Adui mkubwa wa Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe!

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,231
113,594
Naomba nizungumzie kiujumla, licha ya kwamba kati yetu binafsi, wapo ambao wako tofauti na walio wengi.

Watanzania wengi ni wajinga [wasiozijua haki zao] na ni waoga sana.

Mchanganyiko wa hizo sifa mbili ni kikwazo kikubwa sana katika maendeleo ya jamii.

Huwezi kupata maendeleo yoyote yale ya maana endapo idadi kubwa ya watu kwenye hiyo jamii wana hizo sifa za ujinga na uoga.

Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu, pale mtu asiye na mamlaka ya kukupora haki zako anapokupora, na wewe humpingi huyo mporaji kwa nguvu na uwezo wako wote, ni kitu gani kingine utakachoweza kukipigania kwa hali na mali?

Watanzania tumeshuhudia kuporwa baadhi ya haki zetu kwa miaka ya hivi karibuni kuanzia takriban 2016 mpaka hivi sasa. Na tumekuwa wapole na wanyonge mno.

Alianza Rais Magufuli kukiuka katiba na kuvikataza vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kikubwa kikiwa ni mikutano ya kisiasa.

Magufuli kaondoka, kaja Rais Samia naye akaendeleza huo uvunjaji wa katiba.

Wote hawa wawili wamevunja katiba waziwazi kabisa. Na sisi wananchi wenye nchi hakuna lolote la maana tulilolifanya kuwapinga hao wawili!

Tunaburuzwa buruzwa tu. Juzi hapa Samia eti katoa ruhusa ya vyama vya siasa kuanza kufanya mikutano ya kisiasa!

Hiyo ruhusa kaitoa kwa msingi gani wa mamlaka aliyonayo kisheria na kikatiba?

Sisi ni banana republic. Hatuongozwi na sheria wala katiba. Tunaongozwa na hisia, hisani, na matakwa ya mtu ambaye kimsingi ni mtumishi wetu, lakini kiuhalisia ni kama vile sisi ndo tunamtumikia yeye na si vinginevyo.

Kuna wakati kule Marekani, kipindi ambacho Donald Trump alikuwa Rais, kulikuwa na mjadala kuwa endapo angetoa agizo kwa jeshi la nchi hiyo, agizo lililo haramu kisheria na kikatiba, viongozi wa jeshi walikuwa wako tayari kabisa kulikaidi hilo agizo. Hawakuwa tayari kutekeleza agizo lolote linaloenda kinyume na sheria na katiba yao.

Hao ni watu wanaojitambua. Ni watu wasio waoga. Ni werevu na ni majasiri pia.

Hapa kwetu jambo kama hilo bado sijaona kama linawezekana.

Magufuli na Samia walipaswa kupingwa vikali sana.

Maagizo yao haramu ya kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani yalipaswa kukaidiwa na watekelezaji wa sheria.

Mtu kama kweli unajitambua, si mjinga wala muoga, kwa nini utekeleze amri ambayo si halali?

Kwani ukikataa kutekeleza amri ambayo si halali, nini kitakutokea?

Ije katiba mpya au isije, hii tuliyonayo sasa hivi inayotupatia haki tulizonazo sasa hivi, inakiukwa waziwazi kabisa na hatufanyi chochote kulinda hizo haki zetu, hiyo mpya tunayoitaka tutailinda kweli?

Kwa sasa nimeshahitimisha kuwa tatizo letu kubwa wala siyo katiba mpya. Tatizo ni sisi wenyewe. Bado tupo wajinga sana, wapole sana, na waoga sana.

Kwa hizi sifa, hata ije katiba mpya, hakutokuwa na tofauti yoyote ile. Tutaendelea kuburuzwa tu hadi pale tutapobadilika.

Na kwa kizazi hiki kilichopo, sitegemei tubadilike.

Adui wetu mkubwa ni sisi wenyewe!

Rais Samia hastahili pongezi yoyote ile kwa ‘kuruhusu’ vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa.

Hakuwa na haki ya kukataza hiyo mikutano. Hivyo hana haki ya kuruhusu mikutano hiyo.

Hastahili kabisa pongezi.

Anachopaswa kufanya ni kuomba radhi. Aombe radhi kwa kukiuka katiba.

Akiomba radhi kwa hilo, mimi nitakuwa wa kwanza kumpongeza kwa kuona kosa lake na kuamua kujirudi.

Nje ya hapo, siwezi kumpongeza mporaji aliyeamua kunirudishia kilicho changu.
 
Naomba nikusahihishe Watanzania sio waoga. Ila waTanzania ni WAOGA. Andika herufi kubwa na ubold ni WAOGA. Hata mimi ni muoga 😂😂😂😂. Hasahasa vyombo vya dola (polisi, jeshi, usalama) wanatumika kuiba kura pia kunyanyasa raia na kufanya vitendo ambavyo ni kinyume na sheria. Kama tungekuwa na watu imara hata polisi wangekataa kuzuia mikutano ya hadhara. Au wasingekubali kutumika kuiba kura na kuchakachua uchaguzi. Kama wanajeshi walivyokataa maagizo ya trump. Je ushawahi sikia cia, fbi,navy wanaiba kura usa?



Siku ambayo vyombo vya dola vikikataa kupelekeshwa na wanasiasa au kupindua ccm ndio nitaamini hao ni wanaume 😂😂😂. Zaidi ya hapo waTanzania wote sisi ni waoga hata mimi ni MUOGA sana 😂.
 
Naomba nikusahihishe Watanzania sio waoga. Ila waTanzania ni WAOGA. Andika herufi kubwa na ubold ni WAOGA. Hata mimi ni muoga 😂😂😂😂. Hasahasa vyombo vya dola (polisi, jeshi, usalama) wanatumika kuiba kura pia kunyanyasa raia na kufanya vitendo ambavyo ni kinyume na sheria. Kama tungekuwa na watu imara hata polisi wangekataa kuzuia mikutano ya hadhara. Au wasingekubali kutumika kuiba kura na kuchakachua uchaguzi.



Siku ambayo vyombo vya dola vikikataa kupelekeshwa na wanasiasa au kupindua ccm ndio nitaamini hao ni wanaume 😂😂😂. Zaidi ya hapo waTanzania wote sisi ni waoga hata mimi ni MUOGA sana 😂.
Amri au maelekezo haramu yanapaswa kukaidiwa!
 
Amri au maelekezo haramu yanapaswa kukaidiwa!
Ndio inavyotakiwa. Yaani polisi, jeshi na usalama wanapaswa kukataa maagizo yoyote ambayo ni kinyume na sheria. Yena wakiona wanasiasa wanazingua wanawapindua tu 😂😂😂😂. Yaaani libaba lizima na bunduki na silaha zote na kozi zote eti unaagizwa kufanya vitendo ambavyo ni kinyume na sheria na wewe unakubali 😂😂😂. Unakuta libaba lizima linaagizwa kuchakachua uchaguzi na lenyewe linakubali.
 
Na ndo maana Kenyatta alishawahi kumwambi Nyerere "anaongoza wafu"

Tatizo watanzania hatuna sauti ya umma na umoja kuanzia ngazi za chini kabisa mfano nyumbani ,mitaanii. mtu anaweza dhulumiwa haki yake na akashindwa kujitetea akasubiri atokee mtu mwingine aje amtetee, na huyo mtu anaweza asitokee kumsaidia.
Mfano,
Imagine, dala dala inaweza kuwafaulisha kwa gari lingine bila sababu ya msingi utakuta watu wanalalamika chini kwa chini wanashindwa kuunganisha sauti zao kugomea kwa kitendo walichofanyiwa, na anapotokea mtu mmoja kuonyesha msimamo unakuta wengine wanaogopa wanashindwa kumuunga mkono.

Mfano mwengine,
Siku hizi barabara za mjini kuna Traffic wengi sana, kazi yao kubwa ni kukusanya ushuru barabarani kila gari linalopita wanachukua buku mbili mpaka buku tano tena unakuta wametanda kila mahali mpaka unafika mwisho wa gari ushakutana hata na watano ila cha kushangaza madereva wanabaki kulalamika tu ila wanashindwa kuweka msimamo kwenye haki zao, na kuhoji kuhusu huu utaratibu unabaki kuona ujinga tulionao wengi wetu.

ukiangalia hii mifano ndo unapata aina ya watu waliopo Tanzania na ndo unapokuja kujua nini Alimaanisha kenyatta kutuita sisi Wafu.
 
Mimi nilidhani mleta mada unakuja na hoja inayogusa jamii ya wananchi kwa ujumla wake kumbe ni maslahi ya kisiasa na vyama vya siasa.

Kwa hio kama hao viongozi wasingezuia hio mikutano ya kisiasa wasingekua na ubaya wowote.

Hivo mikutano ya kisiasa ilikuwepo kipindi kile cha uongozi wa Kikwete mbona faida yake haionekani katika jamii.

Kwamba kuruhusiwa hio mikutano ya kisiasa ndio mwanzo wa taifa na wananchi kwa ujumla wataondokana na umaskini na kadhia zote zilizo kati yetu?
 
Na ndo maana Kenyatta alishawahi kumwambi Nyerere "anaongoza wafu"

Tatizo watanzania hatuna sauti ya umma na umoja kuanzia ngazi za chini kabisa mfano nyumbani ,mitaanii. mtu anaweza dhulumiwa haki yake na akashindwa kujitetea akasubiri atokee mtu mwingine aje amtetee, na huyo mtu anaweza asitokee kumsaidia.
Mfano,
Imagine, dala dala inaweza kuwafaulisha kwa gari lingine bila sababu ya msingi utakuta watu wanalalamika chini kwa chini wanashindwa kuunganisha sauti zao kugomea kwa kitendo walichofanyiwa, na anapotokea mtu mmoja kuonyesha msimamo unakuta wengine wanaogopa wanashindwa kumuunga mkono.

Mfano mwengine,
Siku hizi barabara za mjini kuna Traffic wengi sana, kazi yao kubwa ni kukusanya ushuru barabarani kila gari linalopita wanachukua buku mbili mpaka buku tano tena unakuta wametanda kila mahali mpaka unafika mwisho wa gari ushakutana hata na watano ila cha kushangaza madereva wanabaki kulalamika tu ila wanashindwa kuweka msimamo kwenye haki zao, na kuhoji kuhusu huu utaratibu unabaki kuona ujinga tulionao wengi wetu.

ukiangalia hii mifano ndo unapata aina ya watu waliopo Tanzania na ndo unapokuja kujua nini Alimaanisha kenyatta kutuita sisi Wafu.
Kama katiba iliyopo inakiukwa na hatufanyi kitu, hiyo mpya ikikiukwa tutafanya nini?

Sisi ni watu wa ajabu sana.
 
Mimi nilidhani mleta mada unakuja na hoja inayogusa jamii ya wananchi kwa ujumla wake kumbe ni maslahi ya kisiasa na vyama vya siasa.

Kwa hio kama hao viongozi wasingezuia hio mikutano ya kisiasa wasingekua na ubaya wowote.

Hivo mikutano ya kisiasa ilikuwepo kipindi kile cha uongozi wa Kikwete mbona faida yake haionekani katika jamii.

Kwamba kuruhusiwa hio mikutano ya kisiasa ndio mwanzo wa taifa na wananchi kwa ujumla wataondokana na umaskini na kadhia zote zilizo kati yetu?
Nazungumzia haki zilizopo kikatiba.

Au hujaelewa nilichokiandika?
 
Back
Top Bottom