Adhabu ya Kunyonga Hadi Kufa imepitwa na wakati?

Mkuu kwanza kabisa kifo ni kwamba kila mtu atakufa siku moja hakuna atakakimbia hii destination..; Pili kazi ngumu na mateso yanaweza yakawa makali kwa mtu hadi akatamani afe...; kuliko kuendelea kuishi (au hii haiwezekani) kwahio sisemi hawa watu wapewe kazi tu, bali kazi ngumu na faida ya hizo kazi kama ipo irejeshwe kwenye jamii husika.

Sisemi kabisa an eye for an eye..., sababu ukirejea maneno ya Gandhi anakwambia will make the all World go Blind..

Kuhusu dini kukubaliana na kwamba ukiua na wewe wakunyonge sidhani kama ni kweli labda sijarejea maandiko vizuri, nadhani maandiko mengi yanasema kusamehe au labda nikumbushe ni wapi maandiko yanasema mtu akiua na yeye anyongwe..

Uhakika ninao kwamba vitabu vya dini zote vinasema hivyo japo siwezi kunukuu vifungu. Naamini wapo miongoni mwetu wenye ufahamu mkubwa wa mambo ya dini watatujulisha. Ni kweli kifo hakiepukiki kila mmoja kimamsubiri. Hoja ni kuna hata mmoja anaependa kufa? Ukweli wa kaiawaida utasema hapana. Adhabu ngumu za kazi zinatesa ni sawa laikini haziwezi kuogopwa kama kifo.

Jamii kufaidika kiuchumi ni sawa lakini lengo la adhabu sio kunufaika kiuchumi bali kuzuia makosa mengi kama hayo kujirudia na kuathiri jamii isiyokuwa na hatia. Hata hivyo, mwisho wa siku kama adhabu hiyo bado inafaa katika mazingira yesu ni watanzania walio wengi ndio wataamua.

Kichwa cha maneno hapa ni adhabu ya kifo kupitwa na wakati. Hiyo inaashiria kuna wakatii ilikuwa inafaa. Ni mabadiliko gani ya msingi katika maisha ya mwanaadamu yanayomfanya mwanaadamu wa leo kutokuwa mhalifu samna kama wa zamani ili tuseme kwamba kwa leo imepitwa na wakati. Mimi naona kadili muda unavyozidi kwenda binaadamu tunakuwa wakatili sana na kuongeza tekinologia ya kuuwana. Ningekuwa mimi ningesema adhabu ya kifo ni muafaka zaidi kwa sasa kuliko enzi za manabii au enzi za ujima
 
Kuna mjumbe mmoja ametoa hoja nzito na ningeomba pia niichangie. Anazungumzia kuhusu matukio ambayo mtu anahukumiwa adhabu ya kifo na mbele ya safari anaonekana kuwa hakuwa na hatiya. Hilo ni moja ya maswali magumu katika uhalali wa adhabu ya kifo. Mimi msimamo wangu juu ya hilo ni kwamba adhabu ya kifo zotolewe tu katika kesi ambazo mtuhumiwa amehukumiwa na kutiwa hatiyani kwa ushahidi wa moja kwa moja na sio ushahidi wa kimazingira.

Je, unaweza kunipa mfano wa ushahidi wa moja kwa moja (ushahidi usiyo wa kimazingira) nielewe pointi yako zaidi?

Pia mahakama ziwe na uhuru kulingana na mazingira yanayoizunguka kesi kutoa hukumu ya kifungo cha maisha badala ya adhabu ya kifo. Sheria iweke wazi mambo ambayo jaji anapaswa kuyazingatia anapotoa adhabu ya kifungo cha maisha badala ya adhabu ya kifo na hiyo iwe katika execeptional curcumstances.

Lakini kama adhabu ya kifo ipo, kuna sababu halali ambayo ingehalalisha kumhukumu adhabu ya kifo muuaji moja na kutokumpa adhabu sawa atendao kosa sawa na muuaji niliotaja awali (kumhukumu kifungo cha maisha badala yake)? I mean, shouldn't it be either all or nothing? Vinginevyo kusingekuwepo usawa.
 
Uhakika ninao kwamba vitabu vya dini zote vinasema hivyo japo siwezi kunukuu vifungu. Naamini wapo miongoni mwetu wenye ufahamu mkubwa wa mambo ya dini watatujulisha. Ni kweli kifo hakiepukiki kila mmoja kimamsubiri. Hoja ni kuna hata mmoja anaependa kufa? Ukweli wa kaiawaida utasema hapana. Adhabu ngumu za kazi zinatesa ni sawa laikini haziwezi kuogopwa kama kifo. Jamii kufaidika kiuchumi ni sawa lakini lengo la adhabu sio kunufaika kiuchumi bali kuzuia makosa mengi kama hayo kujirudia na kuathiri jamii isiyokuwa na hatia. Hata hivyo, mwisho wa siku kama adhabu hiyo bado inafaa katika mazingira yesu ni watanzania walio wengi ndio wataamua.

Kichwa cha maneno hapa ni adhabu ya kifo kupitwa na wakati. Hiyo inaashiria kuna wakatii ilikuwa inafaa. Ni mabadiliko gani ya msingi katika maisha ya mwanaadamu yanayomfanya mwanaadamu wa leo kutokuwa mhalifu samna kama wa zamani ili tuseme kwamba kwa leo imepitwa na wakati. Mimi naona kadili muda unavyozidi kwenda binaadamu tunakuwa wakatili sana na kuongeza tekinologia ya kuuwana. Ningekuwa mimi ningesema adhabu ya kifo ni muafaka zaidi kwa sasa kuliko enzi za manabii au enzi za ujima

Kuhusu adhabu ya kifo kupunguza uhalifu imeonekana statistically sehemu ambazo kuna hii adhabu na sehemu ambazo zipo ni kwamba haipunguzi uhalifu...;

Pili watu kuogopa kifo is debatable sababu kuna watu huwa wanajiua (ambao wanaitwa cowards.., au waoga na wanashindwa ku-face matatizo yao..) hivyo basi utaona kwamba kumbe maisha yanaweza yakakupiga hadi kifo ikawa option rahisi..

Kuhusu adhabu ya kifo kupitwa na wakati sidhani kama ilikuwepo wakati ambapo adhabu hii ilikuwa muafaka na je inafaida gani kwa jamii kama haipunguzi uhalifu..., na je ndugu wanapunguziwa lile simanzi kwa mtuhumiwa kuuliwa..., na hapo kwenye post ya nyuma nilitoa mfano wa mtu aliyeua watoto wawili huko UK na akafungwa maisha na huyu jamaa ameshajaribu kujiua mara 2 (Je bado huyu mtu angenyongwa familia ingeona safi haki imetendeka au wangeona kwamba sasa serikali imesaidia kufanya kile ambacho jamaa alitaka mwanzo)
 
Adhabu hii ya kifo kwa aliye uwa ni bora iendelee!kwani ni hukumu iliyo ya haki kwa aliye uwa kwa dhulma.ila kwa alieua bila ya kukusudia au kosa jingine lolote lisilo husiana na mauji ya kusudiwa,hilo linaweza kuangaliwa kwa makini!ila aliyeua kwa makusudi nae pia auawe!japo hawezi kuwaondolea wafiwa majanzi,lakini angalau!haki itakua imetendeka
 
Je, unaweza kunipa mfano wa ushahidi wa moja kwa moja (ushahidi usiyo wa kimazingira) nielewe pointi yako zaidi?



Lakini kama adhabu ya kifo ipo, kuna sababu halali ambayo ingehalalisha kumhukumu adhabu ya kifo muuaji moja na kutokumpa adhabu sawa atendayo kosa sawa na muuaji niliotaja awali (kumhukumu kifungo cha maisha badala yake)? I mean, shouldn't it be either all or nothing? Vinginevyo kusingekuwepo usawa.

Nakubali sikujieleza vizuri na huenda sikueleweka. Nikianzia na ushahidi wa moja kwa moja ni nini na wamazingira ninini? Chukulia "M" n anatuhumiwa kumuuwa "B" kwa kumpiga nondo kubwa kichwani. A na D wanakuja mahakamani na kusema walimuuona "M" akimpiga "B" mpaka akakata roho na ushahidi wa unathibitika bila kuacha tone la shaka. Hapo tunasema kuna ushahidi wa moja kwa moja. Lakini ikiwa kama "A' atasema alimkuta "B" amekufa akiwa na jeraha kubwa kichwani. A akasema mda mfupi kabla ya tukio alimkuta "M" na nondo ikiwa imelowa damu akikimbia kutoka eneo la tukio na "X" pathologist ameyeaupasua mwili wa "B" na kugundua kwamba sababu ya kifo ni maumivu na jeraha kubwa yaliyosababishwa na kitu kama nondo, tunaweza kusema kuna ushahidi wa kimazingira kuthibitisha kwamba "M" ndiye aliyemuuwa "B".

Hoja yangu ni kwamba uzito wa ushahidi wa moja kwa moja na wa kimazingira sio sawa. Kuna uwezekano "M" alimkuta mtu anampiga "B" kwa rungu akagombana naye na hatimaye kukimbia na rungu. Kuna uwezekano "M" alikuwa na shida ya nondo akakutwa imetupwa njiani akaichukuwa na kukimbia nayo kwenda kumkabili gendre jirani na shamba lake. Ndio maana katika matukio machache ambapo mtu anapatikana na hatia ya mauji alafu badae anaonekana hakuwa na hatia, ushahidi uliyotumika kumhukumu ulikuwa wa kimazingira.
 
Kuhusu adhabu ya kifo kupunguza uhalifu imeonekana statistically sehemu ambazo kuna hii adhabu na sehemu ambazo zipo ni kwamba haipunguzi uhalifu...;

Pili watu kuogopa kifo is debatable sababu kuna watu huwa wanajiua (ambao wanaitwa cowards.., au waoga na wanashindwa ku-face matatizo yao..) hivyo basi utaona kwamba kumbe maisha yanaweza yakakupiga hadi kifo ikawa option rahisi..

Kuhusu adhabu ya kifo kupitwa na wakati sidhani kama ilikuwepo wakati ambapo adhabu hii ilikuwa muafaka na je inafaida gani kwa jamii kama haipunguzi uhalifu..., na je ndugu wanapunguziwa lile simanzi kwa mtuhumiwa kuuliwa..., na hapo kwenye post ya nyuma nilitoa mfano wa mtu aliyeua watoto wawili huko UK na akafungwa maisha na huyu jamaa ameshajaribu kujiua mara 2 (Je bado huyu mtu angenyongwa familia ingeona safi haki imetendeka au wangeona kwamba sasa serikali imesaidia kufanya kile ambacho jamaa alitaka mwanzo)

Kuhusu takwimu za adhabu ya kifo kupunguza au kutokupunguza uhalifu kwa uzoefu wangu najua matatizo makubwa ya kuaminika kwa takwimu hizo. Ukitizama takwimu zinazotolewa na wapinzani wa adhabu ya kifo watakuambia haipunguzi uharifu. Ukitizama takwimu za wanaunga mkono adhabu ya kifo watakwambia inapunguza. Tatizo hapa ni methodology ya utafiti na design pamoja na sampo. Ndio maana katika hoja zangu sijaangalia sana mambo ya takwimu bali nimeangalia mantiki ya kawaida. Sijui kama kuna takwimu zingine zinazoonesha adhabu ya kifungo inapunguza uhalifu? Mwisho wa siku wanazuoni wapinzani wa adhabu watakupa takwimu kwamba adhabu hazipunguzi uhalifu alafu hatimaye tutasema wakosaji wasiadhibiwe bali wapelekwe shule kufindishwa ubaya wa makosa au wapelekwe kanisani na misikitini wakahubiriwe ubaya wa ukosaji.

Mfano wa hao jamaa wa UK ni katika very execeptional cases. Na ukifanya uchunguzi wa kina utaona kwamba wana matatizo ya akili au saikologia yaliyotokana na usongo wa mawazo. Ni sawa na watu wengine wanaojinyonga huku mitaani. Lakini kisayansi na kimantiki mtu mwenye akili ya kawaida hupendelea kuishi kuliko kufa. Ndio maana mahosbitali yanajaa wagonjwa. Kwa nini? Wanapigana na kifo. Hawapendi kufa bali wanapenda kuishi
 
Mfano wa hao jamaa wa UK ni katika very execeptional cases. Na ukifanya uchunguzi wa kina utaona kwamba wana matatizo ya akili au saikologia yaliyotokana na usongo wa mawazo. Ni sawa na watu wengine wanaojinyonga huku mitaani. Lakini kisayansi na kimantiki mtu mwenye akili ya kawaida hupendelea kuishi kuliko kufa. Ndio maana mahosbitali yanajaa wagonjwa. Kwa nini? Wanapigana na kifo. Hawapendi kufa bali wanapenda kuishi

Kuhusu takwimu wamechukua mfano nchi zenye same culture ambazo zina death penalty na ambazo hazina na kuona kwamba zile zenye death penalty hazipunguza crime rate hence kuonyesha hii notion ya hii adhabu kupunguza crime sio ya kweli..

Kuhusu wale wanaojiua wana matatizo ya akili na kisaikolojia I can argue the same kwamba hata watu wanaoua wenzao wanamatatizo ya akili na ya kisaikolojia hence wakitoa roho ya mwenzao sidhani kama watawaza sana ya kwao kutolewa.
 
Takwimu mara nyingi sana hufuata presupositions za mtafiti. Mimi leo nikitaka kufanya risachi nani atashinda uraisi mwaka 2015 na nikakusudia ni Mbowe na Makamba naweza kuprove hyposis yangu. Watafiti wanaotoa takwimu sahihi au karibu na sahihi ni walio huru. Watu wengi wanaofanya tafiti za adhabu ya kifo ni wale wapinzani wa adhabu ya kifo. Lengo lao ni kutumia tafiti kuharamisha adhabu ya kifo. Unategemea hata kama wakifanya tafiti Musoma watakuambia watu wengi wanapenda adhabu ya kifo au adhabu ya kifo inapunguza uhalifu.

Ndio zipo kesi za watu wanaouwa kutokana na matatizo ya akili na kisaikologia na wapo wengi wanaouwa makusudi kwa sababu ya kusaka mali au kuondoa adui zao. Mara nyingi watu wa aina ya kwanza ni raisi kuwaona katika upimaji wa ushahidi kwamba hawakuwa na dhamira timamu ya kusababisha kifo na hivyo kuuwa kwao sio mada. Lakini jambazi linalouwa watu kusaka pesa huwezi kusema linafanya hivyo kwa matatizo ya kiakili au kisaikologia. Sheria za nchi zote hazimtii mtu hatiyani aliyeuwa bila kukusudia au kwa sababu ya kupungukiwa uwezo wa kiakili wa kubainisha haramu na halali
 
Takwimu mara nyingi sana hufuata presupositions za mtafiti. Mimi leo nikitaka kufanya risachi nani atashinda uraisi mwaka 2015 na nikakusudia ni Mbowe na Makamba naweza kuprove hyposis yangu. Watafiti wanaotoa takwimu sahihi au karibu na sahihi ni walio huru. Watu wengi wanaofanya tafiti za adhabu ya kifo ni wale wapinzani wa adhabu ya kifo. Lengo lao ni kutumia tafiti kuharamisha adhabu ya kifo. Unategemea hata kama wakifanya tafiti Musoma watakuambia watu wengi wanapenda adhabu ya kifo au adhabu ya kifo inapunguza uhalifu.

Ndio zipo kesi za watu wanaouwa kutokana na matatizo ya akili na kisaikologia na wapo wengi wanaouwa makusudi kwa sababu ya kusaka mali au kuondoa adui zao. Mara nyingi watu wa aina ya kwanza ni raisi kuwaona katika upimaji wa ushahidi kwamba hawakuwa na dhamira timamu ya kusababisha kifo na hivyo kuuwa kwao sio mada. Lakini jambazi linalouwa watu kusaka pesa huwezi kusema linafanya hivyo kwa matatizo ya kiakili au kisaikologia. Sheria za nchi zote hazimtii mtu hatiyani aliyeuwa bila kukusudia au kwa sababu ya kupungukiwa uwezo wa kiakili wa kubainisha haramu na halali

Naomba utafiti wowote uliofanywa ukaonyesha kwamba sheria ya kifo inapunguza crime...

Pia mimi nimekupa mfano kwamba mbona watu huwa wanajiua wenyewe kama kifo kinatisha sana (wewe ukasema kwamba hao watu hawana akili au wana matatizo ya kisaikolojia..) Hivyo basi nikakuuliza wanatoa roho za wenzao kwa sababu yoyote ile iwe mali au kitu chochote wewe unadhani hao wana akili nzuri.... na hapa siongelei insanity ambayo kama mtu akiwa nayo hii hawezi kuhukumiwa kifo au makosa yoyote ambayo yanahitaji kuwapo kwa guilty mind (mens rhea)
 
Takwimu ndugu yangu japo siziamini sana ninazo nyingi tu zinazounga mkono pande zote mbili. Nipatie muda wa kufanya reference naweza nikakupatia mwisho wa wiki.

Ningekuomba utofautishe kati ya ukatili na wenda wazimu. Mwisho wake tunaweza kusema hata Raisi anayeamrisha jeshi lake liuwe watu wanaoipinga Serikali bila kuzingatia sheria ni mwendawazimu. Kuna tofauti pia kati ya mwenda wazimu na mwenye "akili mbaya". Uenda wazimu ni suala la kisayansi bali kuwa na akili mbaya au nzuri ni suala la kisoshologia.
 
Takwimu ndugu yangu japo siziamini sana ninazo nyingi tu zinazounga mkono pande zote mbili. Nipatie muda wa kufanya reference naweza nikakupatia mwisho wa wiki.

Ningekuomba utofautishe kati ya ukatili na wenda wazimu. Mwisho wake tunaweza kusema hata Raisi anayeamrisha jeshi lake liuwe watu wanaoipinga Serikali bila kuzingatia sheria ni mwendawazimu. Kuna tofauti pia kati ya mwenda wazimu na mwenye "akili mbaya". Uenda wazimu ni suala la kisayansi bali kuwa na akili mbaya au nzuri ni suala la kisoshologia.

Kwahiyo watu wanaojinyonga au kutoa maisha yao ni aina ipi..?
Na wale ambao wanapata shida duniani na kutamani kufa ni kundi lipi..?
Na walio wanaotengwa na kujiona hawafai na kutamani kufa ni kundi lipi..?

Ukweli unabaki kuwa wazi kwamba unaweza ukabaki na maisha yako na ukapata tabu / mateso kuliko kifo (na wengine wanaweza wakasema kwamba kifo inakuwa ni shortcut na easy way out)
 
Watu wa kundi la pili hatimaye wanaweza kuangukia kundi la tatu japo kuna kesi chache za watu wenye akili sawa kabisa wanaocommit suiside kwa sababu mbalimbali za kimaisha kama vile magonjwa ya kutesa na kuogopa kuuwawa kikatili.

Mtu anayesubiri kunyongwa hadharani mpaka afe anaweza kunywa vidonge kwa kuogopa kifo cha kunyongwa na mateso yake. Sio kwa sababu anapenda kifo bali anaogopa mateso ya kifo. Anachagua kati ya kufa kwa vidonge au kunyongwa hadharani.
 
Nakubali sikujieleza vizuri na huenda sikueleweka. Nikianzia na ushahidi wa moja kwa moja ni nini na wamazingira ninini? Chukulia "M" n anatuhumiwa kumuuwa "B" kwa kumpiga nondo kubwa kichwani. A na D wanakuja mahakamani na kusema walimuuona "M" akimpiga "B" mpaka akakata roho na ushahidi wa unathibitika bila kuacha tone la shaka. Hapo tunasema kuna ushahidi wa moja kwa moja. Lakini ikiwa kama "A' atasema alimkuta "B" amekufa akiwa na jeraha kubwa kichwani. A akasema mda mfupi kabla ya tukio alimkuta "M" na nondo ikiwa imelowa damu akikimbia kutoka eneo la tukio na "X" pathologist ameyeaupasua mwili wa "B" na kugundua kwamba sababu ya kifo ni maumivu na jeraha kubwa yaliyosababishwa na kitu kama nondo, tunaweza kusema kuna ushahidi wa kimazingira kuthibitisha kwamba "M" ndiye aliyemuuwa "B".


Hoja yangu ni kwamba uzito wa ushahidi wa moja kwa moja na wa kimazingira sio sawa. Kuna uwezekano "M" alimkuta mtu anampiga "B" kwa rungu akagombana naye na hatimaye kukimbia na rungu. Kuna uwezekano "M" alikuwa na shida ya nondo akakutwa imetupwa njiani akaichukuwa na kukimbia nayo kwenda kumkabili gendre jirani na shamba lake. Ndio maana katika matukio machache ambapo mtu anapatikana na hatia ya mauji alafu badae anaonekana hakuwa na hatia, ushahidi uliyotumika kumhukumu ulikuwa wa kimazingira.

Kama nimekuelewa vizuri, ushahidi wa moja kwa moja ni ushuhuda wa mtu (A) anayedai alishuhudia tukio la muuaji (M) kumuua mwathirika (B).

Lakini, kama A akidanganya mahakamani, bado uwezekano wa M kuhukumiwa adhabu ya kifo ingawa hakutenda crime yoyote upo, sivyo? Au unadhani yawezekana kuwa na uhakika wa 100% kwamba M ndiye aliyemuua B ?
 
Wauwaji wa kweli hawana namna mbadala ya kuwaondoa katika jamii isipokuwa kuwaua,kifo sio adhabu,bali kufungwa gerezani ndiyo adhabu,mtu ambaye kwa sababu na ushahidi uliopo imethibitika kuwa ni hatari kwa jamii na kuwa ametenda kinyume na jamii kwa kuondoa uhai wa jamii isipokuwa kwa kulazimishwa na mazingira halali,hakuna hukumu zaidi ya kumwondoa kwenye jamii (KIFO) binafsi sioni kwa nini kifo kinaitwa adhabu,badala ya kuwa ni maamuzi ya kukuondoa kwenye jamii kwa uovu ulioutenda dhidiu ya jamii.

Kwangu naona ni muhimu kuwa na namna ya kutambua makosa ambayo yatakuwa ni makubwa kwa jamii kiasi cha mtenda kosa hili awe hatakiwi kuwepo kwenye hiyo jamii kwa kuuawa. Makosa na namna ya kutambua mkosaji kuwekea misingi mizuri kuepuka kuondoa kwenye jamii watu wema kwa makosa ya misingi ya kisheria, Hukumu ya kifo (SIO ADHABU YA KIFO) iendelee kuwepo, ili mazingira yakitokea ya mtu kutakiwa kuondolewa kwenye jamii yakijitokeza na AONDOLEWE KWA KUUAWA, kuwepo kwa hukumu ya KIFO kwenye vitabu vya sheria hakutufanyi Tanzania tuwe tunauua hovyo hovyo au hakuna sherehe ya kuua watu imefanyika kwa kuwa vitabu vyetu vya sheria vinahukumu KIFO. SIONI ADHABU MBADALA KWA WANAOUWA MAALBINO NA WATU WENGINE KWA MASLAHI YAO YA KIDUNIA.

Huu mjadala unatakiwa upewa kipaumbele na 'voting right'kubwa kwa watu ambao wameweza kuondokea na wapendwa wao kwa kuuawa,wao ndo wanajua machungu ya kuuliwa wategemezi na wapendwa wao,wanaharakati hawana lolote zaidi ya kuangalia dhima na mikakati yao ya kuombea fedha kwa wafadhili.
 
Kama nimekuelewa vizuri, ushahidi wa moja kwa moja ni ushuhuda wa mtu (A) anayedai alishuhudia tukio la muuaji (M) kumuua mwathirika (B).
Lakini, kama A akidanganya mahakamani, bado uwezekano wa M kuhukumiwa adhabu ya kifo ingawa hakutenda crime yoyote upo, sivyo? Au unadhani yawezekana kuwa na uhakika wa 100% kwamba M ndiye aliyemuua B ?

Suala la kudanganya au kutodanganya Mahakamani mara nyingi huwa linashughulikiwa katika upembuzi wa ushahidi. Ili mtu ahukumiwe kosa lolote la jinai ni lazima ushahidi uwe pasina kuacha shaka. Hiyo haina maana kuwa ni asilimia 100. Inaweza kuwa asilimia 100 kama mtu ametiwa hatiani kwa ungamo lake mwenyewe. Upo uwezekano mdogo kwa mtu kuhukumiwa kwa ushahidi wa uongo. Ndio maana asiyeridhika hupewa nafasi ya kukata rufaa.
 
Suala la kudanganya au kutodanganya Mahakamani mara nyingi huwa linashughulikiwa katika upembuzi wa ushahidi. Ili mtu ahukumiwe kosa lolote la jinai ni lazima ushahidi uwe pasina kuacha shaka. Hiyo haina maana kuwa ni asilimia 100. Inaweza kuwa asilimia 100 kama mtu ametiwa hatiani kwa ungamo lake mwenyewe. Upo uwezekano mdogo kwa mtu kuhukumiwa kwa ushahidi wa uongo. Ndio maana asiyeridhika hupewa nafasi ya kukata rufaa.

Ndiyo, lakini upembuzi wa ushahidi hauwezi kuhakikisha kwa asilimia 100% mtu fulani ndiye muuaji. Kinachoweza kufanya tu ni kutuambia kama uwezekano wa mtu yule kuwa muuaji ni mkubwa au la. Kutokuwepo wa shaka yo yote haiwezekani, hata kama mtu anakiri kwamba yeye ndiye mtenda kosa maana kuna uwezekano anadanganya kumlinda muuaji wa kweli.

Nakubali uwezekano wa mtu asiye na hatia kuhukumiwa ni mdogo, lakini upo. Nafikiri ni sababu ya kutosha kuipinga adhabu ya kifo, don't you think?
 
Unamaanisha kwamba mtu akajisingizia mwenyewe kwamba ameuwa ili kumuokoa mtu mwingine? Kama kuna kesi kama hizo, ambazo ni nadra sana, kwa maslahi ya umma mimi sioni tatizo. Maana, hata kwenye vita kuna wapambe ambao wanaweza kujitokeza kukinga vifua vyao ili risasi isimpate kamanda au kiongozi wao wanaomlinda. Huwezi kusema askari wa upande mwingine wasubiri kwanza hadi huyu aliejitokeza aondoke.

Uwezekano mdogo kama huo upo pia hata katika makosa mengine yasiyohitaji adhabu ya kifo. Kwamba, mtu anaweza kufungwa maisha kwa kosa ambalo hakulifanya. Tukufuata maoni yako inabidi hata adhabu ya kifungo cha maisha au kifungo chochote isitolewe maana hamna uwezekano wa kuthibitisha mashitaka asilimia mia moja.
 
Unamaanisha kwamba mtu akajisingizia mwenyewe kwamba ameuwa ili kumuokoa mtu mwingine? Kama kuna kesi kama hizo, ambazo ni nadra sana, kwa maslahi ya umma mimi sioni tatizo. Maana, hata kwenye vita kuna wapambe ambao wanaweza kujitokeza kukinga vifua vyao ili risasi isimpate kamanda au kiongozi wao wanaomlinda. Huwezi kusema askari wa upande mwingine wasubiri kwanza hadi huyu aliejitokeza aondoke.

Uwezekano mdogo kama huo upo pia hata katika makosa mengine yasiyohitaji adhabu ya kifo. Kwamba, mtu anaweza kufungwa maisha kwa kosa ambalo hakulifanya. Tukufuata maoni yako inabidi hata adhabu ya kifungo cha maisha au kifungo chochote isitolewe maana hamna uwezekano wa kuthibitisha mashitaka asilimia mia moja.

Mkuu tatizo moja mtu akikubali kosa ili amuokoe mwingine (mfano mtoto wake) hapo tatizo lipo sababu jambazi anaweza akawa ameokoka na mtu mzuri ameokoka..,

Pili gharama ya kuhukumu kifo ni kubwa mno kwanza lazima watu wapate uhakika zaidi na zaidi kwamba kweli alifanya alafu ikija kubainika kwamba walifanya kosa hili jambo haliwezi likawa reversible.., kwanza itaweka doa kwenye mahakama forever.., pia watu wanaweza waka-sue kwa gharama kubwa sana.

Anyway ili tusiende mbali naomba unipe faida ya kunyonga ili tuone kweli kama kunyonga kunakidhi hizo faida.., Kufunga maisha sio kwamba tunafunga tu sababu jamii ni masochists au barbaric.., bali ni kutoa watu kwenye jamii ambao ni menace to society pia as well as sheria inabidi ionekane kwamba imetendeka
 
Afadhali umekuja G....Hebu niambie, akinyongwa unajislia nafuu?

Najiskia nafuu mtu aliyemuuwa wangu nae akiondoka...............or else afungwe lakini anilipe fidia :] Maana alomuuwa alikuwa ana economic benefit pia
 
Najiskia nafuu mtu aliyemuuwa wangu nae akiondoka...............or else afungwe lakini anilipe fidia :] Maana alomuuwa alikuwa ana economic benefit pia

Nadhani hii inakuwa na manufaa sana kwako sababu kama mtu alimuua ndugu yako kwa mateso au hawa wanaotoa kiungo cha binadamu (au hata rape) inaweza kuacha kovu la maisha kwa mtu ambalo ni mateso kuliko hata kifo..., nadhani watu kama hawa kupewa instant kifo inakuwa ni kama wameget off lightly
 
Back
Top Bottom