Nilijua nahojiana na mtu ambaye anaweza kuelewa muktadha.
Ngoja nikuwekee hivi penginne
Kuna utofauti mkubwa kati ya mambo ambayo FIFA inayafanya sasa hivi chini ya kapeti na kile ambacho FBI inaruhusiwa kukiandika kisheria kwenye hatua hii ya uchunguzi wa awali.
Kwenye sheria za Marekani FBI sio rahisi kutaja jina la taasisi kubwa kwenye ripoti za mwanzoni.
Kwenye hili sakata FIFA ni third party aliyetumiwa kupitisha hela, katika hatua za awali za uchunguzi anayetazamwa zaidi ni muhusika mkuu.
Kuhusu Romain Molina na kupata title..
Hapa nilimaanisha aina ya kesi ambayo imo kwenye list ya mambo anayoenda kuyachunguza ni hii kashfa ya unyanyasaji wa kijinsia.
Huyu aliwahi kumbananisha raisi wa shirikisho la soka la Haiti kwenye kashfa za unyanyasaji wa kijinsia. Hii ndio kesi iliyompa heshima na kumfanya ajulikane zaidi
Ndio maana nilipotaja swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa ni miongoni mwa vitu anavyo vichunguza nikasema hili swala limeingia kwenye department yake iliyomtambulisha.
Kupitia hiyo picha yako uliyoweka, unatakuwa ujue kuwa Romain Molina hajaja kufungua kesi upya kama kocha huyo alifanya makosa au la
Hilo lilishatokea, ushahidi wake mpya alioupata kupitia nyaraka za siri zilizovuja unalenga zaidi kuonesha jinsi FIFA na AFA walivyo shughulikia kuzima hiyo kesi.
Romain Molina anadai kuwa ushirikiano huo wa kufunika hii kesi haukufanyika bahati mbaya bali ulikusudiwa kulinda interest za viongozi hao.