Abood bado hawajabadilika hadi sasa

Abood bado hawajabadilika hadi sasa

Kuna mdau kasema inawezekana wafanyakazi hawalipwi, naweza kukubali swala. Limekua kama daladala yaaani dereva,makonda,vishoka wote wanapeleka hesabu kwa boss tu ila mishe zote wanafanya wao kuanzia mafuta mpaka kujilipa.
Possibly true.
 
Na ustaarabu na comfort lkn kwa nauli iliyoenda shule...
Ukitaka vya bei rahis na ukereke kama mnavolalamika hapa panda hao wababaishaji aboud.

Me safari zangu ni dar to mwanza usafiri wangu ni allys star tu nikikosa bora nihairishe nisafiri siku nyingne
 
Dawa zao ni kufichua kwenye mitandao ya Jamii, kama hii JF. Muhimu iambatane picha na eneo husika na namba ya basi.
 
Kuna mdau kasema inawezekana wafanyakazi hawalipwi, naweza kukubali swala. Limekua kama daladala yaaani dereva,makonda,vishoka wote wanapeleka hesabu kwa boss tu ila mishe zote wanafanya wao kuanzia mafuta mpaka kujilipa.
Wanapeleka hesabu kama bodaboda!?

Alafu wamezua tabia ya kufaulisha abiria km nyanya wakifika Msamvu kwenda Dar au wakifika Magufuli kwenda Shekilango na baadhi ya abiria wamelalamika mizigo yao kupotea.

Nadhani hata Shekilango wangeondolewa warudi Magufuli.
 
Kutokana na masafari ya mara kwa mara, kitu ninachofanya ni kutumia pesa yangu vizuri, yaani nikijua kuna bus ni wasumbufu naunga route na sijawahi pata shida.
 
Hawaweki mafuta kwy Petrol Station ya mtu ila ya kwao tu Moro na Dar ndiyo maana wakiishiwa mafuta wanasubiri hadi gari la patrol lifike. Wako kama Wapemba ambao hawanunui bidhaa duka lisilo la Mpemba.

Shabiby ana Petrol Station yake na Hoteli yake.

BM ana Petrol Station yake.

Abood ana Petrol Station yake.

Msukuma kule Kanda ya Ziwa ana Petrol Station yake kwa ajili ya mabasi yake 50.

Check and balance hakuna.

Ma-RTOs nchi nzima wanayaogopa mabasi hayo ya wanasiasa. Ukiwapelekea kesi hupati msaada wala ushirikiano.

Ombeni MUNGU ampe mama nguvu za kumalizia SGR ndiyo mwarobaini wao na ndiyo mtajuwa JPM alikuwa proactive.
Wamiliki waliwahi kumuhamisha DTO fulani wa Kibaha akatupwa Kusini hukooo mpakani.

Kosa lake lilikuwa kufuta/kumaliza ajali Kibaha.
 
Taarifa muko kundi mnaotumika kibiashara kuandika taarifa za kuchafua.mimi nilifwatwa niandike nilikataa ndio maana mnaandika mnalipwa niliahidiwa laki 5 kama ntakuwa naandika kuchafua nikamwogopa mungu.
 
Huyu nadhan Mabus yake yashazoea uswahili, nimepanda gar la Mwanza tokea Morogoro, ilibidi nicheke vadala ya kukasirika, inasimama kila kituo hadi inauliza watu nyiee mnaenda ilihal hao watu wamebeba majembe wanaonekana wakienda zao shba kabisa.

Haya gari liko full ila as long kuna abiria anataka kupanda atapandiswa,

Kila stendi ya iwe ya kijiji, wilaya au mkoa itaingia, Stendi ya Gairo ikaingia ikakusanya wauza karanga za kuchemsha na wengineo ikawa hata pa kupumlia hamna,

Likafika Mbande stendi likaingia,

Kibaigwa stendi likaingia,

Nikasema hili Mwanza litatembeea week njiani,

Ikabidi nishuke tu njian nikaanzisha shuguli nyingine ku-buy time ili nipange safari nyingine upya na silu nyingine
😂😂
 
Wakuu habari za asubuhi

Abood ameleta mabasi mengi tu lakini hadi sasa hawataki kubadilika na tabia zao za ajabu ajabu.
Leo na safiri na Bus lao la Abood kutoka Tunduma kwenda Dar lakini cha kushangaza linabeba abiria Kama daradara njiani gari imejaa lakini konda bado anapakia watu njiani viti vyote vimejaa Hadi watu wengine wamekaa kwenye korido na wengine wamesimama.

Lakini pia siti uliyokatiwa ticket siajabu usikae unaambiwa kaa popote pale mjiriekebishe

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Waarabu na waswahili wa pwani mtindo wao wa management wanajua wenyewe. Ukiona wanafanya passenger transport hawafilisiki usifikiri hio ndio biashara yao.
 
Walitoa matangazo kuwa wanaanzisha njia ya Dar kwenda Karagwe.
Hadi leo haijaanza.
 
Wakuu mbona mnanitisha sana leo nmekata siti natoka musoma naenda dodoma, vp kuhusu route ya musoma dar gari za abood mana ndio wapya wameanza na happy nation
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom