2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Nilijua nahojiana na mtu ambaye anaweza kuelewa muktadha.

Ngoja nikuwekee hivi penginne

Kuna utofauti mkubwa kati ya mambo ambayo FIFA inayafanya sasa hivi chini ya kapeti na kile ambacho FBI inaruhusiwa kukiandika kisheria kwenye hatua hii ya uchunguzi wa awali.

Kwenye sheria za Marekani FBI sio rahisi kutaja jina la taasisi kubwa kwenye ripoti za mwanzoni.

Kwenye hili sakata FIFA ni third party aliyetumiwa kupitisha hela, katika hatua za awali za uchunguzi anayetazamwa zaidi ni muhusika mkuu.

Kuhusu Romain Molina na kupata title..

Hapa nilimaanisha aina ya kesi ambayo imo kwenye list ya mambo anayoenda kuyachunguza ni hii kashfa ya unyanyasaji wa kijinsia.

Huyu aliwahi kumbananisha raisi wa shirikisho la soka la Haiti kwenye kashfa za unyanyasaji wa kijinsia. Hii ndio kesi iliyompa heshima na kumfanya ajulikane zaidi

Ndio maana nilipotaja swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa ni miongoni mwa vitu anavyo vichunguza nikasema hili swala limeingia kwenye department yake iliyomtambulisha.

Kupitia hiyo picha yako uliyoweka, unatakuwa ujue kuwa Romain Molina hajaja kufungua kesi upya kama kocha huyo alifanya makosa au la

Hilo lilishatokea, ushahidi wake mpya alioupata kupitia nyaraka za siri zilizovuja unalenga zaidi kuonesha jinsi FIFA na AFA walivyo shughulikia kuzima hiyo kesi.

Romain Molina anadai kuwa ushirikiano huo wa kufunika hii kesi haukufanyika bahati mbaya bali ulikusudiwa kulinda interest za viongozi hao.
Toka mwanzo niliongelea suala la hisia. Alochofanya Molina ni kurudisha Yale ambayo tayari yalishasemwa. Hakuna jipya aliloliongeza hata taarifa yake ya Leo imerudi pale pale, ila hisia zako/zenu ndio zikawatuma kama ni jambo jipya. Hakuna ambacho amesema ni kipya, ndio maana nimekuwekea Hadi media za Argentina na zenyewe zililkalia kooni hilo suala

Kuhusu FBI na Fifa, hakuna popote FBI anaweza kuionea huruma au kuogopa kuihusisha fifa mwanzoni. Punguza hisia na Yale uyatamaniyo
 
Back
Top Bottom