Hatupo pamoja nawe kwa hili. Wala sikubaliani nawe.
Inawezekana kabisa maadui wa Dr. Uli wakajificha katika mgongo wa serikali ambaye pia ni adui wa madaktari wote. Lakini nikuulize swali moja, mkikosana na jirani yako na akakuambua kuwa 'leo utanitambua'. Jioni ukamwona katika kituo cha mafuta akinunua petroli wakati hana gari wala pikipiki na usiku huo nyumba yako ikaungua kwa moto. Neno liwalo na liwe likitumiwa na kiongozi mkubwa lina tafsiri nyingi mno ambazo zote zinakubalika na anaelewa kabisa uamuzi wowote utakaochukuliwa utakuwa na madhara aidha kwa serikali au kwa wananchi
Nonsense of the first order!!!!!!!!!!!!!!!!!
Of course..ikumbukwe kuwa kama "polisi njaa" wangetumika then kusingekuwa na coordination na uongozi wa polisi...Mfano alipopolekwa kituo cha polisi bunju Dr Uli hakupewa msaada wowote na kituo ilhali wakijua alikuwa amedhurika vibaya - hii inamaanisha tayari walikuwa na mwongozo kutoka juu kuwa wasihangaike kumpeleka hospitali. Pili, ukiangalia uongozi wa juu wa polisi na wizara ya mambo ya ndani inatetea huku wakijichanganya - hii inamaanisha uhusika wao hauna mashaka hata kidogo. Tatu, Polisi aliyepewa kibano pale Moi alisikika akiongea na Radiocall kuwa " Ulimboka kafikishwa MOI lakini bado yuko hai.....ikimaanisha kuna mpango uliokuwepo ambao walidhani angekuwa keshafariki hadi kufikia muda huo. kwa hiyo ni kuwa alikuwa anauarifu utawala kuwa jamaa bado hajafa. Yaani inasikitisha ila at the same time inaonesha jinsi ambavyo serikali ya tz haina akili hata kidogo na hasa baada ya JK aka (raisi mdhaifu) alipojipeleka hospitali kama kawaida yake na yale maneno yake ya kukariri" Serikali inampa pole dokta na tunamtakia kupona haraka na naomba madaktari wawe na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu" alafu huyoooo anasafiri leo nje ya nchi asikilizie soo kwa njia ya simu. Shame shame shame on the weak presida mwiba kura
Kwa staili ya uongozi wa JK, yeye binafsi sidhani kama anahusika, kwa kuwa watendajhi wake hukosa busara mara nyingi sana na kwa kuwa hana tabia ya kumlinda mtu, au kumpa mtu maelekezo ya nini cha kufanya, mpaka ashindwe ndio anaingilia kati (rejea swala la katiba, rejea mgomo uliopita vongozi wa kada mbalimbali waliropokwa wee mwinsho wakaumbulia na maamuzi na msimamo tofauti) Kuna Maswali muhimu ya kujiuliza ambayo yanasaidia kutafakari:
1. Je, haiwezekani ikawa ni chombo fulani cha dola au taasisi ya serikali (au kiongozi wake) kimeona kitengo chake kinadhalilishwa kwa kushindwa kuzuia vuguvugu hili na wanaona wajichukulie hatu wanazo ona wao ili kulinda kitengo na nafasi walizonazo? Hasa hasa ukizingatia watu wanavyopoteza kazi serikalini kwa kushindwa kusimamia maeneo yao ya kazi (yani hakuna garantee ya post uliyonayo). wako tayari hata kumshauri waziri mkuu vibaya kama walivyofanya kipindi kilichopita.
2. je kutokana na kuongezeka kwa uadui wa kisiasa (wa ndani au/na nje ya CCM), haiwezekani ikawa madui wametake advantage ya situation ku-set more fire? Na kuhakikisha wanafanya kitu ambacho kitaimarisha mgomo na kuifanya serikali ionekane dhaifu na inatumia mbinu chafu? Na hivyo kupelekea watu wa rika la kati (midle class) ambao ndio chachu hasa ya mapinduzi, ingawa sasa hawashiriki kikamilifu katika siasa kwani wako busy na uzalishaji mali.
3. Je watakuwa ni baadhi ya wale waliothiriwa kwa njia moja au nyingine na migomo hii?
Je hawadhani JK angependa busara itumike zaidi kuliko nguvu na maneno ya kejeli? Au kutaka kuonyesha mabavu kwa watu ambao serikali hii ni yao na si yenu nyinyi mlioko madarakani ambao ni dhamana tu mmepewa na haohao wanaolalamika?
Tunajua kuwa huu ndo upotoshaji mlioupanga kupindisha unyama huu. Mtajilaumu sana kwa kuwatuma wachakachuaji wa mafunzo kutekeleza mpango huu
Awali ya yote yatupasa kumpa pole na kumuombea apone haraka dakatari wetu huyu bwana Ulimboka na walaaniwe kwa nguvu zote wale wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine.
Wengi wetu kwa asilimia kubwa tumekuwa na imani kuwa, utekelezaji wa jambo hilo ni njama au mkakati wa serikali kupunguza kasi ya harakati za madaktari katika kudai haki zao.
Tunapoihusisha moja kwa moja serikali kwa upande mmoja wa mbele, hebu tugeuke nyuma na kuangalia upande wa pili.
Bila shaka Dk Ulimboka alikuwa na maadui wa hatari wenye chuki binafsi naye hasa kipindi cha vugu vugu hili la migomo ya madaktari. Kuna watu waliopoteza madaraka yao matamu kutokana na kadhia hii, upo uwezekano wa kupanga njama za kulipiza kisasi.
Kutumika polisi si kitu mbele ya pesa. Ukiwa na fungu la kutosha ukitaka kuwatumia polisi njaa kwa ajili ya uhalifu unawatumia bila shida. Ikiwa wapo ambao hufanya ujambazi na kupora mali za watu, itakuwa hawa wa kukodiwa! Tugawanye fikra na mitazamo yetu, wakati tunaitupia jicho la mashaka serikali.
Tuangalie na upande wa pili, wale waliomwaga unga kutokana na harakati hizi tunawachukuliaje? Hapa mhalifu halisi anaweza kujificha chini ya kivuli cha serikali.
Mwisho napenda niwapongeza madaktari wote waliotoa kichapo kwa mtu anayedhaniwa kuwa alikuwa mmoja wa wateka nyara.
Mungu msaidie Dk Ulimboka apone haraka ili aendelee na harakati zake.
Ndahani, hawsaaaa, ila kwa mchezo ninaouona, kunauwezekano watu wakaingia kwenye mtego sijui ni akina nani hasa watakaonasa, JK na Pinda wakienda vibaya imekula kwao, lazima swala la Uwajibikaji litawakumba... Sina uhakika kama Mh Pinda alivyoongea jana kwanye Bunge, kama tayari alikuwa ameshapata inteligence briefing ya kutosha ikihusisha swala la Ulimboka?? Na kama alikuwa anajua, ile kauli ni mafuta kwenye moto. Nawasihi wtumie na waonyeshe busara na hekima ya hali ya juu ndiyo silaha pekeee yakutatua matatizo yaliyopo sasa, haijalishi chanzoKwa vyovyote vile ilivyo, aliyeshika dola ndio ana wajibu wa kulinda mali na maisha ya wananchi wake. Ikishindikana kufanya huvyo lawama anabeba nani?
Hawsaaaa, ila kwa mchezo ninaouona, kunauwezekano watu wakaingia kwenye mtego sijui ni akina nani hasa watakaonasa, JK na Pinda wakienda vibaya imekula kwao, lazima swala la Uwajibikaji litawakumba... Sina uhakika kama Mh Pinda alivyoongea jana kwanye Bunge, kama tayari alikuwa ameshapata inteligence briefing ya kutosha ikihusisha swala la Ulimboka?? Na kama alikuwa anajua, ile kauli ni mafuta kwenye moto. Nawasihi wtumie na waonyeshe busara na hekima ya hali ya juu ndiyo silaha pekeee yakutatua matatizo yaliyopo sasa, haijalishi chanzo
Nijuavyo mimi katika hali ile regardless who it was Kituo cha Tegeta as a matter of procedure walitakiwa wampeleke hospitali. Cha kushangaza tunaona Mwanaharakati wa haki za binadamu ndo aliyekwenda kumpeleka hospitali
Pia kuhusika kwa mtu toka ikulu
Pia state propaganda machinery TV ya taifa haikucover hiyo story
Pia kauli ya Pinda before and after the incident
Kabla hatujaja huku Ughaibuni tulisha fanya kazi ndani ya serikali na mashirika yake.
Hatujazaliwa jana we know very well how CCM government operates.
Ili uwe mtendaji bora wa serikali ya CCM ni lazima uwe Schizophrenia, hawa ni watu ambao brain yao haina sense ya emotion. Hawa ni watu ambao wanaweza kula hata ndani ya choo cha City kwa sababu halufu ya mavi haiwasumbui.
Hawa ni watu wanao weza kuua mtu kwa kumwonea wivu kavaa shati jipya.
Hawa ni watu tangu enzi za form one ni kulilia umonita darasani na ukiranja ili kila siku wafaidi kuona mtu akilamba viboko kwa unaa wao.
Hawa ni watu ambao mkifanya biashara ya ubia na kupata faida millioni moja utakuwa na bahati sana akikupa 100,000 katika millioni.
Serikali dharimu siku zote hupenda kuajiri watu kama hawa katika kazi ambazo huhitaji aina fulani ya unyama.
Uchunguzi hapa Marekani umeonyesha Scizophrenic wengi wanafanya kazi Wall Street na wengi ni Ma CEO wa makapuni yanayopata faida kwa kufanya kila unyama hapa duniani.
Kifupi ni kwamba serikali ya CCM inaongozwa na wagonjwa wa akili.
Ukiwasikia kwenye mazungumzo yao ya faragha utashangaa. Hawana ubinadamu hata unyama hawana wana Uibilisi tu.
Unajua hata Fisi hawezi kupanga njama ya kumla Fisi mwenza lakini ukiwa ndani ya serikali ya CCM mazungumzo ya kuua watu wanaowavurugia mlo wao haramu ni ya kawaida tu.
Ndiyo maana watumishi wengi wa serikali ya CCM wakisha staafu hali yao huanza kuwa duni ndani ya masaa 24 tu ni wagonjwa wa akili bila kufanya unyama maisha yao hayaendi.
Hili changa la macho la kujifanya eti kuna watu wenye hasira ni upuuzi wenye utepetevu wa akili na nia mahususi ya kulinda maovu ya serikali ya CCM. Ushawishi huu duni hauna uhusiano na kitu mna ita Looking Ouside the Box. Msemo umetumiwa kimaharamia na si mahali pake.
Dozi ya ujinga ambayo Ideology ya CCM imewabugiza watanzania ilikuwa kubwa sana, Mungu bariki mwananchi mmoja mmoja anaamka na kutambua uovu wa serikali hii dharimu. Uongo wa karne ya 20 hauwezi fua dafu karne ya 21. Uongo mahali pake ni kwenye mikutani ya NEC kwa akina Mamvi Richmonduli.