2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Bellingham





Replay


Kane offside goal

 
Unasema fifa inahusishwa alafu hapo hapo FBI wao hawajaihusisha. Inahusishwa na nani? Uchunguzi wa awali wa FBI si lazima ungeihusisha fifa sababu walifanya hayo malipo?

Unasema kinachompa title huyo Molina ni uchunguzi wa unyanyasaji wa kijinsia? Nimekuuliza hapo huyo Molina ni nani?
Sababu ya kuuliwa hivi ni kwa kuwa haya yote hakuna jipya, hii issue ya sex abuse ni ya tokea 2022, iweje wewe Leo useme inampa title huyo Molina?

Hii issue ya sex abuse Mbona imeandikwa sana wakati huo, media zimepiga sana kelele kuhusu hii issue, nyie mnaijua Leo?
View attachment 3627371
Nilijua nahojiana na mtu ambaye anaweza kuelewa muktadha.

Ngoja nikuwekee hivi penginne

Kuna utofauti mkubwa kati ya mambo ambayo FIFA inayafanya sasa hivi chini ya kapeti na kile ambacho FBI inaruhusiwa kukiandika kisheria kwenye hatua hii ya uchunguzi wa awali.

Kwenye sheria za Marekani FBI sio rahisi kutaja jina la taasisi kubwa kwenye ripoti za mwanzoni.

Kwenye hili sakata FIFA ni third party aliyetumiwa kupitisha hela, katika hatua za awali za uchunguzi anayetazamwa zaidi ni muhusika mkuu.

Kuhusu Romain Molina na kupata title..

Hapa nilimaanisha aina ya kesi ambayo imo kwenye list ya mambo anayoenda kuyachunguza ni hii kashfa ya unyanyasaji wa kijinsia.

Huyu aliwahi kumbananisha raisi wa shirikisho la soka la Haiti kwenye kashfa za unyanyasaji wa kijinsia. Hii ndio kesi iliyompa heshima na kumfanya ajulikane zaidi

Ndio maana nilipotaja swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa ni miongoni mwa vitu anavyo vichunguza nikasema hili swala limeingia kwenye department yake iliyomtambulisha.

Kupitia hiyo picha yako uliyoweka, unatakuwa ujue kuwa Romain Molina hajaja kufungua kesi upya kama kocha huyo alifanya makosa au la

Hilo lilishatokea, ushahidi wake mpya alioupata kupitia nyaraka za siri zilizovuja unalenga zaidi kuonesha jinsi FIFA na AFA walivyo shughulikia kuzima hiyo kesi.

Romain Molina anadai kuwa ushirikiano huo wa kufunika hii kesi haukufanyika bahati mbaya bali ulikusudiwa kulinda interest za viongozi hao.
 
Back
Top Bottom