Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,131
- 35,164
Ukifika Zanzibar na kujitambulisha wewe ni mhubiri au muumini thabiti wa dini fulani (tofauti na dini inayotawala zaidi pale Zanzibar) umekuja kwa shughuli ya kueneza habari njema kwa watu wote, unaweza usipewe hata nyumba ya kulala wageni haijarishi una pesa kiasi gani mfukoni. Lakini ukisema wewe ni mgeni/mtalii umekuja kuponda raha zote safi na chafu basi kwa haraka sana utauziwa kila kitu unachokitaka kuanzia pombe, ngono mpaka madawa ya kulevya. Cha kushangaza sana waratibu wa hayo yote ni washika dini wazuri.
Hutasikia danguro likichomwa moto wala klabu ya pombe ikivunjwa Zanzibar. Mpaka sasa hakuna kumbukumbu zozote za wazi zinazoonyesha teja, mlevi, malaya au shoga kupigwa, kuteswa au kuuawa Zanzibar, lakini kuna kumbukumbu za wazi za viongozi au waumini wa dini fulani kuuawa, kupigwa, kunyanyaswa na kuteswa huku mali zao zikiharibiwa.
Kuna kitu bado sijakielewa vizuri Zanzibar. Nadhani pia Zanzibar inapaswa ibadilishe mitazamo yake.
Hutasikia danguro likichomwa moto wala klabu ya pombe ikivunjwa Zanzibar. Mpaka sasa hakuna kumbukumbu zozote za wazi zinazoonyesha teja, mlevi, malaya au shoga kupigwa, kuteswa au kuuawa Zanzibar, lakini kuna kumbukumbu za wazi za viongozi au waumini wa dini fulani kuuawa, kupigwa, kunyanyaswa na kuteswa huku mali zao zikiharibiwa.
Kuna kitu bado sijakielewa vizuri Zanzibar. Nadhani pia Zanzibar inapaswa ibadilishe mitazamo yake.