Aina ya Wanaume WATONGOZAJI kwa vigezo vya sababu...

Aina ya Wanaume WATONGOZAJI kwa vigezo vya sababu...

AshaDii

Platinum Member
Joined
Apr 16, 2011
Posts
16,189
Reaction score
18,117
Wapendwa wa MMU nawasalimu with Love,

Katika ulimwengu wa utongozaji mambo yamebadilika sasa to the extent hata akina dada/mama huwa tunajilipua once in a while. Ila ukweli unabaki bado kwa kiasi kikubwa wanao ongoza kutongoza ni akina kaka/baba. Na katika kutongoza huko wengi huwa na sababu mbali mbali za kumtongoza huyo mtongozwaji.

Zinazofuata ni sababu hizo zinazomfanya huyo kaka/baba afanye maamuzi na kufanyia kazi malengo yake ya kumpata huyo anae kuwa kadaka jicho lake. Hizi ni sababu tokana na mtazamo wangu, hivyo unaweza kukubaliana/kataliana/ongeza na pia toa maoni ili tuweze elimishana zaidi.

Anakujaribu

Ni mara nyingi nimesikia kaka/baba zetu wakiweka wazi kukubaliwa na mwanamke aliye mtongoza na kukubaliwa bila kutarajia. Ni kuwa just for the sake of it, mazingira yanakuwa yanaruhusu anajikuta kutongoza kwa kujifurahisha.

Kakutamani

Hii ndio sababu inayo ongoza kwa sababu zote za akina baba/kaka kutogoza. Uzuri, Urembo, Mvuto wa dada/mama husika hucheza nafasi kubwa ya mtongozaji kuvutiwa hadi akataka kuwa na wewe. Hii hutokana na ukweli kuwa kiasi kikubwa cha wanaume anapotongoza malengo yake inakuwa kukupata na kuweza kufanya sex na mwanamke huyo. Hata hivyo vivutio vimetofautiana, kuna wale wanafutiwa na miguu, wengine sura, wengine midomo na wengine weengi makalio (kwa kaka/baba zetu hawa wa kibongo).


Kakupenda

Hii ni mara chache, mara nyingi kigezo cha kwanza mwanaume kutongoza huwa kuvutiwa na huyo mwanamke then kupenda kunakuja baadae. Hata hivyo kuna exceptions; mfano kama vile huyo mwanaume anapokuwa yupo mahala ambapo anakutana na huyo dada mara kwa mara. Siku ya kwanza alipo muona hakuwa na wazo kabisa la kumtongoza, ila with time kwa kuendelea kumuona pengine hata kwa kuendelea kuwasiliana kama wana mazoea anajikuta kampenda tokana na tabia or sababu zozote zile alizonazo hivyo kuamua kutongoza. Hii sababu ina probability kubwa ya kuishia kwenye ndoa.

Ana ngunge (Horny) Anahitaji pa kupooza haraka

Ana hitaji kwenda kupoza hamu ya ngune alilo nalo. Pengine anakuwa hajakutana na mwanamke muda mrefu for what ever reason, na hivyo huyo mtongozwaji ndiyo akaonekana chaguo zuri la kuweza kuubali haraka bila uchelewefu wa kwenda kubanjuka. Mara nyingi hii hutokea kwa mwanamke ambae ni kazi yake hio (yaani dada poa) OR yule anayejulikana mtaani kama mama Huruma.

Wa ku beep

Huyu ni aina ya yule mwanaume ambae hayupo committed. Yeye siku zote anakuhitaji wewe siku akitaka kukutana kimwili. Yaani mara nyingi anacheza na hisia zako.. Anakuwa anakujua vema… Namna ya kukuweka sawa, namna ya kuahakikisha huna wasi wasi juu yake na namna ambavyo kukutana na wewe ni lazima siku ambayo anataka kufanya na wewe uone kawaida. Anaweza akawa hata na galfriend/mke huko but akawa na mwingine kwa ajili ya sex tu.

Kukuoa

Hii utokea pale mwanaume anapokuta mwanamke katimiza vigezo anavyotaka kwa mke wake, kama vile utulivu, upole, usafi, aina ya kazi n. k. Inakuwa kamjua tabia yake (iwe kwa muda mrefu ama mfupi) na zikamvutia kutaka kuwa nae kwa muda mrefu zaidi tena kama mke na mume kabisa. Hii ni mara chache, mwanaume huja mpole sana, sex inakuwa si priority sana. Yupo haraka kutaka kukufahamu zaidi wewe na familia yako na anakuwa na bidii ya kutaka kuhakikisha hata upate mimba mara moja.

Mahusiano

Huyu anapenda kuwa safe. Anataka mwanamke wa kuwa nae pamoja kama partner, awe rafiki, waweze kukutana kimwili na wawe waaminifu. Mara nyingi anakuwa kalenga wewe ndio uwe the special lady. Hata ikitokea ana wengine mwisho wa siku huyo mwanamke wa kujenga nae mahusiano anakuwa makini zaidi na invest zaidi katika huo uhusiano.. Mara nyingi ikienda vizuri hata huishia katika ndoa.

Kukuchuna

Huyu mwanaume anataka mwanamke anae onekana una uwezo wa kujikimu kila kitu. Unaonekana independent na huoni taabu kum support mwanaume. Hivyo hutaka wepesi… Haoni taabu siku ya kwanza mmetoka ama siku zingine zote wewe ukitop up the bill ziku zote. Kwake anakuwa so set on enjoying bila kujali partnership ya kweli katika mahusiano hayo.

Kukuzalisha

Hii ni nadra.. Siku hizi kaka/baba zetu anakutamkia kabisa… Hasa hawa ambao hawataki ku commit na kuoa. Ma senior bachelors. Inafika wakati anajua kabisa mke sitaki, but nataka niwe na mtoto so the shortcut anatafuta mwanamke mwenye mwelekeo wa kuwa mama mzuri, tena kwa kiasi kikubwa awe anajiweza kuweza kulea mtoto na anakushawishi ubebe mimba. Pengine hata kwa uongo wa nitakuoa. Thou hii ni wachache sana.

Wa kuzugia

Mwanaume wa namna hii ni yule anataka mwanamke kwa sababu si ya dhati. Kwa kiasi kikubwa anakuwa na huyo mtu kwa sababu maalum. Mfano; anaweza kuwa yupo gay, hayupo tayari sexuality yake ijulikane hivyo anatongoza mwanamke wa kuwa nae (wengine hata kuoa kabisa) ili nae aonekana ana mwanamke na hivyo mwanaume wa kawaida katika macho ya watu.

Ujumbe kwa akina dada/mama wenzangu:-

Kuna wakati ni mtihani kujua mwanaume anakutongoza kwa ajili gani. Ila siku zote tunacheza na insticts na pengine kuingia katika mahusiano kana kwamba wacheza kamali. All in all kuna wale ambao wapo so obvious na ni rahsi kujua sababu ya yeye kukutongoza. Faida ya kujua hilo ni wewe kutoa maamuzi kama upo tayari uwe nae kwa vigezo ambavyo vimemfanya aje kwako.

Naomba michango yenu ladies and Gentlemen. Nawategemea.

Pamoja saana,:grouphug:

AshaDii.

Sababu zingine Courtesy of SMU...

AshaDii , habari za siku? Mimi niongezee haya;

1. "Ego": Kuna wakati inatokea pia "tunatongoza" (naamini kutongoza kunapungua sana siku hizi!!🙂) kwa sababu muhusika 'kajilengesha' na hatutaki kuonekana pengine ni "majoka ya kibisa"! Pengine,technically, hii ndio hiyo unayosema mwanamke amekutongoza. Nilienda saluni juzi kunyolewa ndevu, baada ya kunyolewa nikaingia 'chumbani' kuoshwa na madada wa saluni akawa ananichana nywele na kuweka nyusi zangu vizuri huku akinitizama usoni kwa kurembua na kusema kwa sauti ya kunong'oneza "mimi nipo fresh".......to me this was an invitation lakini nilikubali kuonekana "nyoka wa kibisa" nikajifanya sijamsikia/sijamwelewa!

2. "Tasting": Hii inafanana kwa kiasi na hiyo ya kutamani ingawa ni tofauti kidogo. Hapa nakuwa ama nataka "kuonja" ili nijue mwanamke wa aina fulani yukoje (kwa mifano tu, - wa kimasai, mwanake mnene/mwembaba, wa kizungu/kiafrika, wa kisomali. Niliwahi kuwa na demu wa kiholanzi mwaka fulani, naamini hii ilikuwa ni sababu mojawapo ingawa ilichangiwa na hiyo ya 1 hapo juu (au tuseme tulikutana wote tukisukumwa na sababu hii ya 2!:tape2🙂.

3. "Proof": Hii inataka kufanana na hizo mbili hapo juu lakini kwa kuwa hapa unataka ku-prove kitu fulani. Inaweza kuwa unataka kuonesha (kwa wanaume wenzie au kundi lako) kuwa hata wewe unaweza 'kuwinda na kupata kitoweo'. Inaweza pia kuwa unataka kuprove maneno ya watu au stereotypes fulani katika jamii (kwa mfano: wanawake wa kimakonde wanasifika kwa kukata kiuno, wanawake wa kichaga ni vigumu kuwapata, wanawake wa kipare ni rahisi kuwapata, wanawake wa kihaya/kitusi wanatoa/rusha maji nk nk:banplease🙂.

4. "Strategic": Hapa unatongoza au kutaka mahusiano na mwanamke ili kupata kitu au matokeo fulani ambayo hayahusiani kabisa na mapenzi kwa muhusika. Hili linaonekana zaidi kwa kina dada (maeneo ya kazini kwa mfano ili kupata uhakika wa ajira, kupandishwa cheo/mshahara nk) lakini hata kwa wanaume lipo sana. Kuna rafiki yangu mmoja alikuwa anataka kumuacha girlfriend wake kwa sababu fulani lakini hakuwa tayari kusema ukweli. So alichofanya, aliamua kumtongoza na kutembea na rafiki yake wa karibu na uhusiano ukafa kirahisi tu!:heh:

habari yako dada AshaDii, nami niongezee sababu nyingine:

1: Kijamii: umempeleka nyumbani mtu unayempenda lakini familia yako na ndugu zako (hasa wazazi/mawifi) hawamkubali huo mpenzi wako kwa vile haja-meet criterias 1,2,3 ... hivyo basi itakulazimu (kama akili zako ni za kushikiwa) kuanza kutafuta mtu aliye na vigezo 1,2,3 ... ingawa hii hautoli-admit in the first place kuogopa kuonekana wewe ni wapi ... but utalitekeleza involuntarily as time goes!

2: Stress/Psychological torture - Mwanaume anapokuwa na manyanyaso sana toka kwa mwenza wake/mke, mara nyingi huwa na msongo mkubwa sana wa kimawazo, na hii hupelekea kupoteza furaha na hamasa ya kimapenzi kwa mwenziwe, na matokeo yake hupelekea 1. kutafuta pango la kupunguzia stress zake (kuliwazwa) na au 2. kuwa mlevi na hivyo kuwa prone kupata mtu wa kupunguza stress naye .... ("nani kamwaga pombe yangu style ..." kwenye bars/pubs!)

pia swahiba, kwa mtazamo wangu, sababu hizo hapo chini ni more or less the same.
 
Kadri siku zinavyoenda ndivyo jinsi wanaume tunavyotongozwa zaidi kuliko tunavyotongoza.

Tukimaliza hii tuangalie na vigezo vya wanawake kututongoza...

Kaka Marcopolo, ni kweli suala la idadi ya wanawake kutongoza lipo wazi... Lakini pamoja na kuongezeka huko bado ukweli unabaki wanaume ndio wanaongoza kwa kutongoza. Na suala la wanawake kutongoza lipo mijini zaidi.. Hivyo inevitably asilimia bado itakuwa ni ndogo in comparison.

Hata hivyo, taking it kuwa wewe ni mwanaume, kuna sababu nimesahau kuweka hapo? Ama kuna iliyopo na ukubaliani nayo?

BTW kwa kifupi sababu ya Mwanamke kukutongoza.

1. Unauwezo sana kipesa (Kwa mtazamo wake)
2. Kakupenda - ingawa naona yule ambae anakuwa amekupenda sana ni wachache wenye guts za kukutongoza.
3. Kuna kitu anatarajia kupata toka kwako.
4. Anataka sex na hana soni kuuliza.
5. Ni the type of guy anatamani awe nae (sifa on her list)
6. N.k
 
++

Ajabu moja ni kuwa hata insticts mlizojaliwa,zikuambie aliyepo mbele yako ni muongo
unazipuuzia You rely on flow of words and sound.
Hivyo grafu ya wanawake kuchezewa itazidi kupanda

++
 
Kaka Marcopolo, ni kweli suala la idadi ya wanawake kutongoza lipo wazi... Lakini pamoja na kuongezeka huko bado ukweli unabaki wanaume ndio wanaongoza kwa kutongoza. Na suala la wanawake kutongoza lipo mijini zaidi.. Hivyo inevitably asilimia bado itakuwa ni ndogo in comparison.

Hata hivyo, taking it kuwa wewe ni mwanaume, kuna sababu nimesahau kuweka hapo? Ama kuna iliyopo na ukubaliani nayo?

Unajua AshaDii wewe ni kungwi kwenye haya mambo.

Sijaona sababu ambayo umeisahau au ambayo sikubaliano nayo.

Kama nalazimika kuongezea labda nitasema wakati mwingine huwa ni mchanganyiko wa sababu mbili au zaidi kati ya hizo. Yaani inaweza kuwa mtoto umemzimia halafu unatest zali tu na zali likiwin unakiingiza kitu studio ili kuhakikisha hakiingii mitini. Huo mchanganyiko wa sababu kama tatu hapo.
 
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?
 
unaweza kuishi gest au kwa ndugu huku ukitafuta sehemu permanent unayopenda kuishi...inakubalika sio?
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?
 
Kuna baadhi ya wanawake yaani ukishaanza kuwasifia tu wanakuwa wepesi kupita maelezo.
Je hii inatokana na nini?
 
AshaDii ujumbe mzuri sana
Ila kama ZeMarcopolo alivyosema naona siku hizi kibao kinageuka inakuwa kuwa tunatafutwa sisi badala ya kutafuta tena na tena ukiwa ndo mpenda hayo mambo sana hawatajali una pete ya ndoa au una ndoa au uko committed wao wanachotaka ni kukupata
 
Last edited by a moderator:
++

Ajabu moja ni kuwa hata insticts mlizojaliwa,zikuambie aliyepo mbele yako ni muongo
unazipuuzia You rely on flow of words and sound.
Hivyo grafu ya wanawake kuchezewa itazidi kupanda

++
Himidini, wala hata usishangae.... Lol. Wacha wanawake tuitwe wanawake, na ndio maana John Gray alisema "Men are from Mars, Women from Venus".

Mwanamke mdogo ambae ndio kwanza anajifunza mapenzi... Ni mwepesi wa kuamini kila kitu (na hivi kaka zetu wote mlijaliwa kuigiza when it comes to kumtaka mwanamke); inakua ni rahisi.

But with time wanawake wengi hujua kuwa anadanganywa... Ila shida huja kama kuna kitu anapata/taka kwako. Unaweza dhani kuwa wewe ndio mjanja na wamrubuni, kumbe anajua nini anafanya na nini anataka. Pamoja na kuwa wanawake wanachezewa hapa mjini... Wanaume ni balaa! Wanaume huchezewa sana na wapenzi/wenza/galfriends zao na kamwe hata asijue.

Mwisho wa siku inakuwa ni win win situation.
 
Last edited by a moderator:
Nilishawahi kuambiwa kuwa wanaume wana milango mitano ya hisia lakini wanawake wao wanayo sita, hiyo ya sita kazi yake ni kung'amua mwenzi mwema pindi wanapotongozwa...
Lakini miaka ya karibuni baada ya utandawazi tumejikuta hata sisi wanaume tume-develop hisia ya sita ambayo kazi yake kubwa ni ama kuongopea wanawake wakati wa kutongoza au na sisi kuitumia wakati tunatongozwa na wanawake...
 
Kuna baadhi ya wanawake yaani ukishaanza kuwasifia tu wanakuwa wepesi kupita maelezo.
Je hii inatokana na nini?

Mkuu umesahau kuwa content mojawapo ya tongozo ni kumwaga sifa, hivyo usione kuwa ni urahisi bali tambua kuwa somo limeeleweka
 
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?

Demu wa kuzugia ni yule ambaye unakuwa nae katika mahusiano ila hauna future nae kama vile kumuoa na kujenga familia yenu kwa pamoja. Yaani unakuwa na huyo wa kuzugia huku ukiwa unatafuta yule ambaye unadhani atakufaa maishani.
 
Himidini, wala hata usishangae.... Lol. Wacha wanawake tuitwe wanawake, na ndio maana John Gray alisema "Men are from Mars, Women from Venus".

Mwanamke mdogo ambae ndio kwanza anajifunza mapenzi... Ni mwepesi wa kuamini kila kitu (na hivi kaka zetu wote mlijaliwa kuigiza when it comes to kumtaka mwanamke); inakua ni rahisi.

But with time wanawake wengi hujua kuwa anadanganywa... Ila shida huja kama kuna kitu anapata/taka kwako. Unaweza dhani kuwa wewe ndio mjanja na wamrubuni, kumbe anajua nini anafanya na nini anataka. Pamoja na kuwa wanawake wanachezewa hapa mjini... Wanaume ni balaa! Wanaume huchezewa sana na wapenzi/wenza/galfriends zao na kamwe hata asijue.

Mwisho wa siku inakuwa ni win win situation.


AshaDii,

Nilidhani hili somo limedhamiria kufanya swala zima la "kula mzigo" lisiwe rahisi. Lakini kumbe kuna hiyo win-win situation. Hapo naona watu wataendelea kula mzigo kama kawa kwa sababu kumbe mabinti wenyewe wakati mwingine wanakuwa na "malengo" yao...

Hahahahahahahahaha

Hii saikolojia ya "kula mzigo" inafurahisha sana.

Lakini mimi siku hizi sili mizigo. NIMETULIA...
 
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?

Kwa uelewa wangu... Wakuzungia haipo kwa mwanamke tu, ipo na wanaume pia.

1. Hakunaga promises. Mahusiano ni living the moment.
2. Kwa jina la kiingereza maarufu kama (Booty call). Mara nyingi anakuwa wa kukidhi hamu yako ya sex.
3. Mpo wote on and off, ni aina ya mtu ambae wamfikiria inapotokea wapenzi wako wote hawapo available.
4. Ama unaweza kua nae kila mara but yupo kwa ajili ya kujaza nafasi kwa muda hadi pale the type wapenda apatikane.
5. Mara nyingi wa kuzugia (awe mwaname/mume) huwaga wapole, hawapo demanding, wapo understanding na yawezekana akatambua kabisa kuwa huwezi invest katika hayo mahusiano.

However I should add, kuna watu waliwapata watu wao kwa malengo ya kuzungia na kujikuta huyo mtu ikageuka ndio mpenzi mwenyewe wa kudumu.
 
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?

Mbona hamna msamiati hapo The Boss

Huyo demu hajakidhi viwango vyako lakin kwa vile yupo available huoni hatari kumsugua na unamsugua huku ukiendelea kutafuta toleo lingine type unayotaka wewe
 
Last edited by a moderator:
mie nna swali

nimewahi sana kusikia kina dada wakishauri watu humu
kwa kuwaambia 'tafuta hata demu wa kuzugia'

na mimi binafsi nimewahi ulizwa na mwanamke/wanawake..
swali hili 'unanipenda kweli au mie wa kuzugia'?

sasa najiuliza mno exactly 'demu wa kuzugia ' yukoje?

na unaweza mwambia msichana 'yes wewe ni wa kuzugia?
hii kitu 'demu wa kuzugia' imetoka wapi?
asili yake wapi?

Demu wa kuzugia kule "mtoni" au "kiwanja" kwa kina Nyani Ngabu wanaita "no strings attached".

Ila beware, kuna watu wengi tu wameishia kuoza kwa demu wa kuzugia. Kuna asali ukiionja unaweza kujenga mzinga kwa kunogewa...
 
leo ni birthday yangu sitaki kumkwaza mtu...nina mengi ya kueleza hapa...ngoja niwatizame tu kwa leo

:A S-rose:...Happy Birthday to you...
...Happy Birthday to you...
...Happy Birthday Dear Smile...
...Happy Birthday to yooooou. :A S-rose:

Smile, Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema akubariki, akuneemeshe na kukupa yale yote umedhamiria na kuhitaji katika maisha yako. Kubwa zaidi aweza kukujaalia upate mume bora na familia bora yenye Amani na Upendo pamoja na maisha Mareeeefu.

Happy Birthday Dearest.

Pamoja saana with Lots of Love. :grouphug:
 
AshaDii,

Nilidhani hili somo limedhamiria kufanya swala zima la "kula mzigo" lisiwe rahisi. Lakini kumbe kuna hiyo win-win situation. Hapo naona watu wataendelea kula mzigo kama kawa kwa sababu kumbe mabinti wenyewe wakati mwingine wanakuwa na "malengo" yao...

Hahahahahahahahaha

Hii saikolojia ya "kula mzigo" inafurahisha sana.

Lakini mimi siku hizi sili mizigo. NIMETULIA...

ZeMarcopolo kumbe ukitoka siasani unakuwa na point eehh
Yaani kwa sasa wanawake imebaki ni kama fashion yaani mnakutana just for fun popote pale iwe kanisani au kwenye sherehe au hata shopping mnapeana number za simu muda mfupi mnaambiana mambo yenu na chart kidogo mnaenda kumalizana bila hata kujua mwenzangu ni nani au ana malengo gani na baada ya hiyo starehe tunaweza hata tusionane tena au mpaka na number inafutwa au kila ikipigwa unaambiwa iko busy
Ni hali ya kawaida sana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom