Swali hujajibu, umejitengenezea swali ambalo umeona ni rahisi halafu ndio umelijibu.
Mimi sijahoji kama Argentina hajawahi cheza na Giant kwenye hiyo miaka 17.
Hoja yangu imelenga utetezi wako wa kwamba Argentina anakutana na timu dhaifu kwasababu inanufaika kupitia matunda ya kuongoza kundi.
Ndio maana nikahoji, katika historia ya miaka 17 ya kombe la dunia ni timu gani nyingine ambayo iliwahi kunufaika kwa kuongoza kundi na kufaidi matunda ya kucheza hadi robo fainali bila kukutana na timu ambazo zipo top ten ya ranking?