Nisipo shukuru sitaeleweka kwa hili
Nilikata ticketi ya kwenda Mbeya from Dar tarehe 27 Jumamosi July 2013 ili 28th July 2015 nikielekea Mbeya kwa gari ya New Force, nilikata tiketi ya kwangu mimi na watu wengine watatu hao watu walitakiwa kupandia Morogoro
Basi lilipo fika Morogoro saa tatu hili likawa limejaa na agent wao akajifanya kuwa mkali kinoma, tulipanda kwenye hilo basi number T 222CLU na kusafiri nalo kama km 20 kuna mahala mabasi yanashusha kuchimba dawa pamoja na kula nyama choma, tukashushwa eti tusubiri basi la nyuma yake, sabavu tuliyopewa ni kuwa walikosea kukata tiketi. Konda akatuacha hapo akasepa
Tulipo kaa masaa mawili tukaamua kuwapigia viongozi wa hiyo kampini na walicho kifanya ni hiki, "ukijieleza kwenye simu ukamaliza jamaa anakwambia hajaelewa na urudie tena" tukakata tamaa, nikaamua kumpigia askari usalama barabarani nikamweleza akaniambia imekula kwangu.
Nikamamua kumpigia Mwamedi Mpinga kwa namba alizotutangazia through matangazo ya TZ, akapokea mkuu akatusikiliza akaniuliza unahuakuka nikamwambia ndio
Ndugu zangu kilicho fuata basi lilizuiliwa Iringa, Konda akakamatwa Na nauli zetu zikarudishwa tukapanda usafiri mwingine
THANK YOU KAMANDA MPINGA "MUNGU WANGU AKUBARIKI NA KUKULINDA" Thanks Kwamara yakwanza nimepata msaada polisi