaani, huku ni kuwadekeza na matokeo yake sitaki kuyafikiria.

Kama kuna viongozi humu jamvini hebu lifanyieni kazi hili swala, msisubirie mpaka kiongozi mmoja wa serikali avamiwe au hali iwe mbaya zaidi ndio mu-act.
 
Wazee kama wewe ni hasara kwa taifa hili.Yani wakati wengine tunashukuru walau huku mitaani vijana wenzetu wanabangaiza kupitia hizi boda boda,wewe povu linakutoka eti ni jeshi la uasi.
Tusiwalaumu tu hawa bodaboda tutazame kwanini walifikia kuichoma moto hiyo gari.Je dereva huyo angekuwa anaendesha kwa mwendo wa kawaida hayo yangetokea?
Nimeona wengi tu humu povu likiwatoka na kulipa gari thamani kuliko roho za watu hawa wa3,v8 sidhani hata kama askari wetu wa barabarani huzisimamisha kuzifanyia ukaguzi hata wa matairi .Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni vijana hawa hawajafa katika ile staili tuloizoea ya wao kujichomeka ,dereva wa gari angekuwa kwenye mwendo wa kawaida ingesaidia.Watanzania pia tupunguze tabia ya kuchukua sheria mkononi.R.i.p bodaboda

Nina uhakika hakuna ndugu, rafiki au mtu unayemfahamu aliyekutana na hili genge la bodaboda. Nakubaliana na wewe kuwa kuna madereva wazembe ila wanachokifanya kuwapiga madereva, kuharibu magari na kuiba mali sio sahihi hata kidogo. Kuna siku boda boda iliparamia gari la mtu and wakakusanyana kama boda boda sabini hivi walimvamia yule babu wa watu wakati hana makosa na kuvunja gari lake na kumuibia kila kitu wakati kosa ni la mwendesha boda boda. Mzee yule nina uhakika alipata kilema cha kudumu.

Hili ndilo unalotaka tulitetee humu ndani? Hakuna asiyesikitika kwa watu kupoteza maisha na inawezekana kabisa waliokufa sio kati ya wale wahuni ndani ya kikundi cha waendesha boda boda but kitendo cha kuvamia na kutaka kumdhuru na probably kumuua mtu sio sahihi hata kidogo as huyo dereva sidhani kama aliua kwa kukusudia hata kama alikuwa mzembe.. Angekamatwa na kupelekwa kwenye vyombo vya dola na si vinginevyo..
 
Ni kweli Mkuu sijui niongealo, lakini hujajibu hoja yangu hata moja kiasi cha kuja na generalization,

Ajali imetokeaje? actually wote hatujui kati ya mzungu na hao madereva nani ana makosa....

Ukiiangalia picha kwa makini waliokuwepo pale si wote walikua bodaboda, na hata mleta mada amesema waliochoma gari ni WANANCHI,

Mzungu anaweza kua alikua ana makosa! unakataa? wonderful!...... amepiga risasi hewani amefaulisha mizigo yake kwenye gari nyingine akatembea anawaachia a black corpse kwa ajili ya mazishi.....

Katika Ignorant Society kama hii ya kwetu uamuzi wa haraka ilikua ni kupata mob satsfaction, nayo ni kuchoma gari hilo ......la bima ni geni kwa sisi masikini, na kwa sababu tunaamini hangechukuliwa hatua huyo mzungu then what could we do? na tunaliona gari la thamani Choma moto, hata Fergeson wanachoma moto the same!.....

Kwa hiyo Mkuu Hata kama wewe hupandi Bodaboda, wapo wanaopanda! wengi sana, hata mimi.....wapi bodaboda wapuuzi, wapo wastaarabu, tunaishi nao mtaani...

Kwa unavyowafahamu waendesha boda boda, hebu tujibu kiufasaha kabisa, uko pale ubungo au kimara kwa bahati mbaya ukagongana na boda boda (kama ni dereva mzoefu haya mambo yanawezekana kabisa kutokea hasa kwa kuzingatia uendeshwaji wa bodaboda), utasimama na kuanza kuangalia aliyevunjika mkono au aliyekufa..? Ukijibu hili swali kwa uaminifu kabisa ndio uanze kujadili...

Na kama unafahamu kanuni, mtu akishakufa humbebi tu kama inavyokuwa kwa mtu aliyejeruhiwa tu, kuna kanuni zake za kisheria la sivyo kesi inakuwa ngumu zaidi. So, itakulazimu umalize hizo taratibu huku waendesha bodaboda wakiwa wamekuzunguka wakikuimbia nyimbo za krismasi na mwaka mpya....in your dreams..!!
 
Wazee kama wewe ni hasara kwa taifa hili.Yani wakati wengine tunashukuru walau huku mitaani vijana wenzetu wanabangaiza kupitia hizi boda boda,wewe povu linakutoka eti ni jeshi la uasi.
Tusiwalaumu tu hawa bodaboda tutazame kwanini walifikia kuichoma moto hiyo gari.Je dereva huyo angekuwa anaendesha kwa mwendo wa kawaida hayo yangetokea?
Nimeona wengi tu humu povu likiwatoka na kulipa gari thamani kuliko roho za watu hawa wa3,v8 sidhani hata kama askari wetu wa barabarani huzisimamisha kuzifanyia ukaguzi hata wa matairi .Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni vijana hawa hawajafa katika ile staili tuloizoea ya wao kujichomeka ,dereva wa gari angekuwa kwenye mwendo wa kawaida ingesaidia.Watanzania pia tupunguze tabia ya kuchukua sheria mkononi.R.i.p bodaboda

Unakurupuka fikiri kwanza! Ni jeshi tarajiwa la uasi kama hawatakuwa controlled. Wanavuta bangi, wanakunywa viroba, hawajui sheria za barabarani, wanaendesha ovyo na mmoja wao akigongwa hata kama ndiye mwenye kosa wenzake watakusanyika na kufanya uharibifu. Wewe cku ukiwa na gari ukamgonga bodaboda ndo utanielewa. Binafsi sijapinga aina hiyo ya ajira but nataka mabadiriko. Serikali iangalie namna ya kuwa-handle. Pili serikali iweke idadi ya bodaboda zinazopaswa kuwa barabarani badala ya kuacha kila mtu ajinunulie bodaboda na kuiingiza barabarani.
Halafu bodaboda sio ajira pekee kwa vijana. Think big!!!
 
GAUTAMA usirukie hoja usizozifahamu. Soma comments za watu. Mwenzako kawa tagged ili ajibu na bado yupo kimya, wewe wakurupuka tu.

Hizo Assumptions ulizokua unazitaka kwa kuniquote mimi ulimaanisha nini? watu wengine bwana.....
 
Back
Top Bottom