Abood wamefulia

Tanganyika1

JF-Expert Member
May 10, 2011
422
86
Yaani huwezi amini kilichotokea leo kwenye basi la abood dar- iringa. Gari halikujaza, so kufidia nafasi jamaa wakaamua kupakia vifaranga vya kuku..(mabox meng tu) mara abiria m1 akaanza chokochoko, alipiga simu ofisi za abood dar na moro kueleza tukio hilo. Mara konda kaenda kwa yule abiria na kuanza kumpiga sound ili aache kuchonga. Jamaa katoa msimamo wake, 1. Alitaka wale vifaranga wateremshwe au 2. Gari isimame kusubiri gari nyingine ili yeye apandishwe kupisha hao kuku. Mwisho wa siku vifaranga waliteremshwa.....baada ya hapo pakaanza mjadala wa abiria na mawazo tofauti...wange achia tu hao vifaranga kwani mwenye nao naye anatafuta maisha,...ooh huyo jamaa hajui maisha akikua atajua.....ukute hata yeye uko anakokwenda anakaa nyumba 1 na kuku...aah jamaa kaamua kujionyesha tu kwa watu (kwa abiria wenzake)...kifupi ni kwamba meng yalizungumzwa dhidi ya jamaa kwa kitendo chake cha kuto kukubali kusafiri na kuku.... Sasa mi nikashtuka kidogo kuona ni jinsi gani watz hawajitambui, yaaoi wanaona ni sahh kwa wao kuchanganywa na mifugo ndani ya basi, ndo nikaamua ku shara na wanaj amvi.
 
Kwa nijuavyo na niliyoyaona nikisafiri wiki hii kuja Mbeya...
1. Mabasi mengi hayana & hawafungi mikanda,
2. Mabasi yanayochelewa kutoka Dar baada ya saa 12-asbh...hawajali kuzidisha abiria.
3. Makonda hawajali ni aina gani ya mzigo uingie passenger's lot na mizigo ipi iende kwenye buti.
4. Hakuna coordination nzuri kwa kugonganisha tickets, hawana utaratibu mzuri yaani wako very improper...tena afadhali ya Abood kuliko hizo kampuni zingine ndogo-ndogo, ni balaa.

Tukichukulia kiujumla wa hao vifaranga kiukweli si ustaarabu kuchanganya na abiria waila (kwa mazingira yetu) tunapaswa pia kuwa na hali ya utu (humanity) kwa kumtazama pia huyo aliyeweka kuku huenda ALIWAOMBA 'WAMSAIDIE' nae akajipatie rizki. Ningewashauri hao wote wangejawa na UTU KWANZA (humanity first).
 
Title haiendani na mada, sasa wapi Abood walipofulia?
<br />
<br />
we ndo hujaona au mawazo yako hayaoni tatizo. Walipofulia ni kitendo cha kupanga mabox ya vifaranga kwenye siti. Tena hayapungui 20. Tht means hawatambui kama kufanya hvyo c sahh, au wamewadharau abiria wakijua kuwa watz ni majuha na hawatafanya chochote. Aidha walipokua wanamwomba yule alokua anachonga konda alisema....kaka samahani, leo gari lenyewe c unaliona liko tupu yani hata hesabu ya tajiri haijatimia....mchangiaji mwingine amegusia humanity. Yani huo utu uanze kwa abiria tu?...coz yeye hakuomba, wala hakuwaza adha itakayo wakuta abiri alijal hesabu ya tajiri. Yaan wale vifaranga wanakelele, wananuka, wanatoa vinyoya,....who knws labda wana magonjwa ie mafua? Hayo yote ilbid tuvumilie tu? Au ndo ujamaa huo?.......hahaha tanzania bana.
 
Title haiendani na mada, sasa wapi Abood walipofulia?
Mkuu nakubaliana na wewe kuwa mada haiendani na title, lakini yumkini mwandishi alimaanisha mtu akifulia anaOKOTEZA chochote ilmradi kufidia gharama za mafuta.
Mbali na hilo, ningependa kuongelea kero za magari ya Abood pia! Nilisafiri na mabasi yao Dar Morogoro! Dereva anakimbiza, na kwa kuwa ni mida ya jioni hao madereva hawaogopi kuweka ngedere! (i.e abiria wa ziada wanaokaa karibu na dereva kwenye injini na wengine wanasimama). Kibaya siku hiyo dereva alaikuwa anakimbiza gari sehemu flani kataka kupita gari jingine, kumbe mbele kuna basi nyingine inakuja kidogo kugongana uso kwa uso. Nikamwambia dereva punguza mwendo, kumbe abiria wengine wanaona mwendo huo wa Km 130 au 140/saa ni sawa. Hao abiria wakasema kama sitaki mwendo mimi nipige chini! Nilipoona soo limizidi, nikawatumia text Abood wenyewe kuhusu mwendo wa dereva. Pale pale dereva kapunguza mwendo na kuanza kulalama! Akaamua kutembea spidi 40km/hrs! Tulifika Morogoro saa 3 badala ya saa 1jioni! Ni wajeuri hao madereva
 
Scandinavia Express amekuja kivingine anaitwa Green Star anakwenda Mwanza na kama kawa amewanufaisha wachina... anatumia YUTONG.... nilipanda mwaka jana kwenda Mwanza... mtu wake wa karibu amesema watatisha zaidi ya zamani wameshajifunza somo wanajua wapi walipojikwaa na wapi waliangukia... I pray for them..
 
Hawa jamaa kiukweli kabisa sijui ni wamefulia ama lah!! Nilipanda siku moja abood la saa sita la kuelekea Iringa!!! Loh!! Sirudii tenaaa bora nilale tu Dar na hata hapa Iringa nikilikuta stand sipandi hata kwa dawa!!!

Ubaya wa sura ni case nyingine coz body kaunda mwenyewe hapo Moro sijui!!! Basi baya, ndani halifai hata kuitwa basi, staff carrier zimelegea mizigo inadondokea watu hovyo!!! Masufuria yameegeshwa kama speaker (sitaki kuamini kuwa Abood hawana hela kununua speaker nzuri) , mibati inaning`inia hovyo!!!

Hivyo viti sasa, mabenchi matupu halafu vichafuuu!!! Basi linapotembea kwa kasi na breki za hapa na pale ile top ya juu ya siti inasogea mbele inabidi wote wawili msimame muirudishe nyuma (nilikaa upande wa 2 katika 2*3) ilikuwa ni adhabu kwa kweli hasa kwenye matuta, likiruka tu muanze kurekebisha siti!!!

Kwa kweli kama kuna anayefahamiana na mmiliki wa hayo mabasi ampe taarifa tu kuwa mabasi yake ya saa sita (yakitoka Dar na saa nne yakitoka Iringa) hayapandwi na watu sababu ya ubaya maana siku hiyo binti yangu alikuja na mamaye kunipokea stand alinicheka sana kuwa nimepanda madebe na hiyo story haimpotei kwani mara kwa mara anakumbuka na ni mtoto under 10 years.

Mbona ana marcopolo nzuri zinazokwenda Tunduma??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom