Aibu kubwa

Aibu kubwa

hakuna duka linalouza utu, heshima, heri kufa maskini kuliko kuua mwili na roho na kwa sababu ya hela
 
Mkuu Asprin hiyo like yako hata siielewi maana yake. Ume like hilo tukio au ume like nini?
 
Jana mchana wa saa 8 hivi niliona kituko na nikahisi aibu sana. Nilikuwa ndani ya posta ya Meru(Arusha) kwenye foleni ya dirisha la Western Union. Watu walikuwa wengi wakisubiri kuhudumiwa na wengi tulisimama kwani viti ni vichache. Nilipochoka kusimama nikatupa macho sehemu kwenye viti kama kuna upenyo nikae. Lahaula! Nilimwona kijana wa kiume wa Kiarika mwenye umri kati ya miaka 20-25 akiwa ameketi na mama mzee wa kizungu asiyepungua miaka 60. Uzee wa huyu bibi ulionekana wazi kwani hata ngozi yake ilikuwa imekunjamana na kupwaya. Mama huyo alikuwa amekumbatiwa na huyo kijana kwa mkono mmoja na mkono wa pili wa kijana ulikuwa busy akimkuna kuna bibi kizee yule na kumpapasa papasa kimapenzi. Bibi alikuwa ametulia tuli akionesha kuwa anafurahia zoezi la kijana. Kila mtu pale karibu yao alikuwa akiwatazama lakini kijana hakujali, alikuwa serious na kazi yake. Nilihisi aibu sana kwa sababu yule kijana alikuwa mtoto sana kwa yule bibi na pia niliogopa kuendelea kuwatazama kwa sababu nilihisi yule kijana ni mwanangu nikajikuta nataka nikamchape kibao aache ujinga ule. Mama wa kizungu akaitwa akachukue pesa dirishani. Wakapelekana akiwa bado kakumbatiwa. Mama alipokea pesa akampa mtoto akaziweka kibindoni, haooo wakaondoka wakisindikizwa na macho kama 50 hivi. Jamani! ndo nini hii? Mungu tuhurumie.



Sasa wewe unashangaa nini kwa kijana mwenye umri kama huu kutembea na kikongwe? Kuna dada zetu tunawafahamu ila hatutaki kuwataja humu JF wako in their mid 30's wameolewa na wazee wa kizungu in their late 60's. Waswahili wanasema akili mu kichwa, hupo hapoooo?
 
Sasa wewe unashangaa nini kwa kijana mwenye umri kama huu kutembea na kikongwe? Kuna dada zetu tunawafahamu ila hatutaki kuwataja humu JF wako in their mid 30's wameolewa na wazee wa kizungu in their late 60's. Waswahili wanasema akili mu kichwa, hupo hapoooo?
Umri ni jambo moja ila issue kubwa ni vile vitendo alivyokuwa akifanya huyu mtoto hadharani. Hapo ndipo AIBU ilipokita zaidi. Kuweka maadili pembeni ndo akili mu kichwa? Haya wee.
 
Wacha vijana watafute pesa,hali ngumu ndio maana hata mamayeyo wenzako wana ... tek mi foto giv mane.
 
Umri ni jambo moja ila issue kubwa ni vile vitendo alivyokuwa akifanya huyu mtoto hadharani. Hapo ndipo AIBU ilipokita zaidi. Kuweka maadili pembeni ndo akili mu kichwa? Haya wee.


Yaani wewe? Unashangaa nini? Dada zetu huko majuu wanalazimishwa kufanya mambo ya hajabu na vizee vyao hadharani mbona hawajifichi? Njoo hapa Dar maeneo ya Coco Beach au kule Kigamboni utaona wazee wa kitanzania (vigogo) wa miaka 60+ na visichana vya kibongo fleva wakila bata. Mtoto wa miaka 17 anapakatwa na kikongwe mvi toka matakoni mpaka nyusoni na demu haoni noma anachekelea tu huku akipapaswa matiti. Au ni kwa kuwa mzungu yuko na mbongo mnaanza kulalamika. Wamependana ni kivyao nyie ama sie havituhusu. Waacheni wale raha zao, alaaaaaaa!:A S angry:
 
Yaani wewe? Unashangaa nini? Dada zetu huko majuu wanalazimishwa kufanya mambo ya hajabu na vizee vyao hadharani mbona hawajifichi? Njoo hapa Dar maeneo ya Coco Beach au kule Kigamboni utaona wazee wa kitanzania (vigogo) wa miaka 60+ na visichana vya kibongo fleva wakila bata. Mtoto wa miaka 17 anapakatwa na kikongwe mvi toka matakoni mpaka nyusoni na demu haoni noma anachekelea tu huku akipapaswa matiti. Au ni kwa kuwa mzungu yuko na mbongo mnaanza kulalamika. Wamependana ni kivyao nyie ama sie havituhusu. Waacheni wale raha zao, alaaaaaaa!:A S angry:
Kwa sababu hao wote uliotaja wanafanya hayo mambo bado haihalalishi kuwa ni sahihi. Usiwe na hasira kwa watu kutoa maoni yao. Jambo zuri au baya lazima lisemwe tu.
 
Wazungu wana usemi wao maarufu "Age ain't nothing, just a number" ambao wanautetea sana hasa wanawake vikongwe wanaokuja hapa Arusha kwa sex tour. Mungu ninusuru!
 
Kwa sababu hao wote uliotaja wanafanya hayo mambo bado haihalalishi kuwa ni sahihi. Usiwe na hasira kwa watu kutoa maoni yao. Jambo zuri au baya lazima lisemwe tu.


Nani aliyesema kupakatwa na mze ni makosa? Mpende akupendaye. Nimejibu na wala sina hasira.
 
ahahahahah ahahaha pole kamanda unashangaa nini hapo maana yaani ishu ya kijana hapo kuendelea kumpapasa bb sio kubwa kaamua labda angebakwa utandawazi ni kwere
 
Umri ni jambo moja ila issue kubwa ni vile vitendo alivyokuwa akifanya huyu mtoto hadharani. Hapo ndipo AIBU ilipokita zaidi. Kuweka maadili pembeni ndo akili mu kichwa? Haya wee.

Inaonyesha ww ni mgeni ktk sayari ya mapenzi, kwahiyo ww ulitaka wakafanyie wapi? Aibu ni wa2 kukatana goli hadharani lakini sio kushikana shikana. Labda useme walikurusha roho!
 
Jana mchana wa saa 8 hivi niliona kituko na nikahisi aibu sana. Nilikuwa ndani ya posta ya Meru(Arusha) kwenye foleni ya dirisha la Western Union. Watu walikuwa wengi wakisubiri kuhudumiwa na wengi tulisimama kwani viti ni vichache. Nilipochoka kusimama nikatupa macho sehemu kwenye viti kama kuna upenyo nikae. Lahaula! Nilimwona kijana wa kiume wa Kiarika mwenye umri kati ya miaka 20-25 akiwa ameketi na mama mzee wa kizungu asiyepungua miaka 60. Uzee wa huyu bibi ulionekana wazi kwani hata ngozi yake ilikuwa imekunjamana na kupwaya. Mama huyo alikuwa amekumbatiwa na huyo kijana kwa mkono mmoja na mkono wa pili wa kijana ulikuwa busy akimkuna kuna bibi kizee yule na kumpapasa papasa kimapenzi. Bibi alikuwa ametulia tuli akionesha kuwa anafurahia zoezi la kijana. Kila mtu pale karibu yao alikuwa akiwatazama lakini kijana hakujali, alikuwa serious na kazi yake. Nilihisi aibu sana kwa sababu yule kijana alikuwa mtoto sana kwa yule bibi na pia niliogopa kuendelea kuwatazama kwa sababu nilihisi yule kijana ni mwanangu nikajikuta nataka nikamchape kibao aache ujinga ule. Mama wa kizungu akaitwa akachukue pesa dirishani. Wakapelekana akiwa bado kakumbatiwa. Mama alipokea pesa akampa mtoto akaziweka kibindoni, haooo wakaondoka wakisindikizwa na macho kama 50 hivi. Jamani! ndo nini hii? Mungu tuhurumie.

MASKINI NDUGU ZANGU,
YOTE HAYO NI SHAURI YA KUIWEKA CCM MADARAKANI,LAKINI POA TUH SI TUMEJITAKIA,,

SWALI LA KIZUSHI,,,'KWANI NGO'MBE ANAZEEKA MAINI??
:madgrin:
 
mkuki kwa nguruwe,usikute hapo angemuona mtoto wa kike yupo na kibabu cha kizungu wala wasingeshaa,mbona wapo wengi??tutaje tusitaje..

Wanasema,ukitaka kufaidi chagua dogo dogo,sijui wana maanishaga nini,dunia imeisha
 
Gambia, kule Afrika magharibi kuna utalii unaitwa SEX TOURISM. Ni zaidi ya hicho ulichokiona hapo.
 
Vijana wa kibongo Wake kwa Waume tumekua VIKARAGOSI kwa hivi VINYANYA VYA MAGHARIBI NA AMERIKA sababu ya uvivu wa kufikiri na kufanya kazi. Hiyo umeona Arusha sasa huko ugahibuni ndo balaa .
 
ahahaaaaaa kumbe wengi tumemshangaa huyu kijana....ni bounser pale Pin Point....Yaani ni full kioja...hizi njaa zitawaathiri vijana wanaopenda kubweteka mkuu
Jamani hioz ndo ajira alizotengeneza muheshimiwa jk vijana wamekula shavu mradi maisha yanasogea
 
Back
Top Bottom