AG amemdhalilisha Halima Mdee bungeni

AG amemdhalilisha Halima Mdee bungeni

Omokenye wa kiagata
ha ha ha yani huyu jamaa ni mkurya mwenzangu rakini uwezo wake ni finyu sana...mura weito pore sana sasa cha kufanya kwa sababu unapingana na mchakato wa kupata katiba mpya basi itabidi urudi tarime kwenu kwa sbabu najua ungejitahidi sana tupate katiba mpya ingesaidia hata watoto wetu pare tarime wasitairiwe ha ha ha ha ha ha broken toking werema mura wa bhairighe or bharenchoka
 
Kwani AG anataka kuolewa? mbona anataka kujua kama Mdee ni mwanaume yeye ana shida gani na wanaume? Sina uhakika kama huyu jamaa ni mkurya kweli labda mamake alifanya mchezo mchafu, wakurya hawako hivyo!
 
Mimi sikumwelewa Mh. Halima Mdee kwani yeye mwenyewe alikuwa anacheka tu!
 
MLENGWA WA MLIPUKO ALIKUWA BALOZI WA VATICAN?

(Naona mods wana watu wao wenye haki ya kuanzisha threads, sisi wengine haturuhusiwi)

Ndugu WanaJamvi;

Kwa muda sasa kumekuwa na hoja mbali mbali juu ya uhalali wa uwepo wa Ubalozi wa Vatican hapa Tanzania. Katika hili kuna, kuna pande kuu mbili zinazokinzana - wanaopinga na wanaounga mkono kama ifuatavyo:-

(1) Wanaopinga: wanajenga hoja kwamba kwa kuwa Vatican ni nchi ya kidini (Kikatoliki) na kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba, Tanzania haina dini hivyo sio sahihi kwa "nchi" hiyo kuwa na ubalozi wake hapa nchini. Wengine wanaenda mbali zaidi kiasi kwamba hawataki kukubali Vatican ni nchi. Hata hivyo "wanalegeza" masharti kwamba kama Vatican ina ubalozi wake hapa basi ni halali kwa Tanzania kama nchi kuwa mwanachama wa taasisi za kidini kama OIC. La kushangaza hapa ni kwamba kwao uhalali wa Ubalozi wa Vatican utakuwepo endapo Tanzania itakuwa mwanachama wa hizo taasisi za kidini vinginevyo sio halali.

(2) Wanaounga mkono:hawa wanajenga hoja kwamba; kwanza Vatican ni nchi huru, yenye mamlaka kamili, na inayojitegemea kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya neno "nchi" lilivyo na linavyotambulika kimataifa. Na wanaenda mbali zaidi kwamba sio tu kwamba Vatican ni nchi bali inatambulika hivyo rasmi na UN. Hivyo, kwa hoja hii, ni sahihi kabisa Vatican na Tanzania kuwa na mabalozi wanowakilisha nchi zao.

MLIPUKO WA LEO:

Kati ya viongozi wakuu wa Kanisa waliokuwepo kwenye shughuli ya leo kule Olasiti, Arusha, ni Balozi wa Vatican nchini Tanzania ambaye pia ana hadhi ya Askofu Mkuu. Hivyo zimeanza kuzagaa habari pengine kutokana na ukinzani wa baadhi ya makundi kutotaka Vatican kuwa na ubalozi wake hapa nchini, kuna uwezekano pia mlengwa mkuu alikuwa Balozi husika. Mimi sijui, ila kama GT tudadavue na hili.

LAWAMA:

Lawama pia zimeanza kuelekezwa kwa serikali kwa kutochukua hatua madhubuti na kwa wakati pindi zinapotokea chochoko kama hizi katika jamii. Kwa mfano, hili la upotoshoji wa uhalali wa Ubalozi wa Vatican hapa nchini propaganda zake zimeenezwa kwa muda mrefu sana kwa njia mbalimbali kama mihadhara, ibada, na hata kwenye media mbalimbali. Badala ya serikali kutolea ufafanuzi wa uhalali wa huo ubalozi, imekuwa kimya bila kujali athari za baadaye za propaganda hizi chafu pengine kwa falsafa ya "ni upepo tu utapita". Je, ni kweli serikali inastahili lawama katika hili?

HITIMISHO:

Je, kama serikali ikitekeleza madai YOTE ya haya makundi, kuna uwezekano wa chokochoko hizi kukoma na hivyo nchi yetu kuwa ya amani na utulivu kama ilivyoachwa na waasisi wetu? Lakini je, walengwa wa haya matukio ni wakatoliki peke yao? Au ni pamoja na makundi mengine? Haya matukio yana uhusiano wowote na siasa za nchi yetu? Mimi sijui, nalileta kwenu wakuu.
 
Ni jambo la aibu kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali kutumia muda wa takriban dakika tatu kuelezea tofauti kati ya woman, Lady na Gentleman na kusema kwamba anashindwa kujua kama Halima Mdee ni Lady au Gentleman.

Kwa kweli kuangalia Bunge ni kichefuchefu tupu na hizi Ndioooooooooooo zao!!

Hivi AG hajui kuwa Halima Mdee ni .........naogopa kung'olewa kucha.
 
MLENGWA WA MLIPUKO ALIKUWA BALOZI WA VATICAN?

(Naona mods wana watu wao wenye haki ya kuanzisha threads, sisi wengine haturuhusiwi)

Ndugu WanaJamvi;

Kwa muda sasa kumekuwa na hoja mbali mbali juu ya uhalali wa uwepo wa Ubalozi wa Vatican hapa Tanzania. Katika hili kuna, kuna pande kuu mbili zinazokinzana - wanaopinga na wanaounga mkono kama ifuatavyo:-

(1) Wanaopinga: wanajenga hoja kwamba kwa kuwa Vatican ni nchi ya kidini (Kikatoliki) na kwa kuwa, kwa mujibu wa Katiba, Tanzania haina dini hivyo sio sahihi kwa "nchi" hiyo kuwa na ubalozi wake hapa nchini. Wengine wanaenda mbali zaidi kiasi kwamba hawataki kukubali Vatican ni nchi. Hata hivyo "wanalegeza" masharti kwamba kama Vatican ina ubalozi wake hapa basi ni halali kwa Tanzania kama nchi kuwa mwanachama wa taasisi za kidini kama OIC. La kushangaza hapa ni kwamba kwao uhalali wa Ubalozi wa Vatican utakuwepo endapo Tanzania itakuwa mwanachama wa hizo taasisi za kidini vinginevyo sio halali.

(2) Wanaounga mkono:hawa wanajenga hoja kwamba; kwanza Vatican ni nchi huru, yenye mamlaka kamili, na inayojitegemea kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya neno "nchi" lilivyo na linavyotambulika kimataifa. Na wanaenda mbali zaidi kwamba sio tu kwamba Vatican ni nchi bali inatambulika hivyo rasmi na UN. Hivyo, kwa hoja hii, ni sahihi kabisa Vatican na Tanzania kuwa na mabalozi wanowakilisha nchi zao.

MLIPUKO WA LEO:

Kati ya viongozi wakuu wa Kanisa waliokuwepo kwenye shughuli ya leo kule Olasiti, Arusha, ni Balozi wa Vatican nchini Tanzania ambaye pia ana hadhi ya Askofu Mkuu. Hivyo zimeanza kuzagaa habari pengine kutokana na ukinzani wa baadhi ya makundi kutotaka Vatican kuwa na ubalozi wake hapa nchini, kuna uwezekano pia mlengwa mkuu alikuwa Balozi husika. Mimi sijui, ila kama GT tudadavue na hili.

LAWAMA:

Lawama pia zimeanza kuelekezwa kwa serikali kwa kutochukua hatua madhubuti na kwa wakati pindi zinapotokea chochoko kama hizi katika jamii. Kwa mfano, hili la upotoshoji wa uhalali wa Ubalozi wa Vatican hapa nchini propaganda zake zimeenezwa kwa muda mrefu sana kwa njia mbalimbali kama mihadhara, ibada, na hata kwenye media mbalimbali. Badala ya serikali kutolea ufafanuzi wa uhalali wa huo ubalozi, imekuwa kimya bila kujali athari za baadaye za propaganda hizi chafu pengine kwa falsafa ya "ni upepo tu utapita". Je, ni kweli serikali inastahili lawama katika hili?

HITIMISHO:

Je, kama serikali ikitekeleza madai YOTE ya haya makundi, kuna uwezekano wa chokochoko hizi kukoma na hivyo nchi yetu kuwa ya amani na utulivu kama ilivyoachwa na waasisi wetu? Lakini je, walengwa wa haya matukio ni wakatoliki peke yao? Au ni pamoja na makundi mengine? Haya matukio yana uhusiano wowote na siasa za nchi yetu? Mimi sijui, nalileta kwenu wakuu.

Tulijua tu kuwa mtakuja na simple assumptions kama hizi. But time will tell.
 
Watu wenye hakili ndogo wanaongoza watu wenye hakili nyingi- Mch. Msigwa(MB)
 
Jamaniiii ni utani tuu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Najaribu kufikiria kwa kelele siku Mhe Mdee aseme anashindwa amweke AG kwenye kundi gani kati ya gentlemen au ladies, huo mtiti wake
 
Ni udhalilishaji iwapo tu mnalazimishia mtazamo huo, Lakini kwa mfano wenzetu wamasai mwanamke kuingilia mwanaume akiongea ni zaidi ya kesi ya kuua..Sijui kwenye jamii zenu na hata za hao wakuria...Ninachoona hapa ni kuwa Jaji Werema amejitahidi sana kuvumilia na kuzuia hasira(tena za kikuria).

Ila na sisi tujiulize kama kwa mila zetu sio kawaida mwanamke kuingilia mwanaume anapoongea, Huyu anayethubutu kufanya hivi tena kwa mtu asiye wa rika lake, Amechagua kukaa upande wa gentleman ili "a qualify" kuingilia maongezi ya mwanaume ?

Ni nyie nyie wanaume inapokuja mjadala wa matatizo ya NDOA za kisasa aka "ndoa za dot com" kuvunjika hovyo malalamiko yenu makubwa nyie kina baba ni kuhusu mabinti wa siku hizi walivyo na tabia za kushindana na wanaume ndani ya nyumba.

pia imekuwa ni tabia ya kawaida kwa Bi Khalima kuingilia na kukosa heshima kwa waliomzidi umri. Nakumbuka aliwahi kumkwaza hata Naibu spika, tena alitumia na ishara za vidole.

Je nanyi huwa mnavumilia hali kama hizi ndani ya ndoa zenu ? Wengi mnaishia kupiga wake zenu au kupigana. Lakini kwa kuwa hatufahamiani basi UNFIKI uendelee kuchukua nafasi..
 
Wanawake mnapaswa kuungana kupinga unyanyasaji huu
 
Huyu werema ni mkrya jina tu siyo mkurya aliyezaliwa na mkurya wa kiume, labda mamake ndo mkurya lakini babake nina wasiwasi nae.
 
Wakati akichangia hoja ya sheria na katiba bungeni huku baadhi ya wabunge wakinongona,mwanasheria mkuu amemumshambulia kwa maneno makali mbunge wa Kawe Halima Mdee,amwambia hajui amweke ktk kundi la lady or gentle man.Maneno haya angeambiwa upande wao ingezua balaa na miongozo ingekua mingi bungen,hata ivo mwanasheria aliposkia muongozo aligomea kumskiliza aliyeomba muongozo kwa kusema hakuna cha muongozo hapa huku speaker akishabikia yote yaliyokua yakitokea wakati mkuu huyo anachangia!!!!!Je siku akinyanyuka Halima mdee akatoa maneno kama hayo bungeni kwa mwanasheria mkuu au waziri mtamvumilia km yeye alivyowavumilia!!!

hapo ndo patakuwa patamu. mara nyingi huwa inaudhi mwanaume kuitwa ke kulikox mwanamke kuitwa me.nafikiri siku moja mdee anatakiwa achombweze kuwa werema anajibu, mpaka huwezi kutambua km ni me au ke. jamaa atarusha ngumu hadharani.
 
Back
Top Bottom