Aibu uokoaji wa wahanga wa meli

Hii sasa thihaka kwa waathirika wa meli iliyozama Zanzibar! Ndugu zangu nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV, nimeona waokoaji wakilalamika kuwa baharini kuna miili ya watu wengi tu ila wanashindwa kufanya uokozi sababu hawana vifaa!!!
Jamani, meli yenyewe inasadikiwa kuzama kwa uzembe halafu wanasema vifaa vya uokoaji havipo. Vifaa vyenyewe ni gloves, machela, mafuta ya boti n.k. Jamani wahusika (serikali) acheni mzaha na wananchi. Hivi haya magloves ni tofauti na yale yanayodaiwa na madaktari? Hii nchi jamani acheni masihara hali siyo kabisa!!

Hili suala halitakiwi kuzungumzwa tena hapa maana liko mahakamani. Dr. Ulimboka alikuwa akipigania moja ya vitu kama hivyo...such as gloves na kadhalika zote. Hilo suala lilipelekwa mahakamani hatutakiwi kudiskasi kwa mujibu wa ibara ya 1.8.2.5 ya mwaka 1853 iliyotungwa na na kupitishwa na Bunge la Msoga.
 
Tuwashangae hao wazanzibari kukiweka madarakani chama kisicho wajari waacheni waandelee kufa huku viongozi wao wakishiba rambi rambi inayotolewa ambayo haiwafikii wahanga na wafiwa
Mkuu kumbuka waliozama sii wazanzibari tu, wamekufa watu WA mataifa mengi. Pia hizo rambirambi afadhali zingefika basi lakini ndo hivyo zinaishia midomoni mwa manyang'au.
 
Wakinunua vifaa vya kuokolea watu,watakosa hela za kununua mabomu ya machozi na magari ya kumwaga maji ya kuwasha
 
ZMA dhaifu.
Ndio shida pekee, wamekalia kusajili meli za Iran tu.
 
mi naona tuwe tunasafiri na vifaa binafsi vya kuokolewa kama gloves na mafuta ya boti kama ikitokea ajari kama hii wawe wanachukua na kutuopoa na sio kutuokoa
Akili zako ni za barafu zinaganda na kuyeyuka sasa hivi zimeyeyuka, watu wanafikiria vitu muhimu we unaleta mzaha. kwa fikra zako ukiwa na Groves na mafuta ya boti na meli imezama hivyo vitu vitapatikanaje? Puuuuu. mb. a. v.u
 
Hii sasa thihaka kwa waathirika wa meli iliyozama Zanzibar! Ndugu zangu nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV, nimeona waokoaji wakilalamika kuwa baharini kuna miili ya watu wengi tu ila wanashindwa kufanya uokozi sababu hawana vifaa!!!
Jamani, meli yenyewe inasadikiwa kuzama kwa uzembe halafu wanasema vifaa vya uokoaji havipo. Vifaa vyenyewe ni gloves, machela, mafuta ya boti n.k. Jamani wahusika (serikali) acheni mzaha na wananchi. Hivi haya magloves ni tofauti na yale yanayodaiwa na madaktari? Hii nchi jamani acheni masihara hali siyo kabisa!!

Acheni mjadala wa hili swala kwani tayari wahusika wameisha fikishwa kwenye vyombo vya sheria.
 
Hivi wamarekani hawawezi kuishtaki serikali kwa watu wao waliopoteza maisha? Maana naskia walishatoa tahadhari juu ya hiyo meli.
 
Hizo gloves ndo hizo hizo wanazotumia ma dr waligoma hazipo mahospitali sasa serikali ikaokolee maiti nini, msituseme ccm mlituweka madaktari wenyewe ninyi na wake zenu tuliwavisha kanga na kofia sasa ela za gloves ziliisha mnataka nini? Tuacheni tule bata kwanza mnatishia kututoa 2015 tusipo iba sasa itakuaje?
 
Mapungufu na makosa yale yale kwenye kila janga linalotoke Tanzania, Meli ya tatu sasa inayopata ajari lakini idadi ya abiria haijurikani, alafu Sumatra wapo nao wanatoa idadi zisizo rasmi na hawawajibishwi.
 
Sasa unadhani watafanyaje na vifaa hawana.

Ni kweli vifaa vya uokoaji hawana. yani hata hawa Jeshi letu la maji (Navy) huwa nawaona na magwanda mapya siku za paredi (halaiki) uwanja wa Taifa. Nadhani wamewekeza zaidi kwenye paredi kuliko kwenye shughuli zao husika.
 
Ndugu wana JF, ktk mambo ambayo sisi .km taifa linadhihirisha wataalam/kitengo cha maafa/serikali inaonyesha haipo makini ni hii ajali. Tunakumbuka ajali ya MV Bukoba; ajali ya majuzi tu ya Islander. Haya majanga yalikuwa MAFUNDISHO tosha KABISA kutufanya kujijenga kukabiliana na majanga mengine ambayo yangejitokeza km hili. Nakumbuka Mv Bukoba, tuliomba wazamiaji kutoka S.Afrika kuja kutuokolea watu wetu. Sasa hapa najiuliza, kwa muda muda wote huo, hatukuweza kuwapeleka watanzania wenzetu, nje, aidha hukohuko SA au pengine duniani wakapata huo ujuzi, tukaokoa angalao maiti za ndugu zetu, angalao tukazizika kwa HESHIMA. Najua serikali itajitetea haina hela. Mi naona ni heri KUPUNGUZA BAJETI YA W. UJENZI yenye matrilion, tukaendelea na tabu za barabara zetu, lkn tukawafundisha watu wetu/tukanunua VIFAA vitakavyookoa maisha ya WATANZANIA WATAKAOWEZA POTEZA ROHOO ZAO HAPO BAADAYE, wakaendelea kuishi. Nimeona kwenye TV jana na juzi, wazamiaji wetu wakisema, "....tumeenda mita 30-40 hatukuiona meli, na hatuna uhakika sehemu sahihi ilipozamia........"Hii ilinishangaza sana, kwani siku ya ajali kuna watu waliokolewa wakiwa juu ya sehemu ya hiyo meli ambayo ilikuwa bado haijazama.....cha kushangaza leo baada ya uhuru, sisi km nchi tunashindwa ku-mark point on the surface of our ocean for 2morrow reference. Ni aibuuuuuuuu. Vipo vifaa vya ku-ditect vitu ktk maji, je nchi inashindwa kuvinunuaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa. Nani azaliwe aokoe hiki kizaziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Waswahili wanasema "KUFANYA KOSA (kwa mara ya kwanza) SI KOSA. KOSA NI KULIRUDIA HILO KOSA (kwa mara nyingine). Tukiilaumu serikali yetu tutakuwatumeioneaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!


Sasa kama GLOVES hawana, unafikiri wataweza kuwa na GPS kwaajili ya ku Geo-referencing? Bora tungewaajiri wavuvi kwenye kitengo cha uokoaji, maana wao wana mbinu zaidi za ku-mark point eneo husika kwa uzoefu na usahihi zaidi.
 
Sasa unadhani watafanyaje na vifaa hawana.
Nilimsikia Mhe. Mwaakyembe akisema kuwa "hii ajali imetokea ghafla, hatukuwa tumejitayarisha."
Kwanza hiyo pekee inachekesha, kuna ajali inayokuambia ninakuja jitayarishe?
Pili, ni mwaka tu sasa ilitokea ajali kaitka mazingira kama yale na Serikali zote au yote (kwani SMZ waliahidi na SJMT) waliahidi kuwa janga kama lile lisingetokea tena.

Tuseme mwaka mmoja ulikuwa kidogo angalau kujipanga tu kwa vifaa? - boti, mafuta, waokoaji, machela, mablanketi, gloves.... Ajali imetokea saa saba, uokoaji unaanza saa 11...Boti hazipo, zilizopo hazina mafuta, KMKM hawaju uokozi au hawapo wa kutosha, wanawataka wanannchi wanaojua kuogelea waende wakaokoe maiti.....Serikali imekaa kama mchezo wa kuchekesha. Bora akina Mzee Pwagu na Pwaguzi walikuwa na mantiki katika vichekesho vyao, kwani yao yalikuwa maigizo na hii ni serikali.

Aiseee, najisikia hamu nimlambe mtu japo kibao hapa, lakini sijui nani!
 
Back
Top Bottom