Afrika yaendelea kukumbuka na kuenzi mchango mkubwa unaotolewa na timu za madaktari wa China

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
278.jpg


Ikiwa dunia inaadhimisha siku ya Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu na Hilali nyekundu kila ifikapo Mei 8, nchi mbalimbali hasa hza Afrika zitaendelea kukumbuka na kuenzi mchango mkubwa unaotolewa na timu za madaktari wa China katika barani humo, ambao wamekuwa mstari wa mbele kupambana na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza, na matokeo yake watumishi hawa afya wanakuwa kwenye mazingira makubwa ya hatari ya kupata maambukizi.

Tukikumbuka mlipuko wa Ebola uliotokea mwaka 2014-2015 huko Afrika Magharibi, watumishi wengi wa afya waliopelekwa kukabiliana na ugonjwa huo, waliambukizwa na baadhi yao kufariki, lakini kwa madaktari wa China wa kupambana na ugonjwa huo ambao walipelekwa kutoa huduma muhimu nchini Liberia, hakukuwepo na hata mmoja aliyeambukizwa kwasababu tayari China ina uzoefu mkubwa wa kukabiliana na magonjwa ya maambukizi mfano wa Ebola.

Mbali na ugonjwa wa Ebola, mwaka 2020 ulikuwa ni mwaka uliotanda giza totoro duniani, kwani kilishudiwa kirusi kipya kabisa kikiibuka cha corona, ambacho hadi leo bado kinaendelea kuangamiza na kuchukua roho za watu. Wataalamu wa afya wa China hawakusita wala kufikiria mara mbili kuzisaidia nchi ambazo zilikuwa na uhitaji mkubwa, nyingi zao zikiwa za Afrika.

Baada ya kupambana na virusi hivyo ndani ya nchi na kupata uzoefu wa kutosha, China ilipelekea timu zake barani Afrika ili kushikana mkono pamoja na nchi mbalimbali kuhakikisha hali inakuwa shwari.

Timu za madktari bingwa wa China zilizopelekewa Afrika, hazikushughulikia magonjwa ya kuambukiza pekee, bali zilisaidia kutibu magonjwa mengine mbalimbali, yakiwemo mtoto wa jicho, magonjwa ya uzazi n.k.

Ratymt mwenye umri wa miaka 36 anayeishi kisiwani Pemba huko Zanzibar, Tanzania, sasa amekuwa na kila sababu ya kujivunia na kutabasamu kwani amekuwa mama baada ya kuharibu mimba mara 27. Alihangaika kwa uda mrefu na alipopata ujauzito wake wa 28, alikutana na madaktari bingwa wa China, waliopelekwa Pemba kusaidia kwenye matibabu, na baada ya kuhudumiwa na madaktari hawa akaweza kujifungua mtoto wa kiume.

Wang Juan, daktari wa kitengo cha magonjwa ya wanawake na uzazi katika Hospitali ya Kwanza ya Chuo Kikuu cha Suzhou, ambaye yupo kwenye timu ya 31 ya madaktari bingwa wa China wanaotoa msaada huko Zanzibar, alieleza shida na tabu alizokumbana nazo mgonjwa huo katika kipindi chote anatafuta ujauzito.

“Mwanamke huyo alipata ujauzito mara 28, lakini mimba zote ziliharibika, halafu alikuja Hospitali ya Abdulla Mzee kwa matibabu akiwa na ujauzito wa wiki 14.” alisema dokta Wang

Wakati huo timu ya madaktari wa China ilikuwa imeanza kutoa huduma za matibabu katika Hospitali ya Abdulla Mzee kwa mwaka mmoja. Hali ya Ratymt ilifuatiliwa sana na madaktari wa China. Ikilinganishwa na hali yake ya hapo zamani, baada ya kufanya uchunguzi, madaktari wa China waligundua kuwa chanzo cha kuharibika kwa ujauzito wake ni shingo ya uzazi kutokuwa na uwezo wa kuhimili mimba. Hivyo madaktari waliamua “kufunga kamba” kwenye shingo yake ya uzazi, ili kumsaidia mwanamke huyo kumlinda mtoto wake.

Wang Juan anasema, ingawa hivi sasa upasuaji huo ni wa kawaida nchini China, lakini huko Zanzibar umefanyika mara chache tu. Licha ya kumfanyia upasuaji, madaktari pia waliweka mpango wa nusu mwaka wa kusimamia na kufuatilia hali ya ujauzito ya Ratymt, ili kuhakikisha usalama wake. Wakati Ratymt alipokuwa na ujauzito wa wiki 37, Wang Juan akishirikiana na madaktari wa Afrika walimfanyia upasuaji, na akajifungua mtoto wa kiume.

Kutokana na tatizo la lugha, Ratymt hakuweza kuwasiliana moja kwa moja na madaktari wa China, lakini aliendelea kutoa shukrani zake kwa madaktari wa China kupitia madaktari wa Pemba, kwa kumtoa kimasomaso na kumfanya naye atambe kwa watu kwamba sasa amekuwa mama.

Wang Juan pia anajionea ufahari mkubwa kwa jukumu analobeba akiwa kama daktari wa timu ya matibabu inayotoa msaada nje ya nchi.

“Nataka kutoa msaada ili kupunguza kiwango cha vifo vya uzazi na vifo vya watoto wachanga kwa wenyeji. Pia natumai kuwasaidia kutoa mafunzo, kuboresha elimu ya nadharia, na ustadi wa kimsingi. Bado kuna mengi nitakayoweza kufanya.” alieleza dokta Wang

Zanzibar ni mfano mmoja tu lakini naamini kuna nchi nyingi za Afrika ambazo zina wanawake wanaosumbuliwa na matatizo kama haya, na baada ya wataalamu wa China kufika wamewafunua nyuso wanawake hao kwa kuwapatia huduma zinazohakikisha kwamba wanatapa watoto. Waswahili wanasema “Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi Mungu” Kwa mema mengi yanayofanywa na China kwa rafiki zake wa sehemu mbalimbali duniani, yanastahili kupongezwa na kuenziwa.
 
Back
Top Bottom