Abdul Nondo afunguka kuhusu bodi ya mikopo

Abdul Nondo afunguka kuhusu bodi ya mikopo

Mwanangu funga mdomo. Bado unahitaji shule, Ukumbuke Hii ni awamu ya tano. TLS mguu sawa
 
Vijana wa Lumumba kama kawaida yao kila kitu kwao ni hapana hata wakiambiwa ukweli
 
Ila tuongee ukweli kama umeweza kulipa zaidi ya 2.5 kwa miaka 7 ongeza 4 ongeza 2 halafu leo 1.5 ya chuo itakushindaje miaka 3
Ni kweli lakini alipokuwa analipa kiasi hicho alikuwa anaongeza au anapunguza! Mtu anaweza kuwa amejipanga na kudunduliza kiasi hicho kwa kujinyima. Hivyo siyo vyema kutoa mkopo kwa kigezo cha shule aliyosoma mhusika.
 
Mkuu usijitoe ufahamu, hiyo 1.5 ya chuo ni ada (school tuition fee) pekee bado madudu mengine kibao pesa kama hiyo au zaidi.

mkosoe Nondo ktk siasa zake zingine ila sio kwa hili la mikopo. dogo yupo sahihi kabisa.
hali ya kiuchumi hubadilika. Kuna kupunguzwa kazini, kampuni yako au uliyo ajiliwa kufilisika, kuugua n.k. vinaweza kupelekea mzazi kushindwa kuendelea kumlipia mtoto elimu ya juu kam private.
mzazi anaweza kuwa na mtoto wa kwanza yuko anaingia chuo na ana wadogo zake wako shule. huyu wa chuo anawekwa kando apate mkopo na pengine awapunguzie wadogo zake kwa kujibana. ni kupanga na kupangua na ku balance mambo yaende.
 
Ila tuongee ukweli kama umeweza kulipa zaidi ya 2.5 kwa miaka 7 ongeza 4 ongeza 2 halafu leo 1.5 ya chuo itakushindaje miaka 3

wewe huelewi kusoma . unaambiwa mzazi kaugua au kafilisika utapata wapi pesa
 
Ila tuongee ukweli kama umeweza kulipa zaidi ya 2.5 kwa miaka 7 ongeza 4 ongeza 2 halafu leo 1.5 ya chuo itakushindaje miaka 3
Nondo kajibu swali lako, rudia kusoma
 
Ila tuongee ukweli kama umeweza kulipa zaidi ya 2.5 kwa miaka 7 ongeza 4 ongeza 2 halafu leo 1.5 ya chuo itakushindaje miaka 3
Kwahyo chuo ukitoa 1.5 unapata hostel(malazi), chakula, kopi, vitabu na field allowance humo humo???

Kua uone dogo
 
Sasa kama bodi inakusanya marejesho hadi inavuka malengo kwa nini isiendelee na vigezo vile vile....otherwise wabadilishe wasiite mkopo, Waite msaada
 
Sorry, kabla hatujaingia ktk mjadala kama huu, tujiulize je serikali inapotoa pesa kama hii ya mkopo chanzo cha serikali ni nini?, jibu ni kodi. Kama ni kodi je mtoto wa private school mzazi wake halipi kodi?.
Kama chanzo ni kodi zetu...kuna watu tunalipa ma PAYE makubwa makubwa bado nikinunua bidhaa TRA hawa hapa sasa kwanini mwanangu asifaidi jasho la kodi yangu.??

Hii kitu ni time bomb labda kama zile kauli ni "mtazamo tu" ila kwa baadhi ya watendaji ambao wanafanya kazi kwa mizuka na kukurupuka tayari waneshajiandaa kutekeleza "agizo".
 
Umeongea point. Naamini huwezi kwenda Iringa kwa GF wako maana nasikia DAB sasa hivi kapotezewa na wadau wake hivyo nguvu zimemuishia kwa maana hiyo uko salama mdogo wangu.
 
Ila tuongee ukweli kama umeweza kulipa zaidi ya 2.5 kwa miaka 7 ongeza 4 ongeza 2 halafu leo 1.5 ya chuo itakushindaje miaka 3
Majibu ya maswali yako yapo kwenyr hayo maelezo ya Nondo, labda kama hutaki kuelewa!
 
Kwani huo si ni mkopo ambao mkopaji atarudisha baada ya kumaliza mazomo yake hivi mzazi yeyote mwenye uwezo wa kusomesha Mtoto wake atataka mtoto wake asome kwa mkopo tena wenye riba ya asilimia 6. Mi naona tunapenda kupotosha kwa kuwagawa Wanafunzi kwenye makundimakundi bila sababu ya msingi, kama kiasi kinachotengwa ni cha kukopesha wanafunzi wanaohitaji mkopo basi wote wenye Sifa ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu wakopeshwe kwa kigezo kuwa wameomba na wanasifa ya kusoma chuo kikuu hapo ndo watakuwa wamesaidiwa.
Mkuu umenena vema. Kweli ni mkopo siyo msaada. Na watatakiwa kurudisha. Sasa hii habari ya shule binafsi na za serikali sijui linatoka wapi!! Ninachoona hapa ni kwamba serikali haina pesa za kuwakopesha hao wanafunzi, hayo mengine ni porojo na kisiasa tu.
 
Ndio wakati wa kujifunza sasa Kuweka akiba kuanzia mtoto anazaliwaa
Hizo pesa ulizotaja ukumbuke humo unakuta kuna chakula, malazi, wengine shamba dress, material nk. Chuo ni gharama sana kulinganisha na secondary au primary. ni shule chache sana zenye gharama za juu. na ndo maana serikali haitoi bure inatoa mkopo na unarudishwa, ukitaka kuamini kuwa ni gharama ingia upractice, somesha.
 
Back
Top Bottom