2025 na mbeleni

Umeelewa swali lakini?

Umeombwa kifungu cha katiba kinacho back up maelezo yako.

Ni kifungu gani?
Wewe si uko Marekani? Sijawahi kufika Marekani ila najua kuwa Marekani ipo. Sijui kilipo na wala namba yake siijui, ila najua kuwa kipo. Mimi kutokujua namba ya kifungu cha sheria, hakukifanyi kifungu hicho kutokuwepo, kama kipo. Mimi kutokuwahi kuiona Marekani, hakuifanyi Marekani isiwepo,,,,, unanipata?
 
Mimi sipo Marekani. Mimi nipo Ikungulyabashashi, Simiyu.

Weka kifungu cha katiba kinacho back up maelezo yako.

Kama huna, kaa kimya. Kitafute. Ukikipata ndo urudi hapa.

La sivyo, acha uzushi. Mzushi wewe. 🖕🖕
 
Kuna watu watakuwa disappointed sana Magufuli akimaliza muda wake 2025.
Ni wale wanaonufaika na uwepo wake madarakani

Magufuli akitaka kuujuwa unafki wa CCM afanye hizo hila za kuongezewa muda wakati Hussein Mwinyi ameshaandaliwa kuwa Rais wa JMT 2025.

Leo kanisa katoliki limejitenga rasmi na ramli na wanataka faith na science viende pamoja, you know what i mean?
Mnara wa Babeli.
 
Umeelewa swali lakini?

Umeombwa kifungu cha katiba kinacho back up maelezo yako.

Ni kifungu gani?

Kipo, lakini ni wakati tu pale nchi inapokuwa inapigana vita dhidi ya adui. Soma Ibara ya 42(4)!

Hata hivyo, Katiba haijatoa definition ya neno “adui”. Kwa hiyo, it’s wide open to subjective interpretation. Pandemic, famine, other natural calamities, etc. zote zinaweza kutafisriwa kuwa adui.
 
Na ‘kupigana’ ni nini?

‘Vita’ nayo ni nini?
 

Alichomaanisha Rais ni kwamba Kijazi alistaafu, halafu serikali ikampa mkataba wa kuendelea na utumishi.

Hali hiyo huwa inatokea kwa watumishi wa serikali / civil servants ktk nafasi mbalimbali.

Kwa nafasi za KUCHAGULIWA huwa hakuna kuongezewa muda. utumishi wa hukoma baada ya uchaguzi mpya kuitishwa.
 
Muda ni muamuzi mzuri tusubiri.
Ila na nyie CHADEMA muwage na akiba ya maneno mnajimalizaga wee mambo yakienda tofauti na kukumbushwa mnaishia kutukana
 

No decision is valid at all times and under all circumstances! Vipi, umeshasauhau mwaka 2015 jinsi CDM walivyobadili misimamo yao dhidi ya Lowassa?
 
Bunge linaweza kuondoa term limits kwa nafasi ya Rais.

Linaweza kuongeza urefu wa vipindi vya Urais, kwa mfano kutoka miaka 5 kwenda 7.

Au linaweza kufanya yote mawili niliyoeleza hapo juu.
 
No decision is valid at all times and under all circumstances! Vipi, umeshasauhau mwaka 2015 jinsi CDM walivyobadili misimamo yao dhidi ya Lowassa?

Tafuta popote nilipounga mkono huo uhuni wa cdm.
 
Nimekuelewa, ila unachosha akili. Tuna hesabu mihula kwa miaka au? Unapo amua kuongeza siku za utawala, kipi kina ongezeka tofauti na mihula?
 
Mmmmmmh
 
Kwa hiyo tukubali kuwa lolote linawezekana, mfano kwa wakati huu ninaweza sema sitoongeza muda na kipindi changu kikiisha nang'atuka, ila baadae ninaweza sema kwakuwa moja, Mbili na tatu hazijakamilika basi naongeza muda.

Nilichogundua tatizo kubwa halipo kwa viongozi bali lipo kwetu sisi wafuasi au niseme mashabiki wa mtu au chama.
Tunashindwa kuwa na misimamo na zaidi tunaendeshwa na ushabiki.
 
Hapo kwa Bashiru ni nafasi ya kuteuliwa. U Rais ni nafasi ya kuchaguliwa,na ina ukomo wake kikatiba. Uteuzi wa Bashiru ni matakwa ya mtu(Rais),hapakuitishwa kura ya maoni au kujadiliwa na bunge.

Mchakato wa kumuongeza Rais muda utahitaji kura ya maoni ama kupitishwa na bunge. Lakini,hakuna mahali mpaka sasa imetamkwa kuwa Rais ataongezwa muda......ila kauli za WAPUMBAVU wachache waliopo ndani na nje ya CCM kwa manufaa yao wanaosambaza uvumi huu.

Sasa kila kitakachofanyika kinaunganishwa na mpango wa kuongeza muda.
Nadhani kwa mwanaCCM makini atawaza ni namna gani ya kuiongezea muda CCM wa kukaa madarakani na si kumuongeza mtu muda. CCM ina hazina ya viongozi na wenye uwezo wa kuwa marais na wakafanya vizuri na mazuri kuliko hata Magufuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…