1) Kuna mwanamke ambaye akikasirika huishia kulia tu
2) Lakini mwingine akichukia huongea sana muda wote mpaka ikukere
3) Mwanamke mwingine akikasirika ananuna, haongei, mtapishana kimya kimya mawasiliano kibubububu shavu limejaa kama kobra!
4) Mwingine akishikwa na hasira period ya ghafla ghafla inafuata
5) Kuna wanawake ambao ole achukie. Atachokishika usipokimbia anakutandika nacho halafu majuto baadaye
6) Mwanamke mwingne akikasirika, hasira zake zinaishia kwenye kuvunjavunja vyombo au saa nyingne kugombezagombeza wafanyakazi na watoto. Dizain hii huwa ni wale waliokosa kukidhiwa haja za kihisia na waume zao!
7) Mwanamke mwingne ole akasirike mtajuana kitandani panapo majaaliwa. Nakwambia utaungama yote
8) Kuna ambao wakitibuliwa hukimbia kufunga mabegi na kuondoka
9) Wapo ambao wakikasirika wanagoma kupika
10) Wengne wakikasirika wanaamua kwenda kulala kimya
11) Wanawake wengne wakikasirika tumbo linakata mpaka kupelekea kuharisha
12) Wapo ambao wakishikwa na hasira huingia kwenye maombi na kuugua kusikowezwa kutamkwa. Uchungu ukiisha wananawa uso na kwenda sokoni kuendelea na majukumu
13) Yuko ambaye akishikwa na hasira hucheka saana, hutajua kama amekasirika. Dizaini hii ni hatari sana anaweza kukudhuru kirahisi.
Je wewe unajijua uko kundi gani?


Wote tunatambua kama hasira hasara basi nyie waume zetu ukiona mke wako ili jambo limemkera na limemkasirisha tafuta mbinu yoyote yakuweza kulitatua tatizo na kumfanya mkeo aachane na zile hasira arudi ktk hali ya kawaida.
Sio mume umemkasirisha mkeo basi unajiona wewe ndio kidume hata kumbembeleza imekushinda sivyo ivyo hata mume unatakiwa kuwa MbunifuU sio kila siku ubembelezwe wewe tu hata mkeo ana nafasi yake katika ndoa.
Mwanamke ni dhaifu sana unaweza kufanya kitu kidogo tu na hasira zikaisha.
Tupendane, tuhurumiane, tusameheane, ili tufike mbali katika ndoa zetu.