ACT- Wazalendo kubeba gharama mazishi ya Bwege

ACT- Wazalendo kubeba gharama mazishi ya Bwege

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
2,115
Reaction score
3,489
Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha aliyekuwa mwanachama wake, Seleman Bungara maarufu Bwege, kilichotokea ghafla asubuhi ya Machi 30, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu ya kusafisha figo jijini Dar es Salaam. Chama hicho pia kimeahidi kugharimia mazishi ya marehemu.

Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu, imeeleza kuwa kifo cha Bungara ni pigo kubwa kwa familia yake, chama pamoja na wafuasi wa siasa za upinzani nchini. Semu amesema chama kimepokea taarifa hizo kwa mshtuko na huzuni kubwa, kikikumbusha kuwa Bungara alikuwa mwanachama wao kabla ya hivi karibuni kutangaza kuhama chama.

Aidha, Semu ametoa pole za dhati kwa mke wa marehemu, Mwanawetu Said Zarafi, ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya ACT Wazalendo, pamoja na familia, ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na msiba huo

Soma pia TANZIA - Seleman Said Bungara (Bwege) afariki dunia

1774943490391.png


1774942863264.png
 
Sio kweli
Alishahamia Chadema na hata majuzi tu kawapa Bavicha gari yake kwenda kufanya operesheni ya kukitangaza Chadema jimboni kwake.Ila kama ACT wanataka kugharamia mazishi yake pia siyo vibaya kwani ni mtu ambaye waliwahi kuwa naye kwenye chama chao.
 
Alishahamia Chadema na hata majuzi tu kawapa Bavicha gari yake kwenda kufanya operesheni ya kukitangaza Chadema jimboni kwake.Ila kama ACT wanataka kugharamia mazishi yake pia siyo vibaya kwani ni mtu ambaye waliwahi kuwa naye kwenye chama chao.
😂 ACT wameamua kutangaza kuubeba huo msiba kwa nia fiche. Wanajua wananchi wa kule walikuwa wanamkubali sana, hivyo wanahofia akaitajwatajwa kuwa alihamia cdm watapoteza huo mtaji. Kwahiyo wanataka ionekane bado ni mwana ACT kusudi wasipoteze huo mtaji.
 
Mke wa marehemu Bwege ni kiongozi mkubwa ACT kwahiyo msiba kubebwa na ACT ni sahihi. Ikumbukwe ishu za msiba familia ndo huamua zaidi. Kama familia imeamua ACT ndo ihusike hakuna wa kupinga. Cha muhimu CHADEMA wasije kuanza kuwatukana familia kama walivyozoea kutukana yeyote aliye kinyume nao.
 
Mke wa marehemu Bwege ni kiongozi mkubwa ACT kwahiyo msiba kubebwa na ACT ni sahihi. Ikumbukwe ishu za msiba familia ndo huamua zaidi. Kama familia imeamua ACT ndo ihusike hakuna wa kupinga. Cha muhimu CHADEMA wasije kuanza kuwatukana familia kama walivyozoea kutukana yeyote aliye kinyume nao.
Wacha uzushi dada lini Chadema wametukana? Sisi tunajua Samia ndiye bingwa wa kubwatuka kwa sababu hana uwezo wa kujibu hoja.
 
Kwa kawaida msiba unabebwa na 3rd party kama kuna ridhaa ya familia, hivyo kama ACT wametangaza basi walishapewa ridhaa na familia ya Bwege...
 
Hapana. Ukitangaza bila kadi ina maana katika orodha ya wanachama haumo hivyo ni shabiki tu na sio mwanachama. Ingawa najua kuwa CDM wasingeweza kumpa kadi kutokana na zuio la Mahakama ukweli unabaki kuwa hakuwa mwanachama wa Chadema umauti ulipomkuta. Aidha, alikuwa anahudhuria kesi za Lissu hata kabla hajatangaza kujitoa ACT kwa hiyo hicho sio kigezo cha uanachama wake wa Chadema. ACT Wazalendo ina haki ya kuubeba msiba kwa sababu mjane wake bado ni kiongozi wa ACT Wazalendo.
This is not a legal battle! moaka kihitaji kadi. Nikitangaza inatosha

Amandla...
 
Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha aliyekuwa mwanachama wake, Seleman Bungara maarufu Bwege, kilichotokea ghafla asubuhi ya Machi 30, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu ya kusafisha figo jijini Dar es Salaam. Chama hicho pia kimeahidi kugharimia mazishi ya marehemu.

Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu, imeeleza kuwa kifo cha Bungara ni pigo kubwa kwa familia yake, chama pamoja na wafuasi wa siasa za upinzani nchini. Semu amesema chama kimepokea taarifa hizo kwa mshtuko na huzuni kubwa, kikikumbusha kuwa Bungara alikuwa mwanachama wao kabla ya hivi karibuni kutangaza kuhama chama.

Aidha, Semu ametoa pole za dhati kwa mke wa marehemu, Mwanawetu Said Zarafi, ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya ACT Wazalendo, pamoja na familia, ndugu, jamaa na marafiki wote walioguswa na msiba huo

Soma pia TANZIA - Seleman Said Bungara (Bwege) afariki dunia

habari ya ufahari mazishini ni vitu useless sana wanasiasa hujaribu kuleta
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom