2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Anza kama ulivyoanza na taaluma yako ya urefa.

Hiyo hapo pichani una amua nini?

Na hapo kumbuka kuna favor za Messi na kuna favor za timu.

Faulo 14 hakuna kadi, mwenye faulo 11 ana kadi 5

Kuna vitu hata ukipinga unaweza kujiona mjinga.
Hili kombe lipo kwa ajili ya kumbeba Messi na Argentina
Jamaa linabebwa nje nje na mipenati ya mchongo ambayo anakosa.
 
Hiyo picha sijaiweka kwa bahati mbaya, umeifanya kuwa ajenda kwasababu hujasoma post ambazo nimekujibu.

Huo mtiririko wa matukio wenye aim ya kibiashara na ushabiki ni upi ambao tuki connect na hilo tukio tunapata conclusion ya FIFA kumbeba Olise?

Mfano mimi nikiweka hoja ya Messi na Argentina kubebwa na FIFA naweza ku pointi mapenzi ya raisi wa FIFA kwa Messi.

Infantino alisema anatamani Messi abebe kombe la dunia. (Hii ni average point)

Baada ya kusema kauli hiyo, Argentina alipewa penati 5. Ni idadi ambayo mpaka sasa inashikiliwa na timu moja tu ya Argentina.

Mechi dhidi ya Netherlands Messi aliwakejeli bench la ufundi la Netherlands na hakupewa kadi ya njano, hapa sijahesabia ile handball kabisa (hii nayo ni average point)

Siku 9 kabla ya fainali FIFA na viongozi wa AFA walisaini mkataba wa mabilioni ya fedha yakitumwa kwenye account ambayo sio ya shirikisho la AFA (hii ni big point)

2026 Argentina inapangwa kwenye kundi dhaifu, bado mechi zake zinajaa controversial yenye matukio mengi yanayoibeba Argentina. (Average point)

Mechi dhidi ya Cape Verde, Infantino anaweka wazi mapenzi yake kuwa ameteseka pamoja na mashabiki wenzake wa Argentina. (big point)

Mechi dhidi ya Egypt, bao mbili za kutangulia zinamfanya Infantino akasirike jukwaani. (Average point)

Argentina anafanya comeback na kupata goli la ushindi, Claudio Tapia na Infantino wana hug kwa furaha. (Big point)

Infantino anagundua amefanya mistake anaamua kushika bendera ya Egypt kwenye mechi ya baadaye ili kuua soo kupitia tukio lake alilolionesha kwenye mechi ya Egypt la kukumbatiana na Claudio Tapia baada ya kushindwa kuhimili hisia. (Big point)

Hizi ndio baadhi ya pattern ambazo zinam link FIFA, Infantino kwenye upendeleo wa wazi amaofanyiwa Messi na Argentina.

Wewe hauwezi kuniwekea hii pattern kwa Olise hata kidogo.

Na hiyo nimeifanya tu briefly ila kuna mengi sana nikianza kuandika hapa itachukua muda pengine kuyamaliza.
Duh hii risala hatari, na leo tunawapigia ingetra yenu, kombe hata likienda spain yote sana ni familìa moja hahaaaa, ila first first ni ARG
 
Kwanza Argentina hakupangwa kundi dhaifu bali juhudi zake za kushika nafasi ya kwanza zimemfanya awakwepe vigogo. Hiyo timu unayo ishabikia wewe Ureno, ilipangwa na timu zipi tuanze kwenye Rank za FIFA, tusiongee kwa hisia? Maana hata Ureno angeshika nafasi ya kwanza,basi robo ndio angekutana na timu ngumu ambayo ni Argentina, sasa yeye mwenye kashika nafasi ya pili sasa tutamsaidiaje wakati kazembea mwenyewe.Halafu kwenye michuano hii, timu gani ilipagwa kwenye kundi gumu? Utasema trend najua nyie timu CR7,okay Colombia kashika nafasi ya kwanza, kakutana na Ghana, then akatolewa na Uswizi, Uswizi akakutana na Argentina akapigwa.Okay kwa Trend hii Ureno kama angeshika nafasi ya kwanza si alikuwa anajipigia, ila yy mwenyewe kazingua.
Wapinzani wa Argentina
HatuaMpinzani FIFA Ranking
Kundi JAlgeria28
Kundi JAustria24
Kundi JJordan63
Hatua ya 32Cape Verde67
Hatua ya 16Misri29
Robo FainaliUswisi19


Niambie ni mwaka upi ambao kombe la dunia lilifanyika na ikatokea timu moja inafika robo fainali bila kukutana na timu yeyote kutoka kumi bora ya FIFA ranking?
 
Back
Top Bottom