Unachosema nakubaliana nawe mkuu ni waswahili haswa. Wiki iliyopita nilichelewa kidogo bus zile za saa 12 asubuhi nilikuta zishatoka, jamaa akanilengesha bus la Abood linalokuja Iringa ilhali mi naenda Mbeya wakaniambia watanifaurishia Iringa. Wakanipiga hela ndefu lakini sikujali as long as nitafika Mbeya swadaka. Aisee tulikaa toka saa moja ile mpaka saa nne kasoro, abiria tukamaindi sana ndio wakaamua walitoe lilipopark na kulipeleka kwa mabus ya Moro ili kuongezea abiria ili liondoke. So Kama abiria tusingekomaa bhasi lingeendelea kutega tu pale sheinzy.😬
Kimbembe sasa tulipofika gereji yao pale Moro, washenzi walituwekesha pale mpaka abiria mmoja akashuka kwenda kumkwida dereva ndio akalitoa na kuanza safari. Siisahau hii safari tunaingia Iringa stand saa moja kasoro na kufaulishwa bus la Mbeya na kuingia saa nane usiku.
Abood siwahitaji tena maishani mwangu hata mbadirike vipi.😬😬🙌