sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Huyu alikulia hood mitaa iliyojaa msoto, uhalifu na umasikini, wazazi wake walikuwa kundi la black oanthers wanaharakati wa kupigania haki za wamarekani weusi, ni kundi lililokuwa likisakwa kila kukicha na serikali ,mama yake pekee alikuwa na kesi kama 50 zs uchochezi, kalelewa na ndugu tofauti tofauti ambao nao walikuwa black panthers maana baba yake hakuwepo na mama yake stress zilimsomba aingie kwenye madawa, hata ndugu alioishi nao wengi walipewa kesi za kufungwa jela, hali ya kukulia haya maisha nae alibeba vitu kwenye suala la kuwa mtetezi wa haki.
Tofauti na rappers wengi, 2 pac alipenda sana kujisomea vitabu kuongeza maarifa, kajisomea vitabu zaidi ya 70 !! Shuleni alipenda zaidi kujifunza masomo ya sanaa kwenye uandishi wa mashairi (poetry) na uigizaji,
2pac aliweza kufanya kazi kibao kudai haki, kuelimisha jamii, kutoa postive motivation, n.k. ilikuwa ni ndani ya damu yake kwa maisha aliyopitia na watu waliomkuza, waweza kumsikilizisha hata mtoto wako baadhi ya nyimbo zake apate cha kujifunza.
Changes ilikuwa kazi ya kiharakati kutetea haki za mtu mweusi, kukemea ubaguzi na kuhamasisha umoja wa watu weusi.
Dear mama ilitoa fundisho kuwa mama ni mama tu hata akiwa na mapungufu yake (mama yake alikuwa teja)
Only God can judge me alitoa ujumbe maridhawa kwamba ni Mungu pekee wa kumhukumu kikamilifu,
Brenda got a baby ilikemea mimba za utotoni.
A letter to my unborn child anatoa ramani kwa mtoto anaezaliwa kuwa mmarekani mweusi kwa magumu inayobidi ajiandae kuyapitia pamoja na kuwaasa waepukane na maisha ya usela ili kuepukana na hatari za kwenda jela ama kufa.
Keep ya head high ni bonge la postive inspiration kujua thamani yako.
Wonder why they call you bitch ilitoa darasa kwa dada zetu tabia za kujiepusha ili wasijishushe thamani.
2pac nae alikuwa muhuni japo ilikuwa ni mpaka umchokonoe, Biggie aliwahi kumtesti kilochotokea 2pac alimchapia dem wake na kumtolea diss track iliyovunja rekodi - hit em up.
hizo ni chache tu.........
Ukija kwa Notorious Big, kwanza kabisa anadanganya kwamba aliishi maisha magumu wakati kiuhalisia hakulelewa maisha ya kitajiri ila sio haba aliishi maisha walau ya kati, mama yake alikuwa na kazi ya ualimu, Big alisomeshwa shule private, aliishi mitaa yenye hadhi ya wastan hakuishi hood kama 2pac, n.k. hali yake ilimpa wepesi kujuana na kina pdiddy, mama yake alikuwa anachukia sana kamlea vizuri ila yeye anadanganya kakulia kwenye shida
Big nyimbo kibao kajivika uhusika wa jina lake kuwa mkatoli asie na huruma (Notorious) pamoja na kujibrand zaidi zaidi kama muuza madawa ya kulevya.
anaimba kubrag (kujisifia) ana mkwanja, kuua, kupora, kupiga, n.k. sambamba na kudanganya kwamba aliishi magumu sana, aliacha shule akiwa na miaka kumi, n.k.
Big ufalme wake upo kwenye ku flow kama maji, kwakweli flow zake zina ladha tamu masikioni hata kama hujui lugha una enjoy kusikiliza, kumbuka shuleni alifanya vizuri zaidi somo la kiingereza huenda hii ilisaidia kujua kupanga maneno kwenye flow zake, kazi zake kama ten crack commandments anafundisha namna ya kuuza madawa lakini anavyo flow kama maji waweza kuweka kando ujumbe wake ujikite na flow yake, kazi nyingine kama big poppa kaimba pombe na milupo lakini huchoki kumsikiliza anavyo flow kama maji, aliwahi pia kufanya kazi na eminem - dead wrong kwa hakika aliflow kama maji japo ujumbe wake ni kubaka, kuwapora wanawake, kupiga wanamke na kuua kikatili.
Wayakuja watu kusema kazi zake za juicy na sky is the limit zina ujumbe, huo ujumbe ni upi ?
Juicy kaweka wazi mafanikio aliyopata kwenye mziki yamempa mkwanja wa kufanya umalaya na kupiga pamba kali, sioni cha kuelimisha hapo.
Sky is the limit humo kaendeleza uongo wake kwamba alikulia maisha ya kimasikini, kasifia kwamba kuuza madawa ya kulevya kuna mkwanja, hakuishia hapo alidanganya kwamba aliacha shule akiwa na miaka 10 ili auze madawa, n.k.