Ajali ya chopa: Kamanda Kova ameonesha udhaifu

Ajali ya chopa: Kamanda Kova ameonesha udhaifu

Sio kukuimbia tu, kama ni ziwani basi Dr Bilali angenyang'anywa boya au kukabwa na Kova kuvaa boya na kujiokoa.
Very creative aisee!... Huu ni ukweli kabisa!... Kova halindi mtu ila yeye binafsi!
 
Fikirieni kwanza ndege sio Kama baiskeli eti utaruka Subutu waulize ni marehemu wa ajali ya ndege Malaysia
 
Kumbe na viongozi wanaogopa kufa!:smile-big:
 
Wewe Martini, Kova hakuruka wala nini. Kwa mafunzo yepi alonayo hadi awe wa kwanza kuruka????????????????????? Huyo ni mzee wa kutunga kwa hiyo ukitaka habari ya uhakika muulize DKT bilali ndo mkweli. natamani wakati anaruka angekutana na panga boi la chopa sijui angesimuliaje.
 
Jana katika vyombo vya Habari na magazeti ya leo Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova amenukuliwa ‘akijigamba’ kuwa alikuwa wa kwanza kuruka kutoka katika Helikopita iliyopata ajari.

Ndani ya ndege hiyo alikuwemo Makamo wa Rais Dkt. Bilal, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi Dkt, Magufuli na watu wengine.


Napata shida sana kumuelewa Kova. Atawezaje kutoka ndani ya chopa na kumuacha Makamo wa Rais? Watawezaje kutoka kwenye ndege na kumwacha Mkuu wa Mkoa ambaye ndie mwenyekiti wake wa Kamati ya Ulinzi na Usalama?

Jambo hili analoliona kwake ni ujasiri ni fedheha kwa askari. Ni raia tu (ambaye hajapa mafunzo ya kijeshi) anaweza kufanya hivi na kasha kujisifu kuwa nijasiri.

Kwa hiyo wewe ulitaka amrushe makamu wa rais? Au amrushe mkuu wa mkoa? Kama askari katika ishu kama hiyo alionyesha njia. Tunarukaga hivi
 
kama ndivyo, siku tukiingia kwenye machafuko makubwa viongoz wetu siwatatukimbia halafu wajisifu wao mashujaa!?
 

Jambo hili analoliona kwake ni ujasiri ni fedheha kwa askari. Ni raia tu (ambaye hajapa mafunzo ya kijeshi) anaweza kufanya hivi na kasha kujisifu kuwa nijasiri.

Masoja wanakamsemo ka dharau 'polisi ni raia wakakamavu'

Kama kuna kaukweli
 
Pia alisikika akitoa kilio "jamani njooni mtuokoee!"
 
Maswali mawili kabla ya kumlaumu: was he part of the delegation or security detail?? Mkuu hakuwa na mlinzi wake??

Nami nilikuwa najiuliza hivi makamu wa rais hana bodyguards, very strange
 
Yuko sahihi kuruka wa kwanza kama ilikuwa ni sabotage at least angekuwa wa kwanza kujitoa muhanga, hakuna aliyejua ni nini kimetokea je ni chopper kuharibika au imechezewa,
 
Wana JamiiForums mbona tu-wasahaulifu hivyo kuhusu Kamanda Kova wakati wa ziara ya Obama Tanzania maafisa Usalama wa Marekani walizuka Ofisini kwa Kamanda Kova kutokana na kukosa imani kama anafuata maadili.

Sasa tunadhani Usalama wa Taifa Tanzania wanaomlinda Makamu wa Rais wafanyeje? labda wlimwona Kamanda Kova kapanik kiasi cha kusababisha uokozi wa Bilali kuwa mgumu na hivyo Kamanda Kova akalazimishwa kuruka kwanza ili hali iwe shwari ktk zoezi la uokozi la vigogo...... Source: Makao Makuu Kanda Maalum ya Kipolisi DSM

Ofisa mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), akiwa na mbwa wakati za ziara ya Obama Tanzania aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya ukaguzi. "Walikwenda moja kwa moja mapokezi wakafanya ukaguzi, kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka," alisema polisi huyo na kuongeza:

"Licha ya mimi kutokuwa na cheo pale, lakini hili la kutukagua na mbwa, ni kama wametudhalilisha... sisi ndiyo tunaaminika kwa usalama, leo hii wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu."

 
Akili za hao watu zimeshaharibika hata wasijue cha kufanya au kuongea linapokuja suala la muhimu na hatari, akili yao imebakia kwenye kudhibiti chadema , kutesa wanaharakati na kuua raia wasio na hatia.
 
Back
Top Bottom