Airtel wanayajua mahitaji muhimu kwa binadamu kwa watu wa waliokumbwa na Maafa Hanang?

S
Ukweli kwamba hii Nchi inawatu wengi sana wasio jielewa! Mtu anakwambia FAO ndo walete chakula! Inahuzunisha sana. Kwan Airtel atapata dhambi Gani kuleta hata magodoro pale watu wanalala ovyo? Au hata mahema tu!
Sio majukumu yao wamefanya hisani tuu, hayo ni majukumu ya serikali.
Hicho kidogo walichotoa tushukuru wasingetoa chochote ungelalamika pia?
 
Ina maana hela waliyotoa hujaona? Ulitaka watoe nini hasa. Wametoa hela kwanza kabla ya kutoa hizo huduma za mawasiliano.
Ukiwa na msiba mfugaji akachangia pesa then akatoa mbuzi wa kuchinja utakasirika kwanini ametoa mnyama. Ulitaka mfugaji alete pombe.

Kwenye CSR wapi uliona kampuni inatoa msaada kimbumbumbu bila kutoa na huduma zake.
Mzee watz wengi vichwa maji, airtel wametoa mtandao wa bure watu wanalalamika kwa hao airtel ni hisani wamefanya wala sio jukumu lao.
 
Airtel ndio wakajenge miundombinu ya umeme? Ndio wakasimike nguzo zilizoanguka?

Je wakileta magodoro na mahena mahitaji yote yatakamilika 100%? Sivyo.
Sasa kama hayatokamilika ikakosekana hitaji lolote utalalamikia tena Airtel? Uko hata na hisa 1 pale mpaka kudictate watoe mahema na magodoro? Na hizo fedha walizotoa haziwezi nunua hayo mahema na magodoro?

Kama magodoro hamna, serikali inayokusanya kodi na ambayo ina wajibu direct kwa mwananchi inafanya nini muda wote huu. Ni lini ulisikia Airtel wana kitengo cha dharula kutenga bajeti ya mahitaji yote ya wahanga wa majanga nchi hii?

Na je, Airtel ndio wana wajibu wa kujua kipi kinahitajika na kipi kimepatikana? Unaweza kusema hapa yanahitajika magodoro mangapi na mahema mangapi? Airtel hizo data wanazikusanya kutoka wapi wakati ziko serikalini?

Makampuni ya wawekezaji hayafanyi maamuzi kimatakomatako kama mnavyodhani mkishakunywa wanzuki. Hapo zimekusanywa fedha, data zipo serikali na taasisi zake husika na mashirika husika yanajua nini kinatakiwa. Kampuni nyinginezo ambazo sio experts kwenye hili suala zinaweza toa hela ikanunua kinachohitajika. Wewe kama unaona wanahitaji mapera wapelekee ila Airtel haiwezi fanya hivyo.
Nimekwambia wajenge? Au watengenezee miundombinu?

Walichokifanya ni sawa na mtu mwenye kipara kupewa msaada wa chanuo ! Ni matusi!

Umefiwa,nyumba imebomoka chakula magodoro ndo hivo Tena!
Mtandao shida umeme hakuna hizo dk Bure na internet Zina msaada Gabi kama sio utahira huu? Nani akae mtandaon Watoto hawana pakulala?

Ifike mahala tuambieni ukweli kuwa japo wewe ni sio mkulima basi tumia pesa Yako kufanya exchange na mkulima kwan Kuna dhambi Gani hapo?
 
Nimesoma mahali kwamba Airtel inasambaza bure Internet kule eneo la maafa, hiki ni kichekesho kikubwa sana.

kwanza nani asie jua speed ya Internet ya Airtel? Pili je hizo ni moja ya Needs za watu walio kumbwa na maafa pale? Watu wanahitaji Mahema, Maji, madawa, nguo. Airtel wao wanaona Internet ndii basic needs pale?

Hii ni Marketing strategies ya kijinga sana, kama hawawezi toa Basic needs pale kama Chakula, madawa, mahema, na nguo waache ujinga.

Hawa airtel wana akili sawa na watawala, yaani wote wanafanana akili na jinsi ya kuwaza si bure hata mtandani wao umekaaa kima gumashi gumashi sana.

Sasa bro kwa akili zako hyo habar bila support ya mitandao ungeijua?
 
Nimekwambia wajenge? Au watengenezee miundombinu?

Walichokifanya ni sawa na mtu mwenye kipara kupewa msaada wa chanuo ! Ni matusi!

Umefiwa,nyumba imebomoka chakula magodoro ndo hivo Tena!
Mtandao shida umeme hakuna hizo dk Bure na internet Zina msaada Gabi kama sio utahira huu? Nani akae mtandaon Watoto hawana pakulala?

Ifike mahala tuambieni ukweli kuwa japo wewe ni sio mkulima basi tumia pesa Yako kufanya exchange na mkulima kwan Kuna dhambi Gani hapo?
Sasa kwanini ulalamikie Airtel suala la umeme kukatika? Au hujui mamlaka ya umeme yako chini ya nani.
 
Airtel imetoa GB 2 na Dk. 100, kwa waathirika Hanang kwa siku 3 mfululizo.

Maana yake kwa mtu mmoja wametoa Tsh. 9000, idadi ya watu Ni 300,000+, hii ina maana;

300,000x 9000= 270,000,000/-

Kwanini hii pesa wasingeipeleka kwa wahusika?

Hii haiingii akilini kabisa!
Naipa pole shingo yako kwa kubeba ujinga.
 
S

Sio majukumu yao wamefanya hisani tuu, hayo ni majukumu ya serikali.
Hicho kidogo walichotoa tushukuru wasingetoa chochote ungelalamika pia?
Nisingelalamika ...kwani Azam,Voda,Tigo nk umeona nimeleta Uzi wao hapa?hapa tunazungumzia hitaji maalumu Kwa Wakati huu wa dharula. Hivi umefiwa huna pakuilaza familia mifugo Yako yte imekufa chakula hakuna huo muda wa kuwasha data utapata lini na sangapi? Watu Huwa tunafiwa na wapendwa wetu lkn unaweza kataa siku2 hujaingia mtandaoni
 
Back
Top Bottom