Airtel Tanzania yapandisha gharama za internet!

Status
Not open for further replies.
Yaani huwezi amini sasa hakuna tena 400MB KWA 2500.. HILI NDILO LILILOKUA BUNDLE LA WATANZANIA WALIO NA KIPATO CHA CHINI SASA TWENDE KWA NINI ATAKAYEWEZA KUTUKOMBOA....
KWA HILI WASITEGEMEE TENA WATANZANIA WAENDELEE KUTUMIA AIRTEL KATIKA INTERNET...BYE BYE AIRTEL

Name:
Number: 15444
Content:
Ndugu Mteja Salio lako ni: 1. BUNDLE : 92MB
Time: 3/2/2012 9:48:48 PM
 
bus limejaa.. rudini mlikotoka.. ha ha ha.. wengi walihama toka kwenye vibito vle.. mgongo wa chura..
 
Hapa nilipo natafakari hii bundle ikakata tar 18 mwezi huu sijui nitaishi vp, honestly Airtel walitufaa sana watu wa kipato cha kati lkn kwa mwendo huu cjui hali itakuaje
 
Yaani huwezi amini sasa hakuna tena 400MB KWA 2500.. HILI NDILO LILILOKUA BUNDLE LA WATANZANIA WALIO NA KIPATO CHA CHINI SASA TWENDE KWA NINI ATAKAYEWEZA KUTUKOMBOA.... KWA HILI WASITEGEMEE TENA WATANZANIA WAENDELEE KUTUMIA AIRTEL KATIKA INTERNET...BYE BYE AIRTEL
Yaani huwezi amini mkuu hawa airtell wameniuzia bundle ya 150MB kwa elfu sita jana leo nimeenda kununua ZANTEL ndio nakandamiza nayo tu mkuu sasa hivi Airtell limekuwa genge la wezi tu mkuu.
 
Yaani huwezi amini mkuu hawa airtell wameniuzia bundle ya 150MB kwa elfu sita jana leo nimeenda kununua ZANTEL ndio nakandamiza nayo tu mkuu sasa hivi Airtell limekuwa genge la wezi tu mkuu.

Mbaya zaidi ni kwamba kupanda kwa gharama kumeambatana na huduma mbovu. Tangu wiki ianze mara kwa mara mtandao unakuwa down. EDGE ndio inapatikana zaidi ambayo ni very very slow kama serikali
 
Unajua ndio maana nilisema huu mkongo wa taifa utapunguza garama nyingi c mnaona wenyewe!, lakini hata bibi na babu zenu kule kijijin nimewabustia bei za vibiriti kutoka shs 50 hadi 100@1, mnaonaje! TUMEJARIBU, 2MEWEZA NA 2NASONGA MBELE. Mna2zodoa sana humu mitandaon, na magazet nitapandisha bei, channel zote nzuri mtazlipia yan ilimradi mjute kuzaliwa tz +<§%
 
Nina Blackberry latest vision, nilipokwenda Voda kuwauliza ni kwa nini haiconnect Internet wakanijibu mpaka niwe na BB subscription ambayo gharama yake ni shilling 30,000 kwa mwezi, nikawasihi kwamba hii sio Blackberry yangu ya kwanza kutumia bali ni ya nne nazote hizo nilikuwa nalipia pay as you go, wakaniambia eti sasa hivi mpaka uingizwe kwenye Blackberry server yao na hakuna jinsi ni lazima nilipie 30,000. nimekataa siwezi kujiingiza gharama ambazo ni unneccessary, ni kwa nini laptop yangu nitumie gharama nafuu halafu smartphone ndio inigharimu?

Sasa basi kama hawa Airtel nao watakuwa wameingia kwenye upuuzi wa kusitisha huduma hii rafiki hakuna chaguo lingine zaidi ya ku boycot mtandao wao for good. Watanzania tusikubali kugeuzwa makondoo na mkumbuke zamani tulikuwa tunalipia airtime kwa dolar, ikaja tukawa tunachajiwa kwa dakika na hatimaye sasa tunachajiwa kwa sekunde, pls kama hili swala ni kweli tutaanzisha special thread hapa na kukusanya chip zao tuwarudishie na uzuri media tunazo humuhumu.


Mie najua kwa Airtel unalipia kihivyo tangu few years ago maelfu hayo kwa mwezi ikiisha unalipa tena na ipo safiiiiiiiiiii. kwani umeangalia matumizi gani ulikuwa nayo kwenye pay as you go na nadhani utapata matumizi mengi ya simu yako kwa hiyo bundle ya mwezi.
 
Zantel wao wamepandisha bei kidogo tangu kuanza kwa mwezi huu wa tatu.
Kwa mfano mtu aliyekuwa anasubscribe Z MONO ambayo ni 500MB kwa sh. 10,000 sasa imepanda hadi sh.12,500
ukilinganisha na hiyo ya airtel naona zantel wako fair kidogo.
 
Mi mwenyewe nahama, kawaambieni sasa hivi hatuhamii bali tutahama watapandishaje bila taarifa
 
Jamani mbona mimi imeniletea ujumbe huu

Name/Number: +255786507507
Time: 2012-03-03 00:40:22
Content: Mpendwa mteja! Kifurushi hiki kinagarimu shilingi 2,500/= tu kwa mwezi. Kujiunga SMS INTERNET kwenda 15444. Utaweza jiunga tena mara umalizapo kifurushi chako

hii ikimaanisha huduma bado ipo si ndio
 
Jamani mbona mimi imeniletea ujumbe huu

Name/Number: +255786507507
Time: 2012-03-03 00:40:22
Content: Mpendwa mteja! Kifurushi hiki kinagarimu shilingi 2,500/= tu kwa mwezi. Kujiunga SMS INTERNET kwenda 15444. Utaweza jiunga tena mara umalizapo kifurushi chako

hii ikimaanisha huduma bado ipo si ndio
tupatie screen shot ya ujumbe huo mkuu
Capture.PNG
 
Mkuu tumia simu ya Mkononi piga namba 100 kisha 4 halafu 2 itakuletea hiyo kitu. Nadhani itabidi kujiunga kwa kutumia simu kisha tunarudisha kwenye modem sasa
May be mkuu
Maana kiukweli bundle hii ilikuwa ni kwa watumiaji wa simu lakini hawakutubana tukiweka kwenye modem pia
Nitajaribu kesho
 
Kuna bundle za aina mbili.
1. Time based bundles
2. Data based bundles

2. DATA BASED BUNDLES
50 MB 2000/=
150 MB 6000/=
250 MB 10,000/=
500 MB 20,000/=
1 GB 25,000/=
2 GB 30,000/=
5 GB 75,000/=
15 GB 200,000/= MIEZI MITATU
30 GB 300,000/= MIEZI SITA

TIME BASED BUNDLES
DAY 500/= 20MB
WEEK 7000/=
Nashindwa hata kuendelea jamani.

Source ni customer service!!!
 
Hali inatisha, nadhani tutashindwa kuingia JF sasa na cafe bei nayo itapanda. Nahama Airtell sasa hivi hawafai.
 
You have 34 Seconds to call ANY NETWORK in TZ valid untill 02/03/2012.
 
Nikiwa nimejaa upepo baada ya kunila elfu kumi ya kitanzania (Tsh 10,000) na kujaribu cust care kwa takribani masaa 4 ndipo nikajibiwa kua......karibu huduma kwa wateja.....kwa huduma hii utakatwa sh.....bonyeza moja kukubali...jasho likaongezeka kidogo hapo...nikajiongeza kidume......mhudumu: ni kweli gharama zetu zimepanda .....sikutaka hata kuendelea na nikamwambia nnapokata hii simu NAHAMA AIRETEL kwanza kuwapata customer care ni isue,pili ukiwapata unalipia.....daaaaaaah!!!!! Sasa natafuta mtandao cheap zaidi wa INTERNET uwe wa uhakika ila gharama zisizidi elfu 15 kwa 2 ama 3 GB hivi ama kwa mwezi kabisa mimi hata sasa hv ntaenda tafuta huo mtandao we niambie ulipo.........:A S 465:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom