Accidents at Kibaha: A Scientific Reason?

hahaaa Ogah, mie niliishia kuwa Fundi Mchundo. Majaribio kadhaa ya kutaka kupandisha grade, yamekwama katika dakika ya mwisho na nikaamua kabisa kuachana na haya mambo ya barabara. Ila kumbukumbu imebaki kidogo.

Nafikiri hapo sijui kama utapata michoro yake. Wanaweza kuwa walilipua tu na mtu akachukua hela zake kwa kudesign barabara. Matokea yake ndiyo hayo.
Unafahamu miaka ya 90 nikiishi nchi za watu, kulikuwa na jamaa mmoja akiwa na Masters. Juu yake kulikuwa na Dr na Profesa mmoja. Ila hawa jamaa pamoja na shule kubwa zaidi ya jamaa, walikuwa siku zote wanakuja kumuuliza na walikuwa wanakiri kabisa kuwa wao wana makaratasi na jamaa ana KIPAJI na Uzoefu zaidi yao.

Ndiyo maana siku zote nawaasa watu kuwa Traffic Engineering, si kitu cha kusema "tujenge fly-over, tutenge barabara, tupanue barabara, tuongeze lane......." Ni zaidi ya hiyo. Unaweza kufanya vitu vyote na bado ajali zikaongezeka. Kuna trick nyingi sana hutumika kwa kucheza na tabia za binadamu. Ndiyo maana jamaa wengi walikuwa wakija na planing zao, yule mzee mwenye Master anaanza kucheka na kusema "ohhhhhh, hapa umetengeza MACHINJIONI".

Hebu jaribu kuwasiliana na watu wa Tanroad mkoa wa Pwani na Makao Makuu, wanaweza kuwa msaada mkubwa kwako. Ila kwa haraka haraka, Waziri na watu wa Tanroad, wangeliweka vile vyuma vya kutenganisha barabara/lane haraka sana sehemu zote zinazotokea ajali. Si wote watafuata ila usumbufu watakaoupata, utafanya wengi wawe na subira ya kutokuvuka upande mwingine ili ku-overtake. Sidhani kama vile vyuma ni aghali. Ukifanikiwa basi tujulishe ili tufurahi wote kwa kuwa kazi yako inaweza kuokowa maisha ya watu wengi kama si hata ya kwangu/ya kwako au ndugu zetu.
 
Kwa kweli mnanifanya niwapende kwani mnagusa mambo ya kisayansi!!

Ogah,



Nakubaliana na wewe kitu kimoja, NI MARUFUKU kuweka kona kwenye bonde au mlima. Hapa wala haihitaji kuongeza upana wa barabara kwani HURUHUSIWI kulipita gari kwenye kona au mlima. Lile eneo la ile ajali, kuna bonde na kuna kona. Nashindwa kuelewa Mhandisi aliyeruhusu ujenzi wa hiyo barabara.

Nimemtuma kijana mmoja akipata muda atuletee picha ya hili eneo maana sijaliona vizuri.

Walau wangelizitenga kabisaaa hizo barabara kwa kuweka ukuta au fance katikati ili milele kuzuia watu ku-overtake kwenye maeneo hayo. Hiyo ya pili hapo chini ni nzuri sana kwani mnaweza kuindoa kwa muda na kuruhusu magari kutumia upande mmoja tu. Kuongeza upana wa Lane kunaongeza tu comfort ya kuendesha, ila hakusaidii sana kuongeza usalama. Lile eneo inatakiwa WALAZIMISHE madereva wafuate sheria. Kila njia itumie kuwalazimisha madereva. Hili la eti madereva wetu wazembe, si kweli. Binadamu ni kama Wanyama. Ukimpa mita moja, atachukua km1. Sasa dawa ni kumpa nini ili achukue 1m?

3491584609_92ca7aba50.jpg



wire_rope_dividers.jpg
Nimependa hayo mapendekezo kwa sababu moja ni more affordable, hayahitaji mabadiliko makubwa kwenye barabara na yanafanya kile unachopendekeza.. KULAZIMISHA madereva.. as a matter of fact mimi nilikuwa nafikiria kama wanavyofanya hapa sehemu nyingine wameweka concrete partitions tena ingekuwa kwa kilometa kadhaa kabla ya kuingia mjini..

as a matter of fact hili la partitions linaweza kupunguza ajali nyingine sana... badala ya kuweka matuta.
 
Kwa kweli mnanifanya niwapende kwani mnagusa mambo ya kisayansi!!



Nimemtuma kijana mmoja akipata muda atuletee picha ya hili eneo maana sijaliona vizuri.

Nimependa hayo mapendekezo kwa sababu moja ni more affordable, hayahitaji mabadiliko makubwa kwenye barabara na yanafanya kile unachopendekeza.. KULAZIMISHA madereva.. as a matter of fact mimi nilikuwa nafikiria kama wanavyofanya hapa sehemu nyingine wameweka concrete partitions tena ingekuwa kwa kilometa kadhaa kabla ya kuingia mjini..

as a matter of fact hili la partitions linaweza kupunguza ajali nyingine sana... badala ya kuweka matuta.


Nakubaliana na wazo la KUWALAZIMISHA madereva kufuata sheria, kwa sababu imeonekana hawawezi kuzifuata sheria hizo.
Nimependa huo uzio katika kati ya barabara hapo katika picha.
 
Mwana kijiji,

Hizo za juu si nzuri sana maeneo ya karibu na mjini. Mara yakifanyika matengenezo au dharula, inakuwa shida sana kuziondoa na kutumia upande mmoja. Ndiyo maana zile road barrier zile bana unazifungilia kwenye vinguzo zinakuwa nzuri sana. Ila kwa Tanzania naogopa wataiba.

Nilikuwa nimesahau vile vyuma wanapigilia barabarani vinaitwaje. Hivi kumbe vyote viko kwenye kundi wanaloita "Mechanical Markers". Waweza ziangalia hapa maelezo yake:
[ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Road_surface_marking[/ame]

Baadhi ya picha zake kwa hizi za kisasa zinazotumia mwanga wa jua ziko hapa chini:
solar-road-stud.jpg


Producer wako wengi sana na kama sikosei bei inaanzia kwenye dola 2 kwenda juu kwa piece moja. Hiyo ni bei ya Wachina na ni FOB, hapo ikiwa na maana wewe ni kusubiri mzigo wako Tanzania tayari. Nafikiri kwa Tanzania kwa haraka sana zingeletwa hizi ROAD STUD (pichani juu zinazongaa) na kupigiliwa barabarabarani nyingi tu sehemu zote ambazo zimekuwa zikitokea ajali mara kwa mara.

http://www.alibaba.com/manufacturers/solar-road-stud-manufacturer.html
 
nauliza hivi madereva wa Tanzania( magari makubwa na mabasi ya abiria ) wanakuwa na log book?
Kwani kila dereva wa gari la biashara lazima awe na log book na analog kila anapoendesha na kila kwenye mzani lazima wakague log book na masafa aliyotoka na anayokwenda, ikiwa ni tofauti lazima gari liende uani na malipo pia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom