MWINY WETU
Member
- Dec 14, 2015
- 16
- 16
Huenda bwana Selemani Msindi amefanya makosa lakini ni lipi kosa lake kisheria? Nani wakumshtaki? Nani aliefanyiwa kosa?
Tukianza na kosa lake kisheria, kifungu namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kinaeleza kuwa Nikosa kuumiza hisia za imani ya kidini ya mtu mwingine kwa kuweka maneno,Ishara au picha mbele ya mtu huyo ambayo itaumuumiza hisia zake za kidini.
Hivyo kukashifu dini ya watu wengine ni makosa. Kifungu hicho hakisemi kukashifu Mungu.
Labda tunaweza kusema kuwa dini zinaamini Mungu, hivyo ukikashifu Mungu umekashifu dini.
Swali la pili litakuwa ni nani amekosewa? Hata kama tutasema kukashifu Mungu ni kukashifu dini na nikuumiza hisia za kidini za watu au mtu fulani.
Swali litakuwa ni dini ipi? Kuna dini zaidi ya 360 Duniani na kwenye baadhi ya dini kama wahindu na dini za kimila kuna Mungu zaidi ya mmoja. Swali linakuja kuwa ni Mungu yupi wa dini ipi alietukanwa na Selemani?
Kumbuka kuwa Kuna watu husema kuwa wao Mungu wao ni hela, hawa wana Mungu ila hawana dini.
Kufikia hapo tunagundua kuwa Selemani hana kosa lolote kisheria.
Pia soma> Ujumbe wa Afande Sele akimlilia Magufuli
Tukianza na kosa lake kisheria, kifungu namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kinaeleza kuwa Nikosa kuumiza hisia za imani ya kidini ya mtu mwingine kwa kuweka maneno,Ishara au picha mbele ya mtu huyo ambayo itaumuumiza hisia zake za kidini.
Hivyo kukashifu dini ya watu wengine ni makosa. Kifungu hicho hakisemi kukashifu Mungu.
Labda tunaweza kusema kuwa dini zinaamini Mungu, hivyo ukikashifu Mungu umekashifu dini.
Swali la pili litakuwa ni nani amekosewa? Hata kama tutasema kukashifu Mungu ni kukashifu dini na nikuumiza hisia za kidini za watu au mtu fulani.
Swali litakuwa ni dini ipi? Kuna dini zaidi ya 360 Duniani na kwenye baadhi ya dini kama wahindu na dini za kimila kuna Mungu zaidi ya mmoja. Swali linakuja kuwa ni Mungu yupi wa dini ipi alietukanwa na Selemani?
Kumbuka kuwa Kuna watu husema kuwa wao Mungu wao ni hela, hawa wana Mungu ila hawana dini.
Kufikia hapo tunagundua kuwa Selemani hana kosa lolote kisheria.
Pia soma> Ujumbe wa Afande Sele akimlilia Magufuli