Ajali ya chopa: Kamanda Kova ameonesha udhaifu

Ajali ya chopa: Kamanda Kova ameonesha udhaifu

Ni lazima awe wa kwanza kutoka ili atake cover kama kuna adui aliitungua hiyo helkopter.
Ukimtoa kiongizi mkubwa kama vice presedent halafu akapigwa chuma nje itabidi askari ajifiche ndani then yeye akapona atajibu nini?
Kova ni askari wa zamani hakuingia jeshini kufuata mshahara tuu.Askari anakua wa mwisho kutoka kama kulikua na mechanical defects kwenye helkopta na taarifa ilishatolewa na rubani.
 
No thank you! Naomba nitofautiane na wewe. Nadhani sote tunamkumbuka au tumewahi kusika habari za Lt. Col. Yonatan Netanyahu. Huyu alikuwa KAMANDA (au KIONGOZI) wa makomandoo waliohusika kuvamia Entebe, July 4, 1974 kuwaokoa mateka wa ki-Israel waliokuwa wametekwa na utawala wa Idd Amin.

Kwa nafasi yake (Netanyahu), ungedhani labda angekuwa mtu wa kulindwa lakini haikuwa hivyo, badala yake alikuwa mtu wa mwisho kuondoka kwenye tukio jambo lililosababisha kifo chake. Huyu alijua wajibu aliokuwa nao na sio mwingine bali kumwokoa hadi yule raia wa mwisho masikini kabisa na alitimiza wajibu huo ipasavyo bila kujali hatari iliyokuwa ikimkabili.

Leo, Kamanda Kova yu na Makamu wa Rais na viongozi wake wakuu badala ya kuwa mlinzi anakuwa wa kwanza "kujiokoa" akiwaacha wakuu wake "wakiteketea". Hao ndio maaskari wetu tuliowakabidi dhamana ya uhai wetu. Kama kwa viongozi kafanya hivyo, hivi sisi makapuku atatufanyiaje? Vyeo nchi hii ni kujaza matumbo tu badala ya wajibu wa msingi tunaopaswa kuutimiza.

Dhima ya Jeshi la Polisi ni "kuhakikisha usalama wa raia na mali zao"; ha ha ha! Kova mfano bora wa kuepukwa.
Kuna mtu aliewahi kukuambia kuwa Kova ni komandoo?
 
Kova hapo sasa yeye hakuingia kwenye hiyo ndege kama mlinzi was makamo was Raised.
 
Askari anatakiwa ajiokoe kwanza ndipo aokoe wengine
 
La kujiuliza ni Je yeye alikuwa ni mlinzi wa huyo Bilali ? Afu kufa si mchezo ,yaani ka ingekuwa imepaa kama mita tano tu basi bunge lingekuwa limeahirishwa ,tatizo deleva alikuwa amechanganyikiwa hajui rivazi ,alizani anaenda mbele kumbe ameweka gia ya rivazi.
IMG-20140414-WA0000-564x272.jpg
 
Jana katika vyombo vya Habari na magazeti ya leo Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova amenukuliwa ‘akijigamba’ kuwa alikuwa wa kwanza kuruka kutoka katika Helikopita iliyopata ajari.

Ndani ya ndege hiyo alikuwemo Makamo wa Rais Dkt. Bilal, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi Dkt, Magufuli na watu wengine.


Napata shida sana kumuelewa Kova. Atawezaje kutoka ndani ya chopa na kumuacha Makamo wa Rais? Watawezaje kutoka kwenye ndege na kumwacha Mkuu wa Mkoa ambaye ndie mwenyekiti wake wa Kamati ya Ulinzi na Usalama?

Jambo hili analoliona kwake ni ujasiri ni fedheha kwa askari. Ni raia tu (ambaye hajapa mafunzo ya kijeshi) anaweza kufanya hivi na kasha kujisifu kuwa nijasiri.

Nadhani wewe ndiye huelewi. Katika ajali huwezi kuanza kumsaidia mtu wakati na wewe unatakiwa ujiokoe. Ndiyo maana hata kwenye ndege wanasistiza jiokoe kwanza wewe (kama alivyoruka Kova) halafu angalia uwezekano wa kuokoa wengine. Nakupa pole sana kwa uelewa wako mdogo, na hili si tatizo lako bali ni tatizo la watanzania walio wengi kwani wengi hatujui kanuni za dharula.
 
Mmmmmh jaman munakijua kifo nyinyi hata kama ningekuwa mm kama mwanya upo naruka vizuri tu uhai kunoga nyinyi
 
Tofautisha kati ya kamanda name komando Kova ni kamanda so komando. Alijiokoa kwanza kabla ya wrote. Salsa we we ulitaka aanze kumwokoa kikongwe?
 
Huwezi kuokoa ukiwa kwenye janga, lazima wewe mwenyewe uwe salama, nje ya janga ndipo uweze kuokoa. Ila sijui kama kamanda aliruka kwa ajili hiyo, inawezekana ni woga!
 
Jana katika vyombo vya Habari na magazeti ya leo Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova amenukuliwa ‘akijigamba’ kuwa alikuwa wa kwanza kuruka kutoka katika Helikopita iliyopata ajari.

Ndani ya ndege hiyo alikuwemo Makamo wa Rais Dkt. Bilal, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi Dkt, Magufuli na watu wengine.


Napata shida sana kumuelewa Kova. Atawezaje kutoka ndani ya chopa na kumuacha Makamo wa Rais? Watawezaje kutoka kwenye ndege na kumwacha Mkuu wa Mkoa ambaye ndie mwenyekiti wake wa Kamati ya Ulinzi na Usalama?

Jambo hili analoliona kwake ni ujasiri ni fedheha kwa askari. Ni raia tu (ambaye hajapa mafunzo ya kijeshi) anaweza kufanya hivi na kasha kujisifu kuwa nijasiri.

jeshini kuna kitu kinaitwa USALAMA WANGU KWANZA.
 
Aliwahi kuipigia saluti maiti ya Kanumba!

Wengi msiopitia angalau JKT hamlifahamu hili,mwanajeshi kusalute kwa mwili wa marehemu ni lazima,sio ombi.Hapo haijalishi aliekufa ni nani,mtoto,mzee,mkulima,mwanajeshi,mkaanga chipsi n.k(salute ni lazima).
 
Mkuu Lukosi, hapa mleta maada sio kwamba anamCondemn Kova, most of us would have done the same, tatizo ni kujisifia kuwa katoka wa kwanza, ingekuwa busara kama angekaa kimya, but kujisifia huko wakati yeye aliapa kuwa shield, kuwalinda raia kwa maisha yake ni bonge la udhaifu na inaonesha ni kiasi gani kakosa busara.

Well said, Inashangaza watu wanashindwa kuelewa hili kwa urahisi kabisa. Yeye Kova kujigamba kwenye TV kwamba katoka nduki wa kwanza hiyo ndio haiingii akilini. Angekauka tu.
 
Hapo kila mtu alikua anatetea maisha yake chezea kifo wewe. Hapo kila mmoja alikua na ulinzi wake.

Askari yeyote hana sababu ya kumwacha Mkuu wake kwenye hatari. Yeye alitakiwa kuhakikisha Wakuu wake ( Mkuu wa mkoa na Makamu wa Rais) wako salama na siyo kukimbia. Huo ni wajibu wake kama askari siyo ombi maalum.
 
Jana katika vyombo vya Habari na magazeti ya leo Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova amenukuliwa ‘akijigamba’ kuwa alikuwa wa kwanza kuruka kutoka katika Helikopita iliyopata ajari.

Ndani ya ndege hiyo alikuwemo Makamo wa Rais Dkt. Bilal, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi Dkt, Magufuli na watu wengine.

Napata shida sana kumuelewa Kova. Atawezaje kutoka ndani ya chopa na kumuacha Makamo wa Rais? Watawezaje kutoka kwenye ndege na kumwacha Mkuu wa Mkoa ambaye ndie mwenyekiti wake wa Kamati ya Ulinzi na Usalama?

Jambo hili analoliona kwake ni ujasiri ni fedheha kwa askari. Ni raia tu (ambaye hajapa mafunzo ya kijeshi) anaweza kufanya hivi na kasha kujisifu kuwa nijasiri.

Mkuu elewa mambo ya usalama yanaanza na usalama wako kwanza ndipo inafuata usalama wa watu wengine!! Role ya Kova Haikuwa Bodyguard ! Zaidi ya Yote Kova alikuwa Bonge la Goalkeeper mzuri sana Enzi zake!!! No hard feelings Mkuu, Jaribu kujenga hoja imara ya kudiss siyo hii ...
 
swali la kijinga sana

weee kwenye kifo utaweza kupata muda wa kufikiria mwenzako?

Hata unaposafiri na ndege wanasema jisaidie kwanza wewe halafu ndio uwafikirie wengine, ingelipuka unadhani kungekuwa na muda wa kubebana?

Kama huamini ngoja yakukute ndio utajua kuwa ajali sio mchezo na akili yako haiwezi kuwa sawa kwa sababu lazima uchanganyikiwe labda uwe komando...

we nawe sk moja moja utumiage akili, umeambiwa suala siyo kujiokoa yeye,suala hapa ni kitendo cha kova kujisifu ujinga,angebaki kimya.
 
Back
Top Bottom