Adhabu ya Kunyonga Hadi Kufa imepitwa na wakati?

VoiceOfReason

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,194
1,355
"Why do we Kill People who Kill People to Show that Killing People is Wrong ?"

Je ni sawa kuwa na Hukumu ya Kifo?

Baada ya yule Chizi wa Norway kuua kadamnasi ya watu (ukizingatia Norway life Sentence ni limited kwa miaka 21 tu) Je ni muhimu kuwa na hukumu ya kifo? Ni nini hasa faida ya hukumu ya kifo?

Je hukumu ya kifo inafanya watu waogope kutenda maovu kwahiyo ni njia nzuri au ni kuonyesha hata sisi hatuna tofauti na waliofanya hayo maovu?

I can argue kwamba huenda hukumu ya kifo ni adhabu rahisi sababu badala ya kumfanya mtu ku-suffer kwa kosa lake, tunampumzisha. Je sio vema kumfunga mtu maisha na kumfanyisha kazi ngumu kwa maisha yake yaliyobaki na kila alichonacho au atakachokitengeneza kiende kwa wale aliowatenda?

What do you think?

The answer is simple, "death penalty haina maana".

Tafakari mifano hii:

1. Mtu akiuwa tunataka nasi tumtendee hivyo, yaani tit for tat (jino kwa jino, jicho kwa jicho). Hii ni tafsiri potofu make ni tabia ya kinyama tu kulipiza kuuwa kwa kuuwa, kubaka kwa kubaka. Matokeo yake vifo, ubakaji utaongezeka badala kupungua.

2. Kwa vile kuuwana ni unyama, imetokea mara kadhaa ajira ya kunyonga watu kukosa waajiriwa hasa nchi kama malawi watu hurundikana gerezani wanyongaji hawaonekani. Je wanaoshabikia adhabu hii wapo tayari kwa tenda hii?

3. Adhabu hii ni feki, make kwa kuhofia kutia saini ya kuidhinisha kifo, tangu utawala wa Mkapa, hapa tz hajanyongwa mtu. Ni Nyerere na Mwinyi tu walioidhinisha.

4. Watu wengi hushabikia adhabu hii kwa vile hawahusiki moja kwa moja kama kutia saini na kutia kitanzi shingo ya mtuhumiwa. Mifano michache hapo juu inaonesha ugumu wa jambo hili.

5. Kwa mujibu wa maendeleo na ustaarabu wa kisasa uliotukuka, Haki ya Kuishi kwa Binadamu (Right to life) haiwezi kunyang'anywa na yeyote, regardless kosa lililofanyika. Ndo maana marais wengi wenye kuheshimu hili hawaweki saini.

Hitimisho:Tutumie njia mbadala za kuwafanya wakosaji watumikie adhabu zao huku wakizalisha mali katika magereza ili tukuze uchumi badala ya kushabikia visasi vya kuuwana na kulawitiana.

Maada nzuri sana, lakini majibu hayatoshelezi haja( not adequate). Whether adhabu ya kifo ni sahihi or siyo sahihi inatakiwa ichambuliwe kwa mtazamo wa kisheria na siyo kihisia (emotional).

SECTION 197 OF THE PENAL CODE OF TANZANIA (cAP 16)

Section 197 of the penal code provides inter alia that, Any person convicted of murder shall be sentenced to death:
*Hii inamanisha kwamba kila atakaye patikana na hatia ya mauaji atahukumiwa kunyongwa.


MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU ADHABU YA KIFO

Serikali inasimamia adhabu ya Kifo kwa mujibu wa sheria. kwa kuwa kosa la mauaji limeharamishwa na sheria za nchi, hivyo basi ni jukumu la Serikali kupitia sheria zilizotungwa na Bunge kuwalinda raia wake dhidi ya udharimu/Ukatili.

NINI MAANA YA MAUAJI (MURDER)

Sheria ya adhabu(penal code, Cap 16) particularly on section 196 provides for the difinition for murder, it provides that ,
Any person who of malice aforethought causes the death of another person by an unlawful act or omission is guilty of murder.

MAKOSA YANAYOWEZA KUSABABISHA ADHABU YA KIFO

(1) MAUAJI (MURDER) Contrary to section 196 of the penal code

(2) UHAINI (treason) contrary to section 39 (1) of the penal code

Note: watu waliopiga mawe msafara wa Rais Kikwete huko mbeya wangeweza kushitakiwa kwa uhaini na wangeweza kunyongwa kwa mujibu wa sheria inavyosema.

ADHABU YA KIFO NI SAHIHI OR SIYO SAHIHI

Kumekuwebu mjadala mkubwa kuwa adhabu ya kifo siyo sahihi kwani inakinzana na Katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 14 kwamba kila mtu ana haki ya Kuishi. na hoja ni kwamba sheria ni mbaya, inatoa Haki kwa mkono wa kulia na kuichukua kwa mkono wa kushoto.

KESI ZENYE HISTORIA (LANDMARK) KUHUSU ADHABU YA KIFO


Kesi iliyohusisha serikali dhidi ya Mbushuu, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ilitoa Hukumu ya Kifo. ni Kesi yenye umaarufu wa aina yake kwani ilileta kutunishiana Misuli kwa Majaji wenyewe na Serikali kwa Upande Mwingine.

AGNES DORIS LIUNDI VS. REPUBLIC(1979)

Aliyekuwa mke wa Jaji Liundi ambaye ni mama Mzazi wa Taji Liundi (Mtangazaji wa TBC1) alihukumiwa Kunyongwa na mahakama Kuu ya Tanzania, kwa kupatikana na hatia ya Mauaji. at last, alisamehewa na Rais (Mwl. Nyerere)

DINI VS SHERIA ZA NCHI

Kwa mtazamo wa dini siyo sahihi kuhukumu mtu kwa kuwa mwenye mamlaka hayo ni mwenyezi Mungu Pekee. However, kwa kuwa serikali haina dini, adhabu hiyo inaendelea kuwa sahihi, until otherwise amended to suffice the interest of the ruling class...!!

POINT TO NOTE:

Dunia ya leo sio sehemu salama ya kuishi, changamoto ni nyingi sana. Uhalifu wa kutisha na binadamu amekuwa katili kumshinda hata shetani. Hivyo basi adhabu za kifo haziwezi kufutwa, mpaka jamii inakapostarabika na itachukua muda mrefu sana kufika huko.

Wasalaam!
 
yap ni sawa kuwa na hukumu ya kifo....
(kwa watu kama mafataki na wabakaji)

(ingawa kwa upande wa Dini especially Christianity hairuhusiwi
kumuhukumu mtu)
 
hii hukumu hata mimi nafikiri ni rahisi sana,ukizingatia mtu ana rest in peace bila taabu
Wanasema huwezi kujua machungu ya kifo hadi siku ya zamu yako!
Kimsingi Nia ya adhabu ya kifo ni partly kumwadhibu anayekuwa ametenda kosa, lakini pia ni kutoa funzo kwa wanaobaki, wajue kuwa kosa fulani lina implication fulani, and let me tell you broda, it works out!
 
Hukumu ya kifo ni upande mmoja na kutekeleza hukumu ya kifo ni upande mwingine. Suala la 'uhalali' wa hukumu ya kifo ni tete sana. Inategemea unatilitizama kutoka upande gani (na pande zipo nyingi!). Kwa vyovyote vile, mimi naamini uwepo wake unapunguza kwa kiasi kikubwa 'hamu' ya binaadamu mmoja kutaka kumuuua mwingine (kinyume cha sheria).
 
yap ni sawa kuwa na hukumu ya kifo....
(kwa watu kama mafataki na wabakaji)

(ingawa kwa upande wa Dini especially Christianity hairuhusiwi
kumuhukumu mtu)

Siongelei dini kabisa hapa ninaongelea manufaa yake au kufanya kwake kazi.. Je issue ya mafataki na wabakaji je sio adhabu kali zaidi kuwa-castrate ?; sababu kuwaua ni kuwapa - rest in peace na sidhani kama ita-act kama hindrance kwa crime kuwaua
 
Wanasema huwezi kujua machungu ya kifo hadi siku ya zamu yako!
Kimsingi Nia ya adhabu ya kifo ni partly kumwadhibu anayekuwa ametenda kosa, lakini pia ni kutoa funzo kwa wanaobaki, wajue kuwa kosa fulani lina implication fulani, and let me tell you broda, it works out!

Je kifungo cha maisha sio adhabu tosha (yaani kazi ngumu kila siku) haifanyi watu waogope kufanya hilo kosa ?, sababu hukumu ya kifo sidhani kama ni justice done kwa ndugu wa mfiwa tena wengine might argue ni adhabu ndogo kuliko jamaa angebaki maisha yake yaliyobaki anafanya kazi ngumu kila siku na faida ya hiyo kazi ngumu (kama anazalisha) iende kwa wale waliozurika..
 
Wanasema huwezi kujua machungu ya kifo hadi siku ya zamu yako!
Kimsingi Nia ya adhabu ya kifo ni partly kumwadhibu anayekuwa ametenda kosa, lakini pia ni kutoa funzo kwa wanaobaki, wajue kuwa kosa fulani lina implication fulani, and let me tell you broda, it works out!

Kaka nafikiri kifo sio adhabu,ni ngumu kusema kifo ni kibaya wakati hakuna mtu aliyeenda na kurudi kutuambia jinsi kifo kilivyo kibaya,....inawezekana kabisa huko ni kuzuri kuliko hapo,..binadamu kwa asili tunapenda kuogopa vitu tusivyovijua na kupuuzia tunavyovifahamu,...nafikiri kuwe na dhabu ingine yenye machungu kuliko hiyo ya kifo.

Hebu fikiria,mtu anlawiti vitoto,anaua watu kwa sababu na imani za kipuuzi,............hapa ni lazma mtu ajutie kile alicho kifanya
 
Hii issue ni ngumu sana, mara nyingine huwa nakaa nafikiria naona kama adhabu ya kifo sio nzuri, kwa sababu mhusika anaponyongwa kimsingi waliodhurika na matendo yake hawapati chochote na yeye pengine anaweza asipate nafasi ya kujifunza na kujuta kwamba nilichokifanya hakikuwa sawa, lakini mara nyingine unafikiri unaona kuna watu akili zao ni mboovu na adhabu yao ni hiyo hamna kitu kingine, mfano majambazi wanaovamia na kuua labda familia nzima watu kama hao unadhani utawafanyaje?
 
Siongelei dini kabisa hapa ninaongelea manufaa yake au kufanya kwake kazi.. Je issue ya mafataki na wabakaji je sio adhabu kali zaidi kuwa-castrate ?; sababu kuwaua ni kuwapa - rest in peace na sidhani kama ita-act kama hindrance kwa crime kuwaua
Hukumu ya kifo si kwa ajili yao tubali kuwapa peace of mind waliokosewa.. Na tukiwafunga kifungo cha maisha watakuwa wanaTumia nguvu zetu ku ishi (tax)
 
Hukumu ya kifo si kwa ajili yao tubali kuwapa peace of mind waliokosewa.. Na tukiwafunga kifungo cha maisha watakuwa wanaTumia nguvu zetu ku ishi (tax)
Watatumia nguvu zetu kama watakuwa wanakataa na kulala tu, tunaweza tukawafanya productive kwa kufanya all those unwanted jobs ambazo watu wengine hawataki kuzifanya.., na kama issue ni kuwafanya wasi-abuse watoto je castration sio effective method?
 
Kaka nafikiri kifo sio adhabu,ni ngumu kusema kifo ni kibaya wakati hakuna mtu aliyeenda na kurudi kutuambia jinsi kifo kilivyo kibaya,....inawezekana kabisa huko ni kuzuri kuliko hapo,..binadamu kwa asili tunapenda kuogopa vitu tusivyovijua na kupuuzia tunavyovifahamu,...nafikiri kuwe na dhabu ingine yenye machungu kuliko hiyo ya kifo.

Hebu fikiria,mtu anlawiti vitoto,anaua watu kwa sababu na imani za kipuuzi,............hapa ni lazma mtu ajutie kile alicho kifanya

Ukizingatia method huenda ikawa ni sumu au umeme yaani dakika chache tu mtu ushakufa..., ingekuwa kifo ni kibaya kuliko ku-face reality watu wangekuwa hawajiui (wala hitler asingejimaliza angesubiri aendelee ku-enjoy maisha)
 
Hukumu ya kifo si kwa ajili yao tubali kuwapa peace of mind waliokosewa.. Na tukiwafunga kifungo cha maisha watakuwa wanaTumia nguvu zetu ku ishi (tax)
Wafungwa si kula kulala (hasa kwa tanzania). Huko wanafanya kazi za kila aina, kilimo, ujenzi, uhunzi nk.Na mazao wanayozalisha huwa yanauzwa na nadhani chakula pia wantumia kujilisha kwa kiasi kikubwa. Magereza hutumika kama vyuo vya mafunzo vile....wanafunzwa kazi mbali mbali kwa hiyo shaka ya kodi ondoa.Mi nadhani mkosaji anayestahili adhabu ya kifo ni heri tu apewe adhabu nyingine kali mpaka ajutie kosa lake. Hata waathirika wa kosa lake labda kwa njia hiyo watapata ahueni.
 
Kwa upande wangu kwa kweli sikubaliani na hukumu ya kifo na sidhani kama inaleta nidhamu kwenye jamii, kwamba wengine wataogopa kufanya mauaji!

Mabadiliko ya mtu hayatokani na hofu, bali inahitajika badiliko la ndani kujua kuwa kuua ni vibaya, na sipaswi kufanywa hivyo!
 
Kwa upande wangu kwa kweli sikubaliani na hukumu ya kifo na sidhani kama inaleta nidhamu kwenye jamii, kwamba wengine wataogopa kufanya mauaji! Mabadiliko ya mtu hayatokani na hofu, bali inahitajika badiliko la ndani kujua kuwa kuua ni vibaya, na sipaswi kufanywa hivyo!
Kweli kabisa hata wale watu wanaofanya maovu sidhani kama huwa wafanya huku wanategemea kushikwa, pili kunaweza kukawa na adhabu ambazo ni ngumu na mbaya na zikawanufaisha hata wale waliotendwa mfano hata kama mkosaji ana mali nyingi kuweza kuwapa fidia waliokosewa as well as kufungwa na kufanya kazi ngumu
 
Back
Top Bottom