Tukio gani katika fainali ambalo uliona kabisa mechi hii ni ya kumbeba Argentina.
Kwangu mimi ni hii penati aliyopewa Argentina baada ya Di Maria kufanya diving
View attachment 3612508
Di Maria ambaye ana rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa Laliga kuongoza kwenye diving za kuwahadaa waamuzi lakini refa pamoja na yote akaweka penati hapa licha ya kwamba replay zilionyesha hakukuwa na contact kati ya Dembele na Di Maria.
View attachment 3612509
Tukio lingine la kustaajabisha lilikiwa ni hili.
Kolo Muani alichezewa faulo mbaya na Otamendi na V.A.R iliamua kuwa ni penati.
View attachment 3612510
Lakini maswali yakawa ni mengi.
Sheria ya faulo inasema kumnyima mpinzani nafasi ya kufunga goli (denying a goal-scoring opportunity) hiyo ni straight red card ukizingatia kwamba Kolo Muani alikuwa ni mtu wa mwisho.
Lakini maamuzi yaliyofanyika ni penati bila hata ya yellow card.
Nyingine ni hii controversial ya offside
View attachment 3612526
Hapa ilikuwa Argentina amefunga goli la 3 katika ET time. Ikaonekana kama kuna offside imefanyika na V.A.R ikatuletea picha ambayo ni hii
View attachment 3612518
Picha ilionesha vidole vya Martinel vilikuwa offside.
Goli likasimama kwakile kilichosemwa kuwa mikono haihusiki kwenye kufunga bao hivyo eneo la mkono halitahesabiwa kama offside.
View attachment 3612520
Lakini ukakasi ulikuja pale watu walipoanza kurejea mechi zilizopita kwenye matukio kama haya namna yakivyoamuliwa.
Mechi ya Croatia na Belgium, Croatia walinyimwa nafasi ya kupata penalti kwasababu V.A.R ilionesha tukio la offside katika build up iliyopelekea tukio la penalti.
Sababu kuu ya tukio kuonekana ni offside ni kwasababu ya mikono kuzidi.
View attachment 3612523
Hizi controversial ndio sababu tunasema World Cup 2022 ilikuwa rigged