A Call For A Palace Coup: CHADEMA

..ukiwakutanisha ktk majukwaa ya siasa sioni kama kuna anayemzidi mwenzake.

..kuna kipindi ilikuwa unaona ccm wamewazidi wenzao kwa hoja za kisomi na zenye upeo. sasa hivi ile GAP haiko tena.

..kilichobadilika sasa ni CCM kutumia vyombo vya DOLA. Wenzao wakiwa challenge kwa hoja za kisiasa CCM wanatumia vyombo vya dola kuwadhibiti.

..CCM iko juu ya sheria.
Naam, huu ndo ukweli
 
Write your reply...hahahahaa ni muda wakina Nauye January Mwigulu kuja tupate nao tabu huku hekaluni kipigo cha mbwa koko kimtoke katambi kende kwa Nape
 
My advice:Chadema wasishiriki uchaguzi wowote from now on na hule wa 2020 mpaka aidha katiba mpya ipitishwe au kuwe na level playing field kwenye siasa na tume kuwa huru.
Wasiposhiriki uchaguzi chama kitakosa ruzuku, hayo madeni hewa ya mbowe yatalipwaje?
 
Nyani Ngabu I may differ with you from your notion that there's a crisis in CHADEMA causing all this turnover of politicans from opposition to the ruling party.... It's quite disappointing that none of your views have based on the fact that democracy has deteriorated in our country no freedom of speech,neither freedom of press,banned political rallies and gatherings to say a few

All this reasons demoralise opposition members and foresee no hope of surviving come 2020 elections hence seek assurance of their political survival by crossing the divide.... The problem is not CHADEMA or Mbowe it's the entire political environment which has been jeopardised by a dictator. Just ask yourself how can CHADEMA or ACT grow without political rallies,gatherings and press freedom?? Remember how M4Cs and Operation sangara made CHADEMA a political giant and a force to reckon with.

Please and please Tanzanians let's not blame the shadows and leave the object standing..... We know who's behind all this but we still can't raise our fingers on him!!! like seriously we should not be even arguing if mbowe should go or stay while no matter who comes whether lissu or albanie or heche will still face the same situation and nothing will change for CHADEMA because we are not solving the problem from it's roots.

Shida ni magogoni mkuu sio ufipa
Ni maoni tu

Cc chige JokaKuu Malcom Lumumba
Mbowe ameshindwa mbinu..huo ndio ukweli siasa zimemshinda...Yaani Chadema mnategemea kuendesha chama kwa kutegemea huruma ya serikali..maajabu haya..Lisu amepigwa risasi, Ben amepotea chama kimefanya nini?... Mnategemea serikali ndio imtafute Ben Saanane? Chadema hamna intelligencia? .....Mmeshindwa hata kukodisha Private Investigator kuchunguza Lisu kupigwa risasi? eti mnategemea serikali are you seriuos????.......Endeleeni kutegemea serikali wakati chama kinateketea....simameni wenyewe bila kutegemea huruma.....Serikali imeshaonesha haina ushirikiano na nyie so why mnaing'ang'ania iwasaidie?..... Kila siku ni kulia lia tu kuibiwa kura, kuzuiwa mikutano, kukamatwa lakini hakuna hatua yoyot mnayochukua..Pathetic!!!!! Nendeni Kenya mkajifunze siasa za upinzan zinavyofanywa
 
Kuna sura mbili la suala hili kwa mtazamo wangu

1. Kwamba, Mbowe ajiuzulu kwa wengine ni geni na linachagizwa na hili la kujiuzulu Wabunge. Kwa baadhi tuliongelea siku nyingi sana.

Sababu kubwa ilikuwa ni kushindwa kutafuta majawabu sahihi ya upinzania kutofanya vizuri
Tulisema siku Kikwete alipotangaza kuundwa tume ya katiba na Mbowe kuunga mkono

Niliandika hivi, baada ya kushindwa kutafuta suluhu ya matatizo ndani ya CDM, haikuwa sahihi kwa Mbowe kuunga mkono Mwenyekiti wa CCM kuunda tume ya kubadili katiba

Tatizo ni katiba inayotengeneza mazingira ya wapinzani kufanya vibaya

Mbowe hakuonekana kutambua mwarobani ni kuwa na tume isiyowajibika kwa CCM kwani mchakatto mzima utatekwa. Leo tunajua Polepole na wenzake walikuwa 'wahujumu'

2. Kama watu wanatumia kigezo cha kuhama ndiko kushindwa kwa Mbowe ni makosa.

Kuna ahadi ya kufuta upinzani iliyotolewa kama amri. Watu kama Lissu bei yao haijulikani
Hawa wanaonunuliwa ni 'business' siyo suala la demokrasia bla blah

Yule Mbunge wa Hai, Daktari alirudi CCM na kurudi bungeni hapo hapo. ''Incident''
Mbunge wa Kinondoni alirudi CCM na kurudi Bungeni hapo hapo 'coincidence'
Mbunge wa Ukonga ukonga ahamia CCM na atarudi bungeni ' Pattern'

One's an incident , two's is a coincidence, three's a pattern
Hii pattern inakutana na tukio jingine la kutangaza waliojitosa kupewa nyadhifa(RC,DC,Tawala)

Kuna 'insurance' kwamba usipokuwa mbunge, utapata u-DC. Muulize Katambi na Kafulila

Sanduku la kura lili ibwa, likarudishwa na hakuna aliyeshtuka, kuanzia Polisi, tume, Msajili etc
Mkimlaumu Mbowe ni kumtwisha zigo, anachopaswa kufanya ni kujiuliza kuna jipya alilobakiza?

Halafu nanyi wananchi mjiulize mnakwenda wapi? vyama vingi au chama kushika hatamu

How do you rate Mbowe as a leader?
 
Watz waache unafiki? Kabla hujatutusi watz wote unapaswa tambua hatufanani kimawazo, fikra, maamuzi etc.
Sasa baki hapo ukiwaza ulitakalo lifanywe na watu wote.
Akili fupi hizi ndio hunifanya niwachukie sana wapinzani wa bongo.
basi watanzania wasiache unafiki! umefurahi
 
How do you rate Mbowe as a leader?
Nyani , it's difficult to rate him by fixed quantity

Kama kiongozi amekitoa chama cha tatu kwa upinzani kuwa chama kikuu cha upinzani, kudos
Ameweza kukisimamisha at the the time of trial and tribulations.
NCCR and CUF could not withstand. As a leader he has endured a lot

Kwa upande mwingine ni mtu anayeongoza kwa 'acquired skills siyo embedded leadership traits

Mbowe ameongoza chaguzi zaidi ya tatu bila matokeo ya kuridhisha. Arguably wapo wanaosema kuna ongezeko la Wabunge na madiwani. Wapo sahihi, lakini je wanafikiri nini kuhusu muda?

Mbowe asilaumiwe kwasababu mfumo wetu ambao sanduku la kura linachukuliwa kituoni na kurudishwa bila chombo chochote kushtuka, ni aghalabu kuna kushinda kwa aliye nje ya mfumo

Katika mazingira hayo, kuna haja ya kuwa na maono tofauti. Kilichopo ni 'insane' so to speak
Hapa ndipo alaumiwe, kwa kukumbatia insanity!

Wakati akiwa kwenye peak kulikuwa na pressure ya katiba, ambayo ingekuwa jawabu kwa sehemu kubwa ya matatizo ya chaguzi, siyo absolute but by far

Mbowe akakubali kirahisi uundwaji wa tume na chama kile kile kinachonufaika na mfumo uliopo
Alikuwa na mass support ambayo ingempa leverage na si kumuunga mkono JK kirahisi tu
Katika wakati ule , alipaswa kukataa ili kuwepo na 'uwanja sawa' utakao sawazisha hali

CCM wakatumia Bunge kuvuruga mchakato makusudi na Upinzani wakarudi square one

Pili, lengo la chama cha siasa ni kuchukua uongozi wa nchi. Kuna taratibu za mkato na za mbinu

Kwa sheria za nchi yetu njia za mkato ni chaguzi ambazo zimefeli.
Njia za mbinu ilikuwa ni upinzani uwe na wabunge wa kutosha. Mbowe hakuona hilo

Nguvu nyingi zikaelekezwa kwa kupokea wahamiaji na personality akiwa kiongozi
Hata kama mgombea asingeshinda,ni wazi asingeshinda, kulikuwa na uwezekano wa kuwa na wabunge wengi wa upinzani. Mabadiliko katikati ya uchaguzi ilikuwa kosa la kifundi, alishiriki

Makosa ya kutokuwa na vyombo huru yameendelea kuwagharimu Wapinzani
Mfano, kwanini walisusia uchaguzi wa Singida-Nyalandu, wakashiriki wa Kinondoni na Siha.
Busara zipi zilitumika. Utaona ombwe la uongozi na kukosekana kwa dira ya nini kifanyike

Chama kinapopita katika misuko suko kuna ulazima wa kufanya 'reform' kuona kama kuna wenye mbinu tofauti. Reform inaongozwa na uchaguzi ili kupata mandate

Baada ya chaguzi nyingi kupita nadhani CDM wana uwezo wa kujua kama kuna haja ya mabadiliko au la. Mbowe hajatumia busara kubaini hilo

Kwa vile mandate ya wanachama haionekani ni rahisi kwake kutuhumiwa
Kila anayenunuliwa hoja yake kubwa ni hiyo. Hivyo, anawapa hoja kwa gharama ya chama

Sasa nikijibu swali lako naweza kusema kuna 'ambivalence' kwa kutazama uongozi wake
Ni ngumu kumpa fixed quantity kwasababu kuna so many variables, kwa mfano, yeye kama kiongozi, busara na hekma, wananchi kwa ujumla, wapinzani,vision , mifumo ya vyama n.k.

CDM wanachoweza kufanya ni kuwa na uchaguzi wa reform ya uongozi.
Hii haina maana ya kumuondoa, kama atapewa mandate haina tatizo.

Yeye kama kiongozi anaweza kujipima kama bado ana kitu cha kufanya au ni wakati wa kutoa kijiti kwa wengine. Hilo ni baina yake na wanachama wao
 
Last edited:
Nyani , it's difficult to rate him by fixed quantity

Kama kiongozi amekitoa chama cha tatu kwa upinzani kuwa chama kikuu cha upinzani, kudos
Ameweza kukisimiamisha at the the time of trial and tribulations.
NCCR and CUF could not withstand. As a leader he has endured a lot

Kwa upande mwingine ni mtu anayeongoza kwa 'acquired skills siyo embedded leadership traits

Mbowe ameongoza chaguzi zaidi ya tatu bila matokeo ya kuridhisha. Arguably wapo wanaosema kuna ongezeko la Wabunge na madiwani. Wapo sahihi, lakini je wanafikiri nini kuhusu muda?

Mbowe asilaumiwe kwasababu mfumo wetu ambao sanduku la kura linachukuliwa kituoni na kurudishwa bila chombo chochote kushtuka, ni aghalabu kuna kushinda kwa aliye nje ya mfumo

Katika mazingira hayo, kuna haja ya kuwa na maono tofauti. Kilichopo ni 'insane' so to speak
Hapa ndipo alaumiwe, kwa kukumbatia insanity!

Wakati akiwa kwenye peak kulikuwa na pressure ya katiba, ambayo ingekuwa jawabu kwa sehemu kubwa ya matatizo ya chaguzi, siyo absolute but by far

Mbowe akakubali kirahisi uundwaji wa tume na chama kile kile kinachonufaika na mfumo uliopo
Alikuwa na mass support ambayo ingempa leverage na si kumuunga mkono JK kirahisi tu
Katika wakati ule , alipaswa kukataa ili kuwepo na 'uwanja sawa' utakao sawazisha hali

CCM wakatumia Bunge kuvuruga mchakato makusudi na Upinzani wakarudi square one

Pili, lengo la chama cha siasa ni kuchukua uongozi wa nchi. Kuna taratibu za mkato na za mbinu

Kwa sheria za nchi yetu njia za mkato ni chaguzi ambazo zimefeli.
Njia za mbinu ilikuwa ni upinzani uwe na wabunge wa kutosha. Mbowe hakuona hilo

Nguvu nyingi zikaelekezwa kwa kupokea wahamiaji na personality akiwa kiongozi
Hata kama mgombea asingeshinda,ni wazi asingeshinda, kulikuwa na uwezekano wa kuwa na wabunge wengi wa upinzani. Mabadiliko katikati ya uchaguzi ilikuwa kosa la kifundi, alishiriki

Makosa ya kutokuwa na vyombo huru yameendelea kuwagharimu Wapinzani
Mfano, kwanini walisusia uchaguzi wa Singida-Nyalandu, wakashiriki wa Kinondoni na Siha.
Busara zipi zilitumika. Utaona ombwe la uongozi na kukosekana kwa dira ya nini kifanyike

Chama kinapopita katika misuko suko kuna ulazima wa kufanya 'reform' kuona kama kuna wenye mbinu tofauti. Reform inaongozwa na uchaguzi ili kupata mandate

Baada ya chaguzi nyingi kupita nadhani CDM wana uwezo wa kujua kama kuna haja ya mabadiliko au la. Mbowe hajatumia busara kubaini hilo

Kwa vile mandate ya wanachama haionekani ni rahisi kwake kutuhumiwa
Kila anayenunuliwa hoja yake kubwa ni hiyo. Hivyo, anawapa hoja kwa gharama ya chama

Sasa nikijibu swali lako naweza kusema kuna 'ambivalence' kwa kutazama uongozi wake
Ni ngumu kumpa fixed quantity kwasababu kuna so many variables, kwa mfano, yeye kama kiongozi, busara na hekma, wananchi kwa ujumla, wapinzani,vision , mifumo ya vyama n.k.

CDM wanachoweza kufanya ni kuwa na uchaguzi wa reform ya uongozi.
Hii haina maana ya kumuondoa, kama atapewa mandate haina tatizo.

Yeye kama kiongozi anaweza kujipima kama bado ana kitu cha kufanya au ni wakati wa kutoa kijiti kwa wengine. Hilo ni baina yake na wanachama wao

This is the type of disquisition that I appreciate.

There’s nothing else for me to add.

Thanks man!
 
Tujiandae tu kisaikolojia upinzani kufa,hata ungemuweka malaika ktk uenyekiti wa cdm sidhani kama ataweza kupambana na huyu mkulu Watanzania bado kufikia level ya kukataa cheo endapo ukiahidiwa tena na mwenye nchi,ngoja tusubiri labda wajukuu zetu wataweza
You are wrong. Haisaidii kusingizia jirani katika matatizo ya nyumbani kwako. Reforms are badly needed ndani ya chama chenu
..ccm wakitukana wanaachwa.

..cdm wakitukana wanakamatwa.

..vyama hivi viachwe vipambane kwa hoja na polisi na dola wasiingilie humo.

..wewe umeona demokrasia gani iliyostaarabika maandamano ya kiongozi mkuu wa upinzani yakasambaratishwa kwa risasi za moto kama inavyotokea hapa Tz?

..mpaka ifikie kiongozi wa upinzani analazimika kuandamana kwa kudai haki zake serekalini na kwa chama tawala ujue kuna tatizo kubwa sana la kiuelewa na kimtizamo kwa hao anaowalalamikia.

..Wabunge wa upinzani wanafungwa kwa kesi za kisiasa. Hivi kwenye nchi za wenzetu waliostaarabika Peter Lijualikali angefungwa na kutumikishwa kwa kazi ngumu?

..Hoja yangu ni DOLA needs to change kulingana na mazingira mapya ya mfumo wa vyama vingi.

..Tutendeane HAKI. Is that too much to ask?

NB.

..Majaji Wakuu Wastaafu wanasema mbele ya Raisi HAKI ITENDEKE. Unadhani yale ni mambo wanazusha tu? Raisi gani mwingine wa Tz umewahi kusikia anaambiwa atende HAKI?

Cc Richard
In other words, hayo mazingira ya usawa yakiwepo basi Mbowe is irreplaceable. Ubadhirifu wa ruzuku ndani ya chama utakwisha. Ofisi kuu za chama zitajijenga. Yeah, bado kuna safari ndefu.
 
Afrika ndivyo tulivyo mkuu hio ndio "style" ya uongozi na siasa za Afrika ambazo mpaka leo zinamchanganya mtu asie mwafrika.

Kama wafahamu, Jumatatu kuna uchaguzi huko Zimbabwe, Emerson Mnangagwa wa ZANU -PF na Nelson Chamisa wa MDC tayari leo wamemaliza kampeni za uchaguzi.

Huu utakuwa uchaguzi wa kwanza wa maana tangia mwaka 2000 na Mnangagwa mwenye umri wa miaka 75 anapambana na Chamisa mwenye umri wa miaka 40.

Mnangagwa anawakilisha wazee wote wenye umri zaidi ya miaka 40, wakti Chamisa anawakilisha vijana wote kuanzia miaka 40 kwenda chini.

Pia Mnangagwa ana anatumia rasilimali za nchi kama vile magari ya kufanyia kampeni, mabango makubwa ambayo yanaonyesha sura yake kila kona nchini humo na hata muda wa kutosha kwenye runinga za nchi hiyo.

We fikiria wabunge wote 300 wa ZANU-PF wamepewa magari wazunguke nayo kufanya kampeni unadhani fedha yote hiyo ingekuwepo kama ZANU -PF wangekuwa ndiyo wapinzani?

Nelson Chamisa yeye anachagua wapi pa kufanyia kampeni na sanasana anazunguka Harare na vitongoji vyake na siyo nchi nzima.

Nimetoa mfano huo wa Zimbabwe kutaka kuonyesha jinsi vyama vya upinzani au chama kikuu cha upinzani kisivyoweza kubuni njia mbadala za kupata nafasi ya kuwa na wabunge wengi bungeni kuwazidi wale wa chama tawala.

Hiyo ndiyo silaha ya upinzani, kufanya kampeni kuhakikisha wanapata wabunge wengi ambao wataweza kuwadhibiti9 wale wabunge wa chama tawala.

Lakini hii si kazi rahisi inahitaji muda, fedha (za kwenu na si za ruzuku) rasilimali watu wenye maoni na mawazo chanya yasiyo na taama ya uongozi na uelevu.

Kushindwa huko kupata aina hii ya upinzani ndiko kunaleta kelele zote hizo za kwamba wapinzani wanaonewa na kadhalika.

Lakini pia kiongozi wa upinzani anapoona mambo si mazuri anakaa pembeni kupisha mawazo mbadala ili kukinusuru chama.

Pengine kiongozi mpya atakuja na mbinu mbadala za kukabiliana na chama tawala.
Umesahau kusema kwamba Comrade Robert Mugabe siyo kijana lakini ametangaza wazi kwamba atampigia kura Chamisa.
 
kama chadema ni mbaya kwanini waliyowahi kuktumikia chama hicho wanapata uteuzi????
Jibu la s wali lako:
These are young men and women wameonyesha wana leadership skills za kutekeleza agenda za uchaguzi za CCM - chama tawala. That's, kuwaletea maendeleo wananchi, hasa wanyonge. Hicho ndicho chama kilichopewa ridhaa ya kuongoza kupitia uchaguzi mkuu. Any other question?
 
Wapinzani kwa sasa ni kama kondoo mbele ya simba.hata mwenyekiti awe nape nnauye au mwigulu nchemba hakuna wa kufurukuta mbele ya chuma cha pua Mh.Magufuli.
Ukileta pua wasiojulikana wapo kukudhibiti. Nawapa pole sana. Hata anaesema kunahitajika damu mpya atakuwa katumwa na wasiojulikana.
Huwezi kukabidhi mtu mpya uongozi katika kipindi kama hiki ambapo hata risasi zinatumika, na ahadi za vyeo ziko mbele
 
Mkara-tu, post: 27765988, member: 482919"]You are wrong. Haisaidii kusingizia jirani katika matatizo ya nyumbani kwako. Reforms are badly needed ndani ya chama chenu
Sidhani kama unamwelewa JokaKuu . Anachosema ni kuwa haki ya vyama kufanya shughuli za siasa ni ya kikatiba bila kujali nini kipo ndani ya vyama hivyo
NCCR na CUF vilikuwa na migogoro iliyopapalia kustawi kwa CDM. Chadema nao wakao na mgogoro uliozaa ACT. Na hata CCM walikuwa na mgogoro uliozaa wahamiaji

Yote hayo ni matatizo ndani ya vyama na hakuna chama 'pristine'
Si jukumu la dola kuangalia mienendo ya vyama hivyo. Ni jukumu la dola kujenga mazingira ya vyama kushirikia katika siasa bila bughudha wala uonevu

Ametoa mfano wa Lijua likali, na niongeze kidogo tu. Adhabu ya kosa la Sugu ukilinganisha na na kosa la rushwa waliloeleza Lema na Nassari utaona tatizo.
Kosa la rushwa likamlizwa katika mazingira ya kushangaza, kwamba limetangazwa na la kisiasa

Juzi waziri wa zamani ambaye ni mbunge alikuwa Buyungu akifanya kampeni.
Wakati huo huo kuna marufuku kutofanya mikutano nje ya maeneo yao. Haki ipo wapi?
In other words, hayo mazingira ya usawa yakiwepo basi Mbowe is irreplaceable. Ubadhirifu wa ruzuku ndani ya chama utakwisha. Ofisi kuu za chama zitajijenga. Yeah, bado kuna safari ndefu.
Mambo ya vyama yanabaki kuwa ya vyama si ya kitaifa.
Haki ya kufanya mikutano imeanishwa katika sheria za nchi , ni ya kitaifa. Usichanganye hivi vitu

Ubadhirifu wa ruzuku unaweza kushughulikiwa kichama au kisheria ikibidi.
Kujenga ofisi ni suala la chama si la taifa.
Hayo yote hayaondoi haki ya mikutano au ushiriki wa siasa za nchi au kujenga ushindani katika usawa.
 
Jibu la s wali lako:
These are young men and women wameonyesha wana leadership skills za kutekeleza agenda za uchaguzi za CCM - chama tawala. That's, kuwaletea maendeleo wananchi, hasa wanyonge. Hicho ndicho chama kilichopewa ridhaa ya kuongoza kupitia uchaguzi mkuu. Any other question?
Hapa nichangie kidogo kuhusu dhana ya kuwaletea maendeleo watu

Hakuna kitu kinachoitwa kuleta maendeleo kwa watu. Hakuna kiongozi anayebeba kontena la maendeleo na kulitua mahali. Hakuna kiongozi anayeleta maendeleo peke yake

Maendeleo ni dhana shirikishi ya umma viongozi wakiwa ni viungo tu na si maendeleo yenyewe
Kauli hii inatumiwa na watu katika kuhalalisha uwepo wao kisiasa kinyume na maana halisi

Kuhusu ridhaa (mandate) hilo si hoja kubwa, hoja ni kuwa process ya kupata mandate ilikuwa legit? au ni suala la 'the end justifies the means'?
 
"JokaKuu, post: 27750933, member: 221"]..If I am not mistaken he was elected in 2003.
..the term limits clause was removed to allow him to be eligible for re election.
Hapa ndipo busara za uongozi zilipokosekana kama nilivyojadiliana na Nyani Ngabu awali
1. hiyo clause ilizaa 'waraka' wa Kitila na Zitto. Baada ya hali kutulia Mbowe alitakiwa afanye mambo mawili (a) aitishe mkutano kua affirm clause as it is to avert any unforeseeable crisis
or (b) restore the original clause. Hakufanya lolote
2. Clause ilimpa fursa ya re-election, the question, lini ulifanyika uchaguzi akapata mandate kutokana na advantage ya clause? Clause iliondoa term limits na siyo election
..But I think Mbowe should be step aside so as to infuse new style and ideas into the party.
I think he deserves a fair share of democratic process.
He could seek the mandate in free and fair election. In the end,voters must have the final say
Hili litasaidia kuondoa dhana ya coup de tat inayoweza kuacha makovu

Hoja yangu inabaki kuwa uitishwe uchaguzi. Mbowe ana haki ya kugombea kama mwanachama
Haki ya kama anataka kuendelea au anaona haja ya ku'infuse new style and ideas' kutoka kwingine, yeye ajipime bila kuathiri haki yake ya ya kidemokrasia.

Wanachama wapitie clause na kuona kama kuna sababu za marekebisho.
Wakitaka term limits hata qualify. Wakiacha kama ilivyo ni haki yao kwa kutazama mstakabali wa chama chao

Tahadhari, watu au CDM wasichanganye hoja za madiwani na Wabunge na uongozi wa Mbowe
Hakuna anayeweza kuzuia biashara inayoendelea watu wakijua ushahidi wa Lema na Nassari haukuweza kusaidia. Si Msajili, si PCCB au Tume vilivyoweza kuthubutu!
CCM wanaweza!

Watu wajadili uongozi na Mbowe on political landscape
 
Last edited:
I think he deserves a fair share of democratic process.
He could seek the mandate in free and fair election. In the end,voters must have the final say
Hili litasaidia kuondoa dhana ya coup de tat inayoweza kuacha makovu

If he runs and loses, it will look bad on him.

Best option would be for him to step aside/ resign and leave the seat open for others to vie for.

That way he'll have an 'honorable' exit rather than get defeated by a vote.

He has held the position for far too long. He can voluntarily give it up and let someone else steer the ship.
 
Last edited:
Back
Top Bottom