A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

Mimi hapo penye red ndo panaponifanya nishangae sana juu ya hii skendo. Hata kwenye ile thread nyingine nilijikuta nashindwa kuamini kama serikali imehusika.

Swali langu ni kuwa "Ulimboka alitekwa peke yake, na baada ya kuokotwa alikuwa hana fahamu na hawezi kuongea. Je, haya yaliyomtokea kayasema nani?

Nimeuliza swali hili bado sijajibiwa mkuu
 
sawa mtoto wa mkulima na liwalo liwe, naapa kauli na matendo yenu jehanamu inawangoja
 
Hawezi huyu ni sisi wananchi kumuendea pale IKULU kumzaba vibao na kumuacha hoi kama walivyofanya wananchi wa MALI ndio ataondoka
 
Huyo Dr Ulimboka siyo COMANDO,atakuwa ni mla rushwa (CORRUPT) sana na inavyoonekana anaweza kuwauza wenzake.Nasema hivyo kwa sababu ukiiangalia hii incidence unaona kuwa huyu Dr Ulimboka ana tamaa ya pesa na anaendesha mgomo kwa kushawishi wenzake ili anufaike binafsi.Nasema hivyo kwa sababu hebu fikiria kwa akili ya kawaida tu,wewe una ishu kubwa kama hiyo ya mgomo,halagu unaitwa na mtu usiyemjua ili mkafanye reconcilliation na wewe unaenda tena peke yako!!!!.Bila shaka ni reconcilliation kuhusu mgomo.Hapo naona kuwa anaweza kuitwa na watu asiowajua na yeye akaenda tena peke yake!!!!.Baada ya hapo anaweza kuwageuka wenzake.HAFAI KABISA ANASUMBULIWA NA TAMAA NA NJAA TU.

Ng'wanambula one saa,ubhange ngika si,aliekuambia dr Ulimboka alikuwa peke yake ni nani,na aliekuambia alikwenda kukutana na watu asiemjua ni nani?fuatilia vizuri upate kuhabarika,
 
nchi hii inaongozwa na watu wa hovyo sana...anyway naamini kuna siku inakuja haya yataeleweka tu....
 
Wakati akipokelewa MOI tayari baadhi ya wanaharakati walishafika eneo lile said:

Yaani siipendi hii serikali na mambo yake yote! kama ndo hivyo inabidi awekewe ulinzi wa 24hrs maana wanaweza kurudi na kummaliza hata huko wodini..
 
Mama Heleni Kidjo bisimba mungu akujalie Kwa ujasiri ulionao kama Njelekela na Mwafongo aliadhibiwa kwa kuwa na watoto madawa ya kulevya wanaweza kukataa kutoa gari lakini wewe ukaweza kumsaidia tunakupongeza sana wewe ni Mwanamke jasiri wa Mfano nchii hii

JK aliwakejeli kuwa wanatofauti za kisiasa na walijiingiza kwenye mgomo wa madaktari basi aseme sasa. Tumeona kwamba wanaharakati ndo waliomwokoa Ulimboka ila serikali ilitaka kumtoa roho .Hongereni sana akina mama Bisimba ila mtumaini Mungu sana vita ndo imeanza nanyi mtaanza kuwindwa. Demokrasi imewashinda wanahofia kushindwa na wameanza udikteta ila sisi Mungu yuko upande wetu. aluta continua
 
Kama hali ni hii basi wananchi wote wake kwa waume kesho tuanze kukusanyika viwanja vya JANGWANI(TAHIR SQUARE) kuanzia saa 2 asubuhi ili kuilazimisha serikali iliyo madarakani kujiuzuru....Hii ni nchi yetu wote.

mimi simo. maana alipopigwa sheikh wangu mlisherehekea. kumbe tatizo sio la MMOJA?
 
Kwanza kabisa siungi mkono kwa jinsi iwayo yote matumizi ya nguvu kwa mwananchi wa kawaida kama Dr. Ulimboka. Yeyote aliyefanya ama kuruhusu haya kufanywa ni mtovu wa maadili na hapaswi kuwa uraiani - sehemu stahiki anayotakiwa kupelekwa ni segerea ama eneo jingine linalofanana na hilo. Ila bado nina utata kuhusu mazingira aliyokamatiwa Dr. Ulimboka. Walikuwa wanafanya nini kwenye hivi vikao vya usiku alivyokuwa akifanya na wenzake? Je vilikuwa vinahusu nini? Inakuwaje masuala ya mgomo wa madaktari yajadiliwe usiku wa manane kwani kwani yamekuwa uchawi?
 
Mkuu wa emergency dept anazuia gari kwenda kumchukua Daktari mwenzake aliyeokotwa akiwa hajitambui?
Aisee ndiyo maana migomo yenu haifanikiwi wakuu...

kutokutoa magari pengine ni sehemu ya mgomo who knows...
anyway,binafsi naamini ama mkuu wa kaya anahusika moja kwa moja katika hili au kuna watu wamefanya hili wakiwa ni maadui wa CCM na mkuu wa kaya ili kuidhihirisha ile dhana ya udhaifu wa serikali.
lakini katika yote serikali inatakiwa kwanza itoe tamko, pili ihakikishe wahusika wanatiwa nguvuni.
 
Kwa nini Jakaya bwana?! Wa kujiuzulu kwa hili ni Mizengo Pinda kwani yeye ndie aliyetoa public statement pale Muhimbili na hii ya leo bungeni ya LIWALO NA LIWE. mtoto wa mkulima kumbe muuaji, kweli umdhaniaye ndiye kumbe siye!

Nasema mimi kama mimi ningekuwa ni Jakaya basi hapa ndipo pa kuwaaga wa Tz ,na zaidi ikiwa hakuna mkono wake au hakushauriwa katika hili ,nafikiri tusubirini masaa tusikie kauli ya serikali ,hadi sasa TVbado hazijapata hii issue .
 
Mimi hapo penye red ndo panaponifanya nishangae sana juu ya hii skendo. Hata kwenye ile thread nyingine nilijikuta nashindwa kuamini kama serikali imehusika.

Swali langu ni kuwa "Ulimboka alitekwa peke yake, na baada ya kuokotwa alikuwa hana fahamu na hawezi kuongea. Je, haya yaliyomtokea kayasema nani?

Acha ujinga sasa hujui kama kapata nafuu baada ya first aid na kuanza kuongea? Au wewe naye ni mmoja wa wanaofuatilia au anapumua? Umeambiwa nafuu hakuna kabisa. Angalia picha zake amekaa mwenyewe acha upuuzi wako.
 
If they wanted him DEAD, he'd be dead by now, na mngekuwa mnaongea mambo mengine kabisa.......probably, they still need him for something..........the big question is wat is it??

and kimtazamo wangu, 1st, wat has bin done to him isnt fair, Unless, he(ulimboka) framed it....najua kwa hili, wengi mtanilaumu, but mkisoma stories nyingi kama hizi, mtaona, ulimboka hatokuwa wa kwanza, kufake something like this, but FOR GOOD REASONS..............cause, seriously, kama wangetaka afe, angekufa longtym........

2dnly, killing one person for the benefit of two or more people, i find it reasonable................

..and In my opinion, Spartacus should be the next to be slaughtered for the benefit of all ....what about that?
 
Nchi sasa inayumbayumba kama mlevi watawala wetu wamelewa mvinyo wa madaraka kwa pesa za walala hoi. fred Katulaunda wakondya mkaruka.
 
Last edited by a moderator:
Anaefuatia ni kiongozi wa chama cha walimu,Mh.Dhaifu kaamua kutumia nguvu!ktk mazingira kama haya Mh.Dhaifu anawajibika kwa hili
 
Sasa rais ajiuzulu kwa kipi hasa?

Mimi nadhani ingekuwa busara mheshimiwa kiongozi wa madaktari Dr Ulimboka ajiuzulu mara moja kwa sababu wakati anafanya mazungumzo na hao jamaa kama alizungumza nao kama mwakilishi wa madaktari bila kupata idhini ya chama cha madaktari ni makosa makubwa!!
wanapaswa kutoa huduma hospita ni ulimboka peke yake?hao ambao hawakutoa idhini wenye undugu na magamba wangeenda kutoa huyo huduma.umezuchanga kweli keo.mida ndo hiyo elekea jengo la kijani kamhudumie nape.
 
By Maundumula Sasa rais ajiuzulu kwa kipi hasa?

Mimi nadhani ingekuwa busara mheshimiwa kiongozi wa madaktari Dr Ulimboka ajiuzulu mara moja kwa sababu wakati anafanya mazungumzo na hao jamaa kama alizungumza nao kama mwakilishi wa madaktari bila kupata idhini ya chama cha madaktari ni makosa makubwa!!

:msela:SIYO KAULI YA BUSARA:llama:
 
Back
Top Bottom