Ajali ya Meli: Kikwete na hoja ya upimaji DNA

mi nilicheka vibaya sana....anadhani kupima dna ni kama kupima kinyesi kujua kama mtu ana amoeba au hana..jk bwana

kwani dna sikama watu wameungua wamehibika kiasi hujui nani ni nani.

ila tusilaumu ndio taabu ya kutaka umaarufu kwa viongozi wetu.
 
mie ngoja ncheke tu mie huleeee huleeeeeeeeeeeeeee huleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
Aisee kumbe Jk alitoa hiyo ya DNA? Hiyo ni kali kwa kweli. Yeye anadhani kama anavyotamka DNA kwa urahisi kwa herufi tatu basi hata matumizi ya sayansi na technologia yake yatakuwa rahisi. Halafu raisi mwenyewe hatumii hata logic; nchi iliyo bado kwenye matatizo ya giza itawezaje kuwa na advanced fingerprinting techniques kama za DNA?

Mimi nijuavyo, hata hicho kipimo hicho cha DNA kinahitaji utaalamu wa hali ya juu wa watu watakaoweza kufanya mahesabu ya kistatistics ili kutenganisha huo mfanano wa DNA na kutambua ni yupi hasa ndugu wa karibu bila makosa yoyote ya kiufundi. Wanatakiwa highly technically trained molecular geneticists; na Tanzania hapa ninavyofahamu hakuna mtu hapa kwenye hizo fani, achilia mbali hivyo vifaa vya kuweza kuziisolate,kuzifragment, kuziamplify na kuzilinganisha sawa kwa sawa kuona wapi kwenye mfanano au vipi; Sasa shule zenyewe za bongo ni mkopo wa shilingi 5000 na wenyewe serikali wanaona wamekusaidia kwelikweli halafu anatokea zuzu mmoja na kusema majukwaani eti waliozama wapimwe DNA,tuna rais rahisi kweli kweli!!!
 
On a serious note..this is really embarassing!!..
yaani huu ni umbumbumbu!! inaelekea pamoja na kiburi cha kutohitaji au kutotumia ushauri wa kitaalam ya nini cha kuongea kwenye masuala sensitive ya kitaifa/muungano/kimataifa, huyu inaelekea hajishughulishi walau kuendeleza uelewa/knowledge yake kwa kusoma na kufuatilia matukio muhimu katika source mbalimbali ambazo kama rais nina uhakika kuwa ana access nazo 24/7. Kwa akili hizi sijui ataandika nini..Inshallah, Mungu atupe uzima, tunangoje kwa hamu memoirs yake..haya ndiyo atatakiwa kayazungumzia..maana ni history
 
Nadhani ni wazo zuri sana na litasaidia kuharakisha utambuzi wa maiti. Magwanda sidhani kama kuna sababu ya kupinga kila kitu. Vitu vingine muwe mnapima na kuona uzito wake. Hiki ni kipindi kigumu sana kwa taifi lakini nyie mnazidi kuwabeza waliopoteza maisha, eti wasitumie DNA.
 
Aisee kumbe Jk alitoa hiyo ya DNA? Hiyo ni kali kwa kweli. Yeye anadhani kama anavyotamka DNA kwa urahisi kwa herufi tatu basi hata matumizi ya sayansi na technologia yake yatakuwa rahisi. Halafu raisi mwenyewe hatumii hata logic; nchi iliyo bado kwenye matatizo ya giza itawezaje kuwa na advanced fingerprinting techniques kama za DNA?

Mimi nijuavyo, hata hicho kipimo hicho cha DNA kinahitaji utaalamu wa hali ya juu wa watu watakaoweza kufanya mahesabu ya kistatistics ili kutenganisha huo mfanano wa DNA na kutambua ni yupi hasa ndugu wa karibu bila makosa yoyote ya kiufundi. Wanatakiwa highly technically trained molecular geneticists; na Tanzania hapa ninavyofahamu hakuna mtu hapa kwenye hizo fani, achilia mbali hivyo vifaa vya kuweza kuziisolate,kuzifragment, kuziamplify na kuzilinganisha sawa kwa sawa kuona wapi kwenye mfanano au vipi; Sasa shule zenyewe za bongo ni mkopo wa shilingi 5000 na wenyewe serikali wanaona wamekusaidia kwelikweli halafu anatokea zuzu mmoja na kusema majukwaani eti waliozama wapimwe DNA,tuna rais rahisi kweli kweli!!!

Mkuu, mchango wako umenigusa..naomba nisema kwamba hapo nilipo-bold na ku-underline ukweli ni kuwa tuna Watanzania kadhaa wazuri tuu ambao wamebobea kwenye hii fani..wengi wametapakaa humu duniani katika kusaka mkate na asali ya kila siku..
 
Mkuu, mchango wako umenigusa..naomba nisema kwamba hapo nilipo-bold na ku-underline ukweli ni kuwa tuna Watanzania kadhaa wazuri tuu ambao wamebobea kwenye hii fani..wengi wametapakaa humu duniani katika kusaka mkate na asali ya kila siku..

Ni kweli wapo watanzania baadhi ambao wakiwezeshwa tu kidogo tutaona mabadiliko makubwa sana katika kila eneo muhimu la kimaendeleo.
 
Nadhani ni wazo zuri sana na litasaidia kuharakisha utambuzi wa maiti. Magwanda sidhani kama kuna sababu ya kupinga kila kitu. Vitu vingine muwe mnapima na kuona uzito wake. Hiki ni kipindi kigumu sana kwa taifi lakini nyie mnazidi kuwabeza waliopoteza maisha, eti wasitumie DNA.
Mwita25,
alitakiwa walau ashauri madaktati wachukue sample (ambapo hata unywele mmoja unatosha) kwa kila victim incase DNA matching ikihitajika ifanyike baadae endapo wazazi/ndugu au jamaa wa karibu watajitokeza kwa utambuzi. Lakini kwa mazingira yetu, pamoja na tukio lenyewe, picha ya marehemu ina uzito zaidi na ndiyo njia nafuu na rahisi zaidi ya utambilisho wa marehemu kwa wazazi/ndugu/jamaa au marafiki.
 
Nadhani ni wazo zuri sana na litasaidia kuharakisha utambuzi wa maiti. Magwanda sidhani kama kuna sababu ya kupinga kila kitu. Vitu vingine muwe mnapima na kuona uzito wake. Hiki ni kipindi kigumu sana kwa taifi lakini nyie mnazidi kuwabeza waliopoteza maisha, eti wasitumie DNA.
<br />
<br />

Mbona tayari yamesemwa mengi tu kuhusu technology ya DNA hapa Tz, bado hujaelewa tu, au ni lazima utetee kila kitu kinachohusu magamba, badilika kidogo basi ndugu yangu au ni kweli mnalipwa kwa post?
 
Nijuacho mie DNA ya utambuzi ni lazima pawe na data base inayokuwa ama ina taarifa ya mtu anayepimwa, ama wajitokeze baba na mama mzazi wa mpimwaji wapimwe wao kwanza na ndipo na huyo marehemu apimwe ili kuona common genes. Sasa huyu jamaa anaibuka na kusema 'wapimwe DNA' hivi wajameni huyu mtu ana nini kichwani, ama niulize hivi... hivi hana washauri wanaompa jinsi ya kuongea mbele ya kadamnasi? Rais asione haya kufundishwa speech na namna ya kuongea na hadhira, wote huwa wanapewa darasa huwezi ku win hadhira kama unaongea vitu ambavyo havipo duniani.

Huyo ni haambiliki na kwa umri alionao hakuna wazo ama kitu kipya kinaweza kupenyezwa kwenye ubongo wake!!!, Kilichobaki kwa Wadanganyika ni kulia na kusaga meno labda tuthubutu kuamua vinginevyo kama inavyotokea kwa wenzetu.
 
Siku kadhaa zimeshapita na miili yote hata ile isiyotambuliwa tayari imeshazikwa bila kutambuliwa which means upimaji wa DNA haukufanyika.
Jk anajisikiaje?
 
Pamoja na kwamba sielewi vizuri upimaji wa DNAs, nilihisi kabisa kuna kitu hakiko sawa kwenye kauli ya mheshimiwa. Nikajiuliza, wakishafanya hiyo DNA, halafu watalinganisha na wapi ili kujua nani ni nani? Au wa-TZ wote tutafolenishwa kupimwa ili hiyo comparison ifanyike?
 
Back
Top Bottom