2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Portugal wanapiga pasi za karibu karibu sizipendi. Hawatengenezi positions wakiwa na mpira, mwenye mpira anampa aliye karibu yake sio aliye position nzuri. Mkakati mbovu huu hauna malengo na mnaweza piga pasi nyingi bila kushambulia na hata ni vigumu kumiliki mpira kwa hivi.
 
Naomba kujua, je mkasa kama wa Bolegun umewahi tokea kwenye WC?
Yaani mchezaji kufutiwa kadi nyekundu kwa ushawishi wa raisi wa nchi. NV aona UEFA wamelalama
 
Kapiga vizuri ila Ronaldo wa zamani pale anamchukua yule beki na kumsogelea zaidi kipa
Ronaldo akifanya jambo zuri ambalo linawa prove wrong kuhusu ubora wake, mnamfananisha na "Ronaldo wa zamani"

Ikitokea bahati mbaya mambo hayajaenda vizuri mnasema "tulisema yule jamaa kachoka hana msaada kwa timu"

Mnavyotoa mifano kwa rejea za miaka ya zamani ni kama kwenye prime yake Ronaldo alikuwa hajawahi fungwa.

Ni kama kwenye hicho kipindi chake cha ubora ambacho mnamfananishia nacho hajawahi kuwa na low performance.

Swali linakuja, katika hicho kipindi mliwahi kumsifia kwa huo ubora?

Jibu ni kwamba hamkuwahi kufanya hivyo kwasababu hata mazuri yake mlikuwa hamyapendi kwasababu tayari mlishachagua upande.

Hii inanipa sababu ya kuona hata hizi criticism zenu hazitakiwi kupewa attention kwasababu hamkuwahi kuukubali ubora wake hata hizo nyakati mnazo zitaja leo kuwa zilikuwa nyakati bora.
 
Portugal wanapiga pasi za karibu karibu sizipendi. Hawatengenezi positions wakiwa na mpira, mwenye mpira anampa aliye karibu yake sio aliye position nzuri. Mkakati mbovu huu hauna malengo na mnaweza piga pasi nyingi bila kushambulia na hata ni vigumu kumiliki mpira kwa hivi.
Spain walitakiwa kuitumia hiyo opportunity kufunga.

Mbona bado nyau nyau?

Mkakati mbovu, halafu mpinzani anashindwa kuona nafasi ya kunufaika kupitia huo udhaifu, hapo nani ni dhaifu?

Au tuseme Spain hawajaweza kuona hiki ulichokiona?
 
Unaangalia kupitia TBC 🤣🤣
Kesho kaandamane tu uwe front
Nipo kwa shemeji kagoma kulipia kinga'muzi napita na TBC tu , nimewakimbiza watoto sebuleni walikuwa wanacheki movie kwenye flash nikatumia udikteta kama Mbappe , bando langu nahifadhi kwa ajili ya kuStream mechi za night Kali nikiwa chumbani kwangu.

Kwenda front siwezi nalinda mbupu zangu kwanza kwa ajili ya manufaa ya baadae
 
Angalieni nafasi hizi wanazokosa Spain japo ni offside ila ziangalieni sana.

Hizi nafasi zimebeba ujumbe mzito sana.

Hawa wanaokosa hizi nafasi ni under 25 ambao wapo kwenye prime yao.

Mzee wa miaka 41 akikosa vile tungesikia "ona tulisema sisi, huyu amechoka"

Tusisikie
 
Back
Top Bottom