Tanganyika1
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 422
- 86
Yaani huwezi amini kilichotokea leo kwenye basi la abood dar- iringa. Gari halikujaza, so kufidia nafasi jamaa wakaamua kupakia vifaranga vya kuku..(mabox meng tu) mara abiria m1 akaanza chokochoko, alipiga simu ofisi za abood dar na moro kueleza tukio hilo. Mara konda kaenda kwa yule abiria na kuanza kumpiga sound ili aache kuchonga. Jamaa katoa msimamo wake, 1. Alitaka wale vifaranga wateremshwe au 2. Gari isimame kusubiri gari nyingine ili yeye apandishwe kupisha hao kuku. Mwisho wa siku vifaranga waliteremshwa.....baada ya hapo pakaanza mjadala wa abiria na mawazo tofauti...wange achia tu hao vifaranga kwani mwenye nao naye anatafuta maisha,...ooh huyo jamaa hajui maisha akikua atajua.....ukute hata yeye uko anakokwenda anakaa nyumba 1 na kuku...aah jamaa kaamua kujionyesha tu kwa watu (kwa abiria wenzake)...kifupi ni kwamba meng yalizungumzwa dhidi ya jamaa kwa kitendo chake cha kuto kukubali kusafiri na kuku.... Sasa mi nikashtuka kidogo kuona ni jinsi gani watz hawajitambui, yaaoi wanaona ni sahh kwa wao kuchanganywa na mifugo ndani ya basi, ndo nikaamua ku shara na wanaj amvi.