DOKEZO Afisa utumishi, PSSF wachezea mfumo na kumstaafisha mtumishi kabla ya muda, alilipwa Milioni 72, akapokea Milioni 2 tu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Ofisa Utumishi mmoja ambaye alihudumu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu kwa kushirikiana na Afisa kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii PSSF wanaida kuchezea mfumo na kusataafisha watumishi wa serikali kabla ya muda.

Licha ya Maafisa hao kitendo hicho, mtumishi huyo alilipwa Milioni 72 kama mafao yake baada ya kustaafishwa, jambo la kinyama na la kuumiza zaidi ulifanywa mchezo na taasisi moja ya kifedha iliyokuwa inamdai mtumishi huyo ambapo alikatwa kiasi Cha Sh. Milioni 70, na kumbakizia kiasi cha Sh. Milioni 2.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda leo kwenye kikao cha Baraza maalumu la Madiwani Halmashauri ya Mji wa Bariadi la kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG), ndiye ameeleza jambo hilo.

Dkt. Yahaya Nawanda amesema kuwa kitendo hicho ni cha kinyama, ambapo ameagiza Maafisa hao kutafutwa popote walipo hata kama wamehamishwa na amehaidi kupambana nalo hadi hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Amesema kuwa Maafisa hao walikuwa wanachezea mfumo wa utumishi, ambapo mtumishi anashtukia anapigiwa simu kuwa anastaafu jambo ambalo siyo kweli, lengo likiwa ni kutaka kujipatia fedha kwa njia haramu.

“Huyu Afisa utumishi na afisa wa PSSF baada ya kufanikiwa kumstaafisha, huyu mtumishi kuna kampuni moja ya kifedha ilikuwa inamdai, wakala njama, akaingiziwa penshioni yake Milioni 72, walichomfanyia ni kitu cha kinyama, wakamtaka Milioni 70 akabaki na Milioni mbili tu” amesema Nawanda….

“ Nimeagiza uchunguzi uanze mara moja, tunakwenda kuunda tume tuchunguze jambo hili, lakini huyu Afisa Utumishi na Afisa wa PSSF watafutwe popote walipo waje hapa watueleze kwani nini walifanya jambo hili,” ameeleza Nawanda.

Chanzo. simiyublog.

View attachment 2665711
Aseee! Ni ushetani mkubwa sana.
 


Alafu ela za zambi hvyo anatamba nazo na kujiona yeye mpambanaji wengine tunabak kutumia kichwa jamaa mbona anatoboa.
Kumbe huwa unapoteza muda kuwaza watu? Utakufa braza!

Hata wasioiba wanaroga balaa, kawaangalie Wakinga pale Kariakoo wanavyoroga...

Shauri yako
 
Hao Bank wanamkopeshaje mtu anayekalibia kustaafu? Lets say amebakiza miaka mi5 je kwa calculations zao kwa huo muda wa miaka 5 hiyo hela ingerudi? Ukizingatia AJIRA yake ndio dhamana ya Mkopo?

Kuna kitu sijakielewa.. je huy mtumishi alikopa kias gani..? Muda aliokopa ni upi? Na kama alikopa je terms za kurudisha mkopo upoje..? Haiwezekan mkopo wa miaka 7 wewe uchukue hela yako ndani ya miaka miwili...


Haya turud ktk kanuni na taratibu za kibenk.. je ni sahihi kunyofoa hela zote hizo bila kuruhusiwa na mwenye account..

Je kiwango cha kurudisha mkopo kwa mkupuo ndio kipo hivyo?

Kuna maswali mengi kwa uelewa wangu mdogo nashindwa kudadavua hii ishu.
 
Hapo PSSSF kuanzia makao makuu Dodoma pameoza.

Hicho kitengo cha Huduma kwa wateja wanatumia hiyo ofisi kutapeli wastaafu wengi tu.

Kinachofanyika ni pale mstaafu akiwasiliana nao kuomba ufafanuzi kwa mawasiliono ya ofisi wao humpigia kwa namba zao binafsi na kifuatacho ITV ni kwamba hupotoshwa na kutapeliwa.

Either wanashirikiana na watu wa nje ya PSSSF kwa kuwapatia taarifa za wazee hao ili wapigwe au wenyewe kabisa wanasimamia show.

RB zipo kila mahali ila cha kushangaza hakuna hatua za maana zimechukuliwa.

Polisi kitengo cha cyber kingebinafsishwa wakapewa watu competent.
 
Hapo PSSSF kuanzia makao makuu Dodoma pameoza.

Hicho kitengo cha Huduma kwa wateja wanatumia hiyo ofisi kutapeli wastaafu wengi tu.

Kinachofanyika ni pale mstaafu akiwasiliana nao kuomba ufafanuzi kwa mawasiliono ya ofisi wao humpigia kwa namba zao binafsi na kifuatacho ITV ni kwamba hupotoshwa na kutapeliwa.

Either wanashirikiana na watu wa nje ya PSSSF kwa kuwapatia taarifa za wazee hao ili wapigwe au wenyewe kabisa wanasimamia show.

RB zipo kila mahali ila cha kushangaza hakuna hatua za maana zimechukuliwa.

Polisi kitengo cha cyber kingebinafsishwa wakapewa watu competent.
Mimi uncle wangu aliyekuwa Afisa Mwandamizi EAC walimtengenezea cheti feki cha kifo na wakakomba mafao yake na pensheni zote 100%.

Siku alipozuka kuzichukuwa mwaka 2012 baada ya Mahakama ya Tz kuamuru walipwe, wale staffs wa huduma kwa mteja baada ya kuangalia kwenye mfumo wa tarakilishi (computer) wakapiga ukunga/yowe/nduru kuwaita staffs wenzao eti wamezukiwa na mzimu.

Walipofika staffs hao na kuuliza mzimu upi, wakamwonyesha huyo hapo (yaani uncle wangu).

Uncle alipouliza ni kwa vipi wamnyanyapae kiwango hicho kwa kumuita mzimu wakati amekuja kudai haki zake?

Wakasema mfumo unaonyesha wewe ni marehemu tangu mwaka 1985 na kivuli cha cheti cha kifo hiki hapa kwenye tarakilishi na mafao uliishachukuwa ushahidi huu hapa na mwenzi wako alichukuwa nusu pensheni hadi 1986.

Wale staffs walioitwa kushuhudia mzimu wakayeyuka, uncle puuuuu.... chini, pepewa pepewa pale na walinzi, fahamu ziliporudi akaacha laana ya karne (kama serikali inalaanika sijui!?) na kuondoka hapo Hazina Makao Makuu hadi leo yuko hai Kijijini kama EL kule Peninsular; na akasusa kabisa kurudi Hazina.

Aina hii ya watumishi ndiyo wamejaa serikalini na ndiyo watafanya models kama za akina Makonda zisiishe nchi hii, zitakuja na kutoweka na kurudi tena na kutoweka tena na kurudi...
 
Mimi uncle wangu aliyekuwa Afisa Mwandamizi EAC walimtengenezea cheti feki cha kifo na wakakomba mafao yake na pensheni zote 100%.

Siku alipozuka kuzichukuwa mwaka 2012 baada ya Mahakama ya Tz kuamuru walipwe, wale staffs wa huduma kwa mteja baada ya kuangalia kwenye mfumo wa tarakilishi (computer) wakapiga ukunga/yowe/nduru kuwaita staffs wenzao eti wamezukiwa na mzimu.

Walipofika staffs hao na kuuliza mzimu upi, wakamwonyesha huyo hapo (yaani uncle wangu).

Uncle alipouliza ni kwa vipi wamnyanyapae kiwango hicho kwa kumuita mzimu wakati amekuja kudai haki zake?

Wakasema mfumo unaonyesha wewe ni marehemu tangu mwaka 1985 na kivuli cha cheti cha kifo hiki hapa kwenye tarakilishi na mafao uliishachukuwa ushahidi huu hapa na mwenzi wako alichukuwa nusu pensheni hadi 1986.

Wale staffs walioitwa kushuhudia mzimu wakayeyuka, uncle puuuuu.... chini, pepewa pepewa pale na walinzi, fahamu ziliporudi akaacha laana ya karne (kama serikali inalaanika sijui!?) na kuondoka hapo Hazina Makao Makuu hadi leo yuko hai Kijijini kama EL kule Peninsular; na akasusa kabisa kurudi Hazina.

Aina hii ya watumishi ndiyo wamejaa serikalini na ndiyo watafanya models kama za akina Makonda zisiishe nchi hii, zitakuja na kutoweka na kurudi tena na kutoweka tena na kurudi...
Kama hakuchukua yeye kwanini asidai haki yake .hata bank Hela huwa inaibwa Ila uchumguzi inafanyikia mhusika anarudishiwa
 
Hao Bank wanamkopeshaje mtu anayekalibia kustaafu? Lets say amebakiza miaka mi5 je kwa calculations zao kwa huo muda wa miaka 5 hiyo hela ingerudi? Ukizingatia AJIRA yake ndio dhamana ya Mkopo?

Kuna kitu sijakielewa.. je huy mtumishi alikopa kias gani..? Muda aliokopa ni upi? Na kama alikopa je terms za kurudisha mkopo upoje..? Haiwezekan mkopo wa miaka 7 wewe uchukue hela yako ndani ya miaka miwili...


Haya turud ktk kanuni na taratibu za kibenk.. je ni sahihi kunyofoa hela zote hizo bila kuruhusiwa na mwenye account..

Je kiwango cha kurudisha mkopo kwa mkupuo ndio kipo hivyo?

Kuna maswali mengi kwa uelewa wangu mdogo nashindwa kudadavua hii ishu.
Kukopa Kwa mstafu ni kawaida....hata aliyestafu anaruhisiwa kukopa against a pension
 
Back
Top Bottom