No thank you! Naomba nitofautiane na wewe. Nadhani sote tunamkumbuka au tumewahi kusika habari za Lt. Col. Yonatan Netanyahu. Huyu alikuwa KAMANDA (au KIONGOZI) wa makomandoo waliohusika kuvamia Entebe, July 4, 1974 kuwaokoa mateka wa ki-Israel waliokuwa wametekwa na utawala wa Idd Amin.
Kwa nafasi yake (Netanyahu), ungedhani labda angekuwa mtu wa kulindwa lakini haikuwa hivyo, badala yake alikuwa mtu wa mwisho kuondoka kwenye tukio jambo lililosababisha kifo chake. Huyu alijua wajibu aliokuwa nao na sio mwingine bali kumwokoa hadi yule raia wa mwisho masikini kabisa na alitimiza wajibu huo ipasavyo bila kujali hatari iliyokuwa ikimkabili.
Leo, Kamanda Kova yu na Makamu wa Rais na viongozi wake wakuu badala ya kuwa mlinzi anakuwa wa kwanza "kujiokoa" akiwaacha wakuu wake "wakiteketea". Hao ndio maaskari wetu tuliowakabidi dhamana ya uhai wetu. Kama kwa viongozi kafanya hivyo, hivi sisi makapuku atatufanyiaje? Vyeo nchi hii ni kujaza matumbo tu badala ya wajibu wa msingi tunaopaswa kuutimiza.
Dhima ya Jeshi la Polisi ni "kuhakikisha usalama wa raia na mali zao"; ha ha ha! Kova mfano bora wa kuepukwa.