Ajali mbaya Mbezi Afrikana

Ajali mbaya Mbezi Afrikana

Hiyo barabara kutoka hapo Afrikana mpaka njia panda ya wazo sijui kuna kiumbe gani kimefichwa kwa chini

Halafu Huwezi Amini Hicho Kipande Kina MAKANISA Mengi YALIYOTUKUKA Kimaombi Sasa Sijui SHETANI Huyo Kawashinda Na Nguvu Zao Wamezielekeza Tu Kutudai SADAKA, DHAKA Na FUNGU LA KUMI Ambapo Usipotoa Hubarikiwi Ng'o!
 
barabara kati ya mwenge na tegeta usiku inaua sana na hii inatokana na giza kali kwenye njia hiyo taa zinahitajika kumwezesha dereva kuona pande zote za barabara
Mkuu nakubaliana na wewe kuwa taa zinahitajika, lakini kutii sheria za barabarani nalo ni jambo la muhimu. Ile barabara imewekewa speed limit ya 50/60 (kama sijakosea,) lakini watu wanakimbia kwa speed kubwa sana na bila sababu za msingi, hata Morogoro Rd nayo ina vibao vya speed limit ya 50, lakini wanaoheshimu hilo ni wachache sana. Kwa tabia yetu ya kutokutii sheria haya majanga ni ndoto kuyamaliza. Huyo angekuwa anaenda mwendo unaoruhusiwa kisheria naamini madhara yangekuwa madogo sana pamoja na giza lililokuwepo. Anyway apumzike/wapumzike kwa Amani.
 
Hii ajali imeninyima furaha kabisa. Kushuhudia Mtu akiungua si jambo rahisi
 
20160403_053958.jpg
Hiyo ajali ni kweli me ni shuhuda niliyeishudia ucku ni gari aina ya land cruser prado v 8 mpya plate no.DFL 598 alikuwa baba mmja kwenye gari imegonga truck ikaanza kuwaka hapohapo tumejitahd kuokoa tumeshindwa kwani gari ilivyoanza kuwaka milango ilijilock na kuanza kupga alam wananchi wakaanza kusema bomu linalipuka watu wakaingia hofu
 

Attachments

  • 20160403_053958.jpg
    20160403_053958.jpg
    41.7 KB · Views: 50
Moto ulikuwa mkubwa sana...ni vigumu faya wanakuja mtu ashakuwa majiv lilipta lory la mchanga tumemuomba apige tiper amegoma kwani alikuwa na mchanga binadam tunaroho mbaya sana mwezetu anaungulia pale hata kusaidia uwezo alikuwa nao kabsa
 
View attachment 334475 Hiyo ajali ni kweli me ni shuhuda niliyeishudia ucku ni gari aina ya land cruser prado v 8 mpya plate no.DFL 598 alikuwa baba mmja kwenye gari imegonga truck ikaanza kuwaka hapohapo tumejitahd kuokoa tumeshindwa kwani gari ilivyoanza kuwaka milango ilijilock na kuanza kupga alam wananchi wakaanza kusema bomu linalipuka watu wakaingia hofu
 

Attachments

  • 20160403_053952.jpg
    20160403_053952.jpg
    62.1 KB · Views: 62
Kuanzia mida ya SAA NNE usiku kuendelea madereva wanaendesha Magari wajuavyo wao,wako tungi bayaaa,hakuna mtu anayefata taa za barabarani etc

Hiyo jamaa apumzike kunako stahili,amen
 
Moto ulikuwa mkubwa sana...ni vigumu faya wanakuja mtu ashakuwa majiv lilipta lory la mchanga tumemuomba apige tiper amegoma kwani alikuwa na mchanga binadam tunaroho mbaya sana mwezetu anaungulia pale hata kusaidia uwezo alikuwa nao kabsa
Afadhali na wewe umeshuhudia. Turudi nyuma, huu pia ulikuwa uzembe wa dereva na mwenye truck.

Madereva epukeni speed za hovyo. Hii Bagamoyo road magari yana spidi za hovyo sana
 
Afadhali na wewe umeshuhudia. Turudi nyuma, huu pia ulikuwa uzembe wa dereva na mwenye truck.

Madereva epukeni speed za hovyo. Hii Bagamoyo road magari yana spidi za hovyo sana
Wewe unasema nn, wakati umeshaambiwa kile kipande kina ngongoti ana mguu mmoja, ndio asababishayo yote hayo.
 
hujapata hata picha ya kagari jinsi lilivoteketea
 
Majira ya saa kumi na moja asubuhi kumetokea ajali mbaya sana eneo la Mbezi Beach Afrikana.

Gari aina ya Nissana xtrail au Honda ikiwa inatokea Mwenge imegonga kwa nyuma truck na kuungua hapohapo.

Kwa mujibu wa mashuhuda watu wawili waliokuwemo ndani ya gari wamefariki kwa moto wakiwa ndani.

Kwa adabu zangu sitoweza kuweka wala sikupiga picha.

Mbona picha zinaonyesha land cruiser?
 
RIP huyo dereva aliyefikwa na umauti.Huyo wa Lori la mchanga aliyeshindwa kutoa msaada roho yake itamsuta sana,km yule jamaa aliyeshindwa kumuokoa mtoto sudani kusini akitaka kuliwa ni tai yeye anakomaa na kumpiga picture,Tumuombe Mungu atupe roho zenye utu kidogo tu.
 
Labda tuweke namba tu ya gari kama mtu anaweza kuifahamu anaweza toa msaada. T598BEL TOYOTA LANDCRUISER
 
Back
Top Bottom