Kuna kitu ambacho nimeki observe kwa watu wanaosema kuwa Ronaldo sijui amechoka, au sio tishio kwa defenders kwasababu wanamjua udhaifu wake.
Defenders wa mtandaoni wana mawazo tofauti na wale defenders ambao wapo kwenye pitch wakikabiliana na Ronaldo.
Kila mtu mtandaoni humuongelea Ronaldo kama mchezaji asiyekuwa tishio mbele ya mabeki lakini swali linakuja, mbona kwenye kila mechi Ronaldo anayocheza tunaona mabeki zaidi ya watatu wanamzunguka yeye?
Kwamba hii inatokea tu kwa bahati mbaya mchezaji ambaye sio tishio achukue attention kubwa ya mabeki? Au ni kwasababu mabeki wanajua uwezo halisi wa jamaa ndio maana wanafanya kila kitu kuhakikisha hapati fursa?
Jaribu kufikiria tu hata ile freekick ambayo Ronaldo alikuwa nyuma ya mpira, fuatilia muda uliotumika kupanga ukuta mpaka Ronaldo akakasirika? Hayo yangewezekana vipi ikiwa mpigaji wanajua ni mtu ambaye sio tishio?