Ajali mbaya Mbezi Afrikana

Ajali mbaya Mbezi Afrikana

Natamani waliofariki isiwe ni mke na mume. Najaribu kuwaza kuhusu watoto wao ikiwa ni hivyo. Mungu awape faraja wafiwa
Hata kama ningepiga picha gari si rahisi kutambua namba. Imeungua yote vibaya sana. Inaonyesha dereva alikuwa anaomba msaada kwa kunyoosha mkono lakini ilishindikana kupata msaada kwa sababu after impact iliwaka ghafla.
Picha huwa muhimu kwani namba za gari zingesaidia kujua gari la nani hujatoa taarifa kamili mkuu

ungepiga picha gari tu
 
Jamani watz wenzangu, tusiendeshe tukiwa tumelewa,hata kama tunaharaka jaribu kutuliza akili yako ukiendesha, kagua gari yako kabla ya kutoka,usitembee speed zaidi ya 50 kwenye watu/magari mengi, R.I.P.
 
picha ni muhmu sana,wazee wetu wasingepga picha matukio ya nyuma tungeyajua vp? Achen uhuni,maiti ni kama mwili tu msiogope ni kitu cha kawaida
 
Asilimia kubwa watanzania huwa tuna drive magari tukiwa tungi mbaya?mtu akiulizwa anakujibu oh mm mzoefu
Jamani watz wenzangu, tusiendeshe tukiwa tumelewa,hata kama tunaharaka jaribu kutuliza akili yako ukiendesha, kagua gari yako kabla ya kutoka,usitembee speed zaidi ya 50 kwenye watu/magari mengi, R.I.P.
 
Majira ya saa kumi na moja asubuhi kumetokea ajali mbaya sana eneo la Mbezi Beach Afrikana.

Gari aina ya Nissana xtrail au Honda ikiwa inatokea Mwenge imegonga kwa nyuma truck na kuungua hapohapo.

Kwa mujibu wa mashuhuda watu wawili waliokuwemo ndani ya gari wamefariki kwa moto wakiwa ndani.

Kwa adabu zangu sitoweza kuweka wala sikupiga picha.
Ulipaswa kupiga picha,kama watazamaji wangekuruhusu. Usiwe squeamish. Unaifahamu Aztec religion? Kupiga picha maana yake you are recording history. Siyo kama hawa lasses ambao wanapiga picha kila baada ya siku mbili Facebook wamevaa nguo tofauti. Wana nguo nyingi kama Imelda Marcos.
 
Hiyo barabara kutoka hapo Afrikana mpaka njia panda ya wazo sijui kuna kiumbe gani kimefichwa kwa chini
 
Muhimu ni kuinua mikono yetu kumuelekea Muumba wetu na kushukuru...kwani kila nafsi itaonja u mauti na kwake sisi tutarejea.Tumuombe Mungu awasemehe makosa yao na sisi pia.
 
So sad indeed, haya Maisha Mungu pekee ndie anaejua

SIP loved ones
 
Tukubaliane na sababu zake kwanza...hivi gari ikilipuka moto watu huwa inakuwaje kuhusu milango....
Milango ni chuma /bati,ikipata moto inatanuka,pia kumbuka iligonga kwa nyuma so inawezekana pia milango ilipinda so huwezi fungua,labda useme fire extingusher,labda japo kwenye magari watu wanaziweka kwenye buti alafu inafungiwa na kofuki inapata kutu so kwenye ajali huwez fungua
 
Hiyo barabara kutoka hapo Afrikana mpaka njia panda ya wazo sijui kuna kiumbe gani kimefichwa kwa chini
Hakuna kilichofichwa, madereva wanaendesha kwa spidi sana bila uangalifu. Usisahau hiyo barabara inapitisha wafanya tafakuri wengi kama mimi.......hasa usiku mkubwa
 
Majira ya saa kumi na moja asubuhi kumetokea ajali mbaya sana eneo la Mbezi Beach Afrikana.

Gari aina ya Nissana xtrail au Honda ikiwa inatokea Mwenge imegonga kwa nyuma truck na kuungua hapohapo.

Kwa mujibu wa mashuhuda watu wawili waliokuwemo ndani ya gari wamefariki kwa moto wakiwa ndani.

Kwa adabu zangu sitoweza kuweka wala sikupiga picha.

Nilidhani JINI Lililozoeleka Hapo Mbezi Beach Afrikana Lilishaondolewa Kumbe Bado? Tutegemee AJALI Hizi Kila Mara! Huwa Linapenda Sana Kukaa Hapo Africana au Makonde Karibu Na Kwa Yule Mpemba Mwenye Mbuzi Wengi Wanaojichunga Wenyewe Na Lugalo / Makongo Kituo Cha Supa. SIFA Yake Kubwa Ni Kusababisha AJALI Isiyotegemewa, Kali Na Yenye Madhara Makubwa Na Wajuvi Nao Wanasema Kuwa Hata Ile AJALI Mbaya Ya Bagamoyo Lilikuwa Ndiyo Lenyewe. Tupende KUSALI Sana Huku Tukiwa Makini Uwapo Na Gari Hasa Hayo MAENEO Hatarishi Matatu Niliyoyataja.
 
Back
Top Bottom