Adhabu ya Viboko Shuleni na Nyumbani,wewe una maoni gani?

Bakora ziendelee kama kawaida,tusizidi kudesa kila kitu kutoka katika nchi nyingine.
 
Kwa taarifa yako hata hiyo adhabu ya viboko Tanzania walileta wazungu, ndio waliotufundisha kuchapa watoto, yaani jinsi wanavyochapwa leo shuleni, matakoni au mikononi na ni viboko vingapi vinaruhusiwa hayo yote walileta wazungu, na walileta kutoka kwao kwa maana wakati huo hata wao pia watoto wao walikuwa wanachapwa shuleni, lakini sasa hivi hawachapi watoto wao tena kwa maana wameshapima na kujiuliza maswali mengi sana pamoja na hayo unayojiuliza wewe na wakagundua kuwa kumchapa mtoto hakumsaidii chochote katika maendeleo yake ya kitaaluma na kimaisha wakaamua kufuta, sasa kwa nini na sisi tusifute, kama waliotufundisha kuchapa hawachapi tena?


JUSTIFICATION: Tulichapa kwa sababu walitufundisha (tuliwaiga) na tunataka kuacha kwa sababu wameacha.
 
Kama ni lazima mtoto achapwe, basi mzazi / mlezi rasmi aje shuleni na yeye ndiye atakayemchapa. Waalimu wapigwe marufuku kuwapiga wanafunzi, iwe viboko au kuwaumiza kwa njia yoyote ile. Nyumbani hakutuhusu! Kimsingi mwalimu kumpiga mwanafunzi ni shambulizi (assault).
 
Bakora ziendelee kama kawaida,tusizidi kudesa kila kitu kutoka katika nchi nyingine.

Naunga mkono hoja. Tofauti ya nchi zilizoendelea na akina sie, ni kwamba wenzetu hulea watoto wao magetini mwa nyumba zao. Sisi? Watoto hulelewa mitaani. Mambo wanayojifunza huko kamwe hawawezi kuyaacha kwa kutumia maneno matupu tu. Bakora serves as a reminder.
 
Mimi nimekula viboko sana na hata watoto wangu watakapo enda nje ya mstari lazima waipate sharubati.
 
adhabu ya viboko ni nzuri kama ikitumiwa vizuri na bila jazba. ingawa nlivyokuwa mdogo nlivuwa namind sana viboko ila model ya mzee wangu nliiapreciate. unapewa kichapo halafu vikipoa unaitwa kuelezwa why umechapwa. wazazi wengine wanawapiga watoto halafu mtoto haelewi kosa lake hadi anakuwa nunda. pili kuna umri viboko vinaisha mnakuwa mnaongea, mzee alisitisha viboko darasa la sita sio hadi form four unachezea mboko
 
wapigwe tu na mtapigwa tu ma dent kama hamuelewi nasema wachapeni viboko ..viboko sita kwa vitatu uthibitisho wa mkuu wa shule ni muhimu wavulana kwa makalio na wasichana kwa mkono
 
Wakuu, visu vinauzwa holela-sokoni, dukani hata barabarani tunaona vinauzwa wala havina shida yoyote, tatizo linakuja kisu icho kinapoingia mkononi mwa mtu asiye sahihi ndipo kinapo geuka kuwa hatari. ni kwa staili hii hii viboko vya awali vilikua na msaada kwa kuwa walimu na wazazi wengi walikua wazazi au walimu sahihi , kwa sasa walimu sahihi wamepungua sana yani wengi ni waganga njaa baada ya kukuosa selection zingine za maisha ndo wanaingia ualimu tena unaskia wanasoma miezi 6 matokeo yake sekondari kutofautisha mwanafunzi na mwalimu sio rahisi wote wanakua na akili zile zile badala yake fimbo ndio inatumika kutofautisha mamlaka ya mwalimu na mwanafunzi kwa hili nadhani walimu wa sasa hawawezi kufunza kwa kiboko wanatuongezea shida watoto wanakua sugu mioyoni sababu ya kupigwa pigwa na kutukanwa hovyo, upande mwingine ni sisi wazazi wa sasa wengine tunazaa fasheni tu yaani hatuja komaa kuhimili malezi ndo maana hata matumizi ya fimbo hayasaidii kwa kua fimbo hiyo haichapwi katika mazingira sahihi na hivyo mtoto anabakia kusikia maumivu kwenye nyama na sio moyo wake kuona sababu ya kubadilika. Mi nadhani kwa upande wa shule fimbo ichapwe na mwalimu mkuu tu tena kwa utaratibu utakao msaidia mtoto kubadilika yani sio kuchapa kama mazoea. ukitaka kujua utaratibu wa fimbo umepoteza mashiko ukikuta vitoto vidogo vinacheza kishule shule yule anae kuwa mwalimu lazima awe na fimbo, simply watoto wetu wanaona mwalimu ni fimbo tu so haiwasaidiii kubadilika
 
Back
Top Bottom