Aibu: Meya Gaudence Lyimo apata kura 0

Aibu: Meya Gaudence Lyimo apata kura 0

Mungi

JF Gold Member
Joined
Sep 23, 2010
Posts
16,975
Reaction score
9,580
Wakuu,
Ni ukweli usiopingika kuwa Lolote litakalofungiwa Duniani pia litakuwa Limefungiwa Mbinguni, na Lolote litakalokataliwa Duniani litakuwa limekataliwa Mbinguni!

Ni hivi:
Leo kulikuwa na uchaguzi wa kumpata mwenyekiti wa Parokia ya Kijenge iliyopo kata ya Olorieni hapa Arusha, ambapo Meya(wa kichina) wa Jiji la Arusha Gaudence Lyimo alikuwa mwenyekiti hapo awali. Huwa kunakuwa na taratibu za kumpata mwenyekiti kila baada ya miaka mitatu. Sasa leo viongozi kutoka vigango vya parokia ya Kijenge waliamua kupiga kura ya mwenyekiti. Kulikuwa na majina mawili la Gaudence Lyimo na Nicas Lila. Wapiga kura walikuwa 58.
Kura zikapigwa, Meya wa Kichina Gaudence Lyimo ambaye wakati kura zinapigwa alitokomea alipata kura 0, Nicas Lila alipata Kura zote 58.

Pia kwa kuweka Kumbukumbu sawa, Jumapili ya tarehe 21 July kulikuwa na uchaguzi wa mwenyekiti wa kigango cha kijenge. Katika uchaguzi wa kigango huyu huyu Nicas Lila alimpiga chini Gaudence Lyimo aliyepata kura 1 Nicas Lila alishinda kwa kura 260.

Baada ya uchaguzi baadhi ya watu walikuwa wakizungumza kuwa Gaudence Lyimo mwaka wa 2010 mwezi kama huu wao walimchagua kuwa mwenyekiti wa kigango na parokia ya kijenge, sifa hiyo ikampa nguvu na umaarufu uliomfanya apate ushindi wa udiwani, matokeo yake anakwenda kukalia umeya ambao hakuupata kwa haki, na bado anaendelea kukalia kiti cha damu. Watu waliuawa Januari 5 2011 kwa ajili yake, madiwani wakafukuzwa kwa ajili yake, bomu la soweto likaua watu kwa ajili yake, sasa tumemkataa kanisani na kwenye jamii.
Kwa ujumla mengi yalisemwa .....

Huyu ndiyo Meya Gaudence Lyimo


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Hii inadhihirisha kuwa Gaudence Lyimo amechokwa na wananchi, siyo kanisani, msikitini na kwa jamii yote

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Damu za innocent people siyo mchezo, fedheha itaanzia hapahapa duniani kama ilivyotokea kwa Mwigulu na kamkutano chake jana. It is just a beginning
 
Amechokwa na wananchi amechokwa na hicho kikundi cha watu 58?

Inasikitisha kuona kuwa mtu huwezi kuwa mwana CHADEMA mpaka uwe mzandiki kama huyu Mungi.

Sasa huu uchaguzi unadhani unaweza kuthibitisha kuwa meya Lymo amechokwa?

BTW, sidhani kama taarifa yako ina tija kwa maana madiwani wenu wote wameridhia kufanya nae kazi kama meya wa jiji la Arusha.
 
Tupilia mbali magamba. sisi tunataka mtu kipenzi cha watu ambaye hatumiki kisiasa kama kondom.
 
Tumemchoka kiukweli huku Arusha kama CCMni wajanja wamtoe tu huyu meya wa Kichina.
 
Eti uchaguzi wa Kigango! Halafu mtu analeta hiyo habari kwenye jukwaa la siasa. Niseme nini juu ya uelewa wa mtu kama huyu? Hajaenda shule? Akili zimepungua? Alipata ajali ya kichwa? Au aliugua degedege utotoni? Niseme nini?
 
Inamaana hata yeye hakujipigia kura!?

Aibu hii...ukiona hadi waumini wenzako wanakukataa jua...
 
Amechokwa na wananchi amechokwa na hicho kikundi cha watu 58?

Inasikitisha kuona kuwa mtu huwezi kuwa mwana CHADEMA mpaka uwe mzandiki kama huyu Mungi.

Sasa huu uchaguzi unadhani unaweza kuthibitisha kuwa meya Lymo amechokwa?

BTW, sidhani kama taarifa yako ina tija kwa maana madiwani wenu wote wameridhia kufanya nae kazi kama meya wa jiji la Arusha.

Waliomkataa ni kikundi kinachowakilisha familia zaidi ya 50.Uliza ni namna gani uchaguzi huu huwa unafanywa,siyo namna unayofikiria.Hao watu 58 ni viongozi waliochaguliwa kwenye mitaa ya kanisa husika.Kwa mantiki hiyo ni rahisi sana kwa mama huyo kutopata huo Udiwani tena.
 
Amechokwa na wananchi amechokwa na hicho kikundi cha watu 58?

Inasikitisha kuona kuwa mtu huwezi kuwa mwana CHADEMA mpaka uwe mzandiki kama huyu Mungi.

Sasa huu uchaguzi unadhani unaweza kuthibitisha kuwa meya Lymo amechokwa?

BTW, sidhani kama taarifa yako ina tija kwa maana madiwani wenu wote wameridhia kufanya nae kazi kama meya wa jiji la Arusha.

Hao watu 58 ni wakazi wa Arusha pia...na hao ni wachache tu kuna maelfu kama hao wapo huko mitaani, hiyo ni dalili mbaya kwamba huyo bwana hakubaliki sio kanisani tu hata huko mtaani.
 
Sasa we Juliana mbona unajichanganya?
Amekataliwa na viongozi waliopiga kura kwenye vigango, yeye akaambulia kura yake moja, huku mwenzake akalamba kura 260.
Bado kwenye parokia ameambulia sifuri....

Hebu utueleze kuhusu mkutano wa Mwigulu jana..

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Tatizo haelewi namna ambavyo kanisa linapata viongozi wake.
 
Sasa jamani Lymo.....alikuwa anagombea ili iweje kama hata yeye mwenyewe amekosa imani na uongozi wake kiasi cha kutojipigia hata kura yake mwenyewe?
 
Amechokwa na wananchi amechokwa na hicho kikundi cha watu 58?

Inasikitisha kuona kuwa mtu huwezi kuwa mwana CHADEMA mpaka uwe mzandiki kama huyu Mungi.

Sasa huu uchaguzi unadhani unaweza kuthibitisha kuwa meya Lymo amechokwa?

BTW, sidhani kama taarifa yako ina tija kwa maana madiwani wenu wote wameridhia kufanya nae kazi kama meya wa jiji la Arusha.
...we kilaza unapotoa hoja jipange u justify uhalali wa bk 7. Sasa hao 58 ni wanyaruanda au wasomali. The point here ni kwamba meya wa kichina kagonga pua chini...
 
Ha! Ha! Ha! Malipo ni hapahapa , kuna mwingene jana amehutubia viti !
 
Sasa jamani Lymo.....alikuwa anagombea ili iweje kama hata yeye mwenyewe amekosa imani na uongozi wake kiasi cha kutojipigia hata kura yake mwenyewe?

Alipogundua mgombea mwenzake kwenye uenyekiti wa parokia ni yule yule aliyempiga chini kwenye kigango ikabidi atokomee haraka...


Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Amechokwa na wananchi amechokwa na hicho kikundi cha watu 58?

Inasikitisha kuona kuwa mtu huwezi kuwa mwana CHADEMA mpaka uwe mzandiki kama huyu Mungi.

Sasa huu uchaguzi unadhani unaweza kuthibitisha kuwa meya Lymo amechokwa?

BTW, sidhani kama taarifa yako ina tija kwa maana madiwani wenu wote wameridhia kufanya nae kazi kama meya wa jiji la Arusha.

Wewe wazimu kweli kweli hivi una umri gani you human being? maake sijawahi kuona point kutoka kwako kila kitu wewe unabishia tu bila kufanyia uchunguzi sasa kama Meya wa Kichina kapata kura ZERO au tusema hakuna sasa na hapo tu bado hujaelewa alichoandika Mungi??Hadi uanze kuminyana lol ama kweli kuna watu na viatu wewe unafaa sana kwa sifa hii,hebu jaribu kuwa makini si kila hoja ujibu,kwani hata ukiacha bado utabakia Hammy D tu.
 
Safi kabisa, sasa hivi adhabu za madhambi zinaanzia hapa hapa duniani.
 
Back
Top Bottom